Subscribe to receive latest Updates

Online :

You Are Here: Home - - Chatanda ni Tatizo. CCM iwe makini

IDADI YA WATU WALIOSOMA HABARI HII: counter
MBUNGE wa  Viti maalum  Tanga ambaye pia ni Katibu wa CCM MKoa wa Arusha, Mary Chatanda, anazidi kuvuruga watu, sasa baada ya kuwavuruga Chadema na CCM, ameanza kuwashambulia waandishi wa habari na kuwaita wahuni, huku akiwatishia kuwapiga bastola.

Hali hiyo ya kusikitisha imetokea  , wakati  Katibu  huyo  alipoitisha  mkutano na waandishi wa habari, kwenye jengo la CCM Mkoa, ili kuelezea tamko la kamati ya siasa MKoa wa Arusha, kuhusina na vurugu zilizotokea  januari 5 mwaka huu.

Akitoa tamko hilo alianza  kwa kusema, anaipongeza  serikali  kwa kutumia vyombo vya dola yaani Polisi, kudhibiti  wahuni  kwa kutumia jeshi la Polisi, kisha akawageukia waandishi wa habari na kuanza kuwafukuza.

Waandishi  waliofukuzwa na huku akiwatamkia maneno ya kashfa kuwa wameletwa sababu ya kufuata uchumi, ni mwandishi wa gazeti la Mtanzania, Fortunata Ringo, John Shija wa radio MJ, Rose JAkson wa radio Safina na Wankyo Ghati wa radio five na gazeti la Jamb oleo.

Aidha baada ya kuwafukuza hao, Mwenyekiti wa CCM  Mkoa wa Arusha naye alilazimika kuingilia kati na kumsihi  Katibu huyo awaache kwa kuwa waandishi ni kazi yao kuchukua  habari.

Lakini  Chatanda aliendelea kushikilia msimamo wake na kusema hapo siyo mahali pa kupata uchumi, watoke nje na waandishi hao walitoka nje ya  jengo hilo.

NAye Adamu Ihucha wa gazeti la East Africa, akielezea kwa  masikitiko, alisema yeye ni mmojawapo, alipoingia ndani ya kikao hicho, alimuuliza swali Mary Chatanda, kuwa kwanini wanapingana na IGP, kwa sababu IGP alisema kuna askari walitumia nguvu kubwa kupita kiasi na wewe unasema unawapongeza?

 
Mara baada ya swali hilo, Mary Chatanda aliingilia kati na kumkatisha huku akimkejeli mwandishi huyo kuwa, anamshangaa kuvamia mkutano ambao hakualikwa na alikuwa  ametokea wapi.

 "Hivi wewe umetoka wapi? Maana hatukujuwi, sisi tunazungumzia mambo yetu na kunyanyuka kutoka nje ya kikao" alisema Ihucha.

 NAye Paul  Sarwat wa gazeti la Raia Mwema, naye anasikitishw ana kauli za Katibu huyo na kusema awali, alishawahi kumfuata na kumtaka atoe ufafanuzi juu ya habari za CCM, lakini katibu huyo alimjibu kwa kejeli na kumwambia atamchapa makofi akiendelea kuandika habari za CCM.


Alisema Chatanda alimwambia kuwa yeye haoni habari za kuandika sipokuwa habari ni cCM tu, akiendelea atamchapa makofi.

Sarwat alisema kauli kama hizo zinazotolewa na kiongozi mkubwa wa ngazi ya juu ya Mkoa, zinasikitisha sana na zinapaswa kukemewa.

Akizungumzia kuhusu kauli za Mary Chatanda na kuwaukuza  waandishi wa habari, MAkamu Mwenyekiti  wa chama cha waandishi wa habari, APC, Charles Ngereza, alisema yeye amesikitishw ana udhalilishaji wa Mary Chatanda dhidi ya wanahabari.

Alisema kuwa yeye kama kiongozi amekuwa akipata malalamiko  ya mara kwa mara ya waandishi kutolewa vitisho na lugha chafu na Mary Chatanda, hivyo kama waandishi wanasikitika sana na hali hiyo ikiendelea italeta mvurugano mwingine kati ya CCM na waandishi wa habari.

Ngereza alisema kuwa mbali ya kuleta mvurugano, pia itahalalisha viongozi na watu wengine kuwadhalilisha waandishi na hiyo tayari imetokea kwa Polisi  kuwakamata baadhi ya waandishi kama Musa Juma wa MWananchi, ambaye alikamatw ana Polisi na kupigwa, kasha kunywang'anywa Kamera na kulazimishwa kufuta Picha.

Alisema huo ni unyama na kuingilia kazi za waandhishi wa habari, ambao hawana mipaka na kazi zao, hivyo wanaomba serikali na viongozi wa juu, kuingilia kati na kuwakalisha viongozi wa Arusha, ili waheshimu uhuru wa  wanahabari.


Sent from my iPhone
Tags:

3 comments

  1. Anonymous says:

    huyu mary chatanda jeuri yake anatamba kuwa ni shemeji yake rais kikwete kwa kuwa alizunguka na mama salma kikwete katika kampeni za mwaka 2005,hivyo hakuna mtu wa kumbabaisha unaambiwa hata huyo kikwete hapo ndio break,so ndio kinachompa jeuri na kumdharau kila mtu hata mwenyekiti wake wa chama hakohoi kwa chatanda kwanza advertise alimnyang'anya gari,na amekivuruga chama arusha hakuna mwenye hamu nae kwa usalama,mwenyekiti wa ccm taifa busara inahitajika huyu mama hafai kabisa!but bif lake na waandishi amekanyaga pabaya!raia mwema

  2. Anonymous says:

    hivi kweli huyu mary anadhani ccm ni yakwake hadi afukuze waandishi eti wanadhani ccm ni uchumi,huyu mama hafai kuwa kiongozi tatizo ccm inawapa madaraka watu wa darasa la saba ambao upeo wao unaishia hapo kama mary chatanda,anajiona yeye ndio yeye waandishi arusha kama mpo makini susieni kuandika habari za ccm arusha!

  3. Anonymous says:

    mary chatanda umelewa madaraka kama kunamtu anakubeba katika chama anakuharibu na wewe unatumia vibaya madaraka yako mama wewe ni kiongozi na ni kioo cha jamii hukupaswa kupongeza polisi kuuwa na kumwaga damu za watz je angekuwa mmojawapo ni mwanao au ndugu yako ungewapongeza polisi kwa mauaji acha unafiki pumbavu wewe,ni huo ubunge wa viti maalum ndio unakupa kiburi hii dunia tuu wee mama!

Post a Comment