Rais John Magufuli ametoa vitambulisho 670,000 kuwatambua wafanyabiashara wadogo nchini Tanzania kuhakikisha wanafanya shughuli zao bila kusumbuliwa.
Rais ametoa vitambulisho hivyo leo Jumatatu Desemba 10, 2018 kwenye mkutano wake na watendaji wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), wakuu wa mikoa yote nchini humo kujadili namna ya kuboresha mazingira ya ukusanyaji mapato.
Amesema kwa muda mrefu amekuwa akiiagiza TRA pamoja na halmashauri kutowatoza kodi wajasiriamali wadogo ambao mitaji yao haizidi Sh4 milioni lakini utekelezaji wake umekuwa wa kusuasua.
Kila Mkoa utapewa vitambulisho 25,000 na kila mjasiriamali mdogo atalipia Sh20,000 na fedha hiyo kupelekwa TRA.
Kila Mkoa utapewa vitambulisho 25,000 na kila mjasiriamali mdogo atalipia Sh20,000 na fedha hiyo kupelekwa TRA.
Kwa malipo hayo, kila mkuu wa Mkoa atakusanya Sh500 milioni na ikilazimu aagize vitambulisho vingine kwa ajili ya watakaovihitaji.
Rais Magufuli amesema hajaridhishwa na utaratibu wa kuunganisha kitambulisho cha TRA na kile cha Taifa kuwatambua wafanyabiashara wadogo akibainisha baadhi yao kutozwa kodi nje ya maagizo.
“Suala la kuwasajili wafanyabiashara wadogo linaenda polepole sana, tangu nimetoa maagizo kwamba mamalishe na wamachinga wasisumbuliwe. Unakuta mtu ana mtaji usiozidi Sh4 milioni lakini wanasumbuliwa kila siku anatafutwa kulipa kodi na ushuru wa kila aina,” amesema.
Amesema vitambulisho hivyo ni kwa ajili ya kuanzia na endapo kutakuwa na mahitaji zaidi vitatengenezwa kulingana na mahitaji ya mkoa husika.
“Nimeamua kufanya tofauti, nimechapisha vitambulisho mimi mwenyewe. Mfanyabiashara akishavaa kitambulisho hiki asisumbuliwe na mtu yoyote na kwa vile nimekitoa mimi, sioni mtu atakayeenda kumsumbua,” amesema Rais Magufuli.
Katika hatua nyingine, Rais Magufuli ameeleza kutoridhishwa na kiwango cha ukusanyaji wa mapato nchini Thumo huku akitaja baadhi ya sababu zinazochangia kuwa ni viwango vikubwa vya kodi vinavyotozwa na TRA.
Ameitaka TRA pamoja na Wizara ya Fedha na Mipango kuboresha mazingira ya ukusanyaji mapato ikiwamo kodi ya majengo ili ilingane na hali halisi ya maisha ya Watanzania
x
![]() |
| Katibu wa Jumuiya ya Madaktari, Dk Edwin Chitage akitoa tamko la Jumuia hiyo kwa Waandishi wa Habari |
Madaktari hao wa hospitali za Muhimbili, Moi, KCMC, Mbeya, Bugando na Ocean Road ya jijini Dar es Salaam, jana walitangaza rasmi kuwa wameingia kwenye mgomo huo kushinikiza pamoja na mambo mengine, Serikali kutoa tamko kuhusu utata wa tukio hilo.
Tukio hilo la aina yake kutokea nchini, limeathiri upatikanaji wa huduma zote za matibabu katika hospitali hizo, huku madaktari katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na Moi, wakielekeza nguvu zao kunusuru maisha ya mwenzao aliyeumizwa.
Katibu wa Jumuiya ya Madaktari, Dk Edwin Chitage, aliwaambia waandishi wa habari kuwa mgomo huo utaendelea hadi hapo Serikali itakapotekeleza madai yao.
"Tunaitaka Serikali kuacha vitisho kwa madaktari nchini, tunaitaka itambue kwamba mgogoro huu hauwezi kumalizwa kwa njia yoyote vikiwemo vitisho bali ni kwa kukaa meza ya majadiliano na kukubaliana na madaktari," alisema Dk Chitega na kuongeza:
"Ninawashukuru madaktari wote nchi nzima, wauguzi na wafanyakazi wa sekta ya afya kwa ujumla wao kwa kusitisha huduma baada ya kupigwa mwenzetu. Tunaomba mshikamano huu uendelee," alisema Dk Chitega.
Gazeti hili lilishuhudia wagonjwa wakiwa wamekaa katika makundi bila kujua la kufanya, huku wengine wakiamua kuondoka na kwenda hospitali binafsi.
Waliliambia Mwananchi kwamba kitendo alichofanyiwa Dk Ulimboka ni cha kinyama na kuungana na madaktari hao kuitaka Serikali kutatua mgogoro huo haraka.
Wagonjwa waliofika katika eneo hili pia walielezwa bayana na maofisa wa Moi kwamba huduma zimesitishwa kutokana na madaktari kugoma.
Ocean Road
Madaktari bingwa katika Taasisi ya Ocean Road nao waligoma kutoa huduma hatua iliyozua taharuki kwa wagonjwa waliofika kwa ajili ya matibabu.
Gazeti hili lilishuhudia ofisi za madaktari hao zikiwa zimefungwa na hata zile ambazo zilikuwa wazi, madaktari hawakuwapo.
Mmoja wa wagonjwa aliyejitambulisha kwa jina la Joyce Dachi, alisema kuwa, wagonjwa wengi wamekuwa wakiandikishwa mapokezi, lakini wanachukua muda mrefu kumuona daktari.
Mgomo huo pia umeendelea katika Hospitali ya Amana wilayani Ilala huku uongozi wa hospitali hiyo ambao uligoma kuzungumza na vyombo vya habari, ukihaha kunusuru hali hiyo.
Katika Hospitali za Temeke na Mwananyamala huduma ziliendelea kutolewa kama kawaida.
Mbeya
Katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya ,madaktari bingwa ambao awali hawakugoma jana waliingia kwenye mgomo na kusababisha wagonjwa katika hospitali hiyo hususan kitengo cha wazazi, kusota bila matibabu.
Habari kutoka katika hospitali hiyo zilieleza kuwa hivi sasa madaktari bingwa wanatoa huduma kwa kujuana.
Mmoja wa madaktari hao ambaye hakutaka kutajwa gazetini, alisema kitendo alichofanyiwa Mwenyekiti wa Jumuiya yao kimewakatisha tamaa.
Alisema kuwa, hali hiyo sasa imehamia hadi katika Kituo cha Wazazi cha Meta na kufafanua kuwa hali ni mbaya, tayari wajawazito wametakiwa kuhamia katika Hospitali ya Mkoa ambayo imefurika wagonjwa.
Mkurugenzi wa Hospitali hiyo ya Rufaa, Dk Eliuter Samky hakuweza kuzungumzia tukio hilo jana kutokana na kile kilichoelezwa na katibu wake muhtasi kwamba ana kazi nyingi.
Mwanza
Madaktari katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando (BMC) mkoani Mwanza nao wamegoma, huku kiongozi wa Kamati Ndogo ya hospitali hiyo inayoshughulikia migomo, akikataa kuzungumzia hali hiyo.
Akizungumza na Mwananchi kwa njia ya simu baada ya kutoonekana katika maeneo ya hospitali, mmoja wa viongozi wa Kamati hiyo, Dk Geogre Adrian, alisema kwa sasa hawezi kulitolea ufafanuzi suala hilo na kwamba kufanya hivyo, ni kwenda kinyume na maagizo aliyopewa na Kamati Kuu.
Akizungumzia huduma katika hospitali hiyo alisema kuwa hajui lolote kwa kuwa hawajagusa maeneo ya kazi kwani wapo kwenye mgomo.
Kaimu Mkurugenzi wa hospitali hiyo alipotafutwa kwa njia ya simu ili kuzungumzia huduma katika hospitali yake, hakupatikana.
Watimuliwa
Jana Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali hiyo, Dk Charles Majinge alitoa tangazo la kuwataka madaktari waliopo mafunzoni ‘Interns’ katika hospitali hiyo kurejea kazini na kama watakiuka agizo hilo, watakuwa wamejifukuzisha wenyewe.
Manyara
Mkoani Manyara, madaktari kumi katika Hospitali ya Haydom Wilaya ya Mbulu wamegoma tangu juzi.Idadi ya wagonjwa katika hospitali hiyo inayomilikiwa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), inaongezeka siku hadi siku.
Wakizungumza na waandishi wa habari kwa masharti ya kutotaka kutajwa majina yao, madaktari hao ambao wanafanya mafunzo ya vitendo katika hospitali hiyo, wamesema kuwa hawatatibu wagonjwa mpaka madai yao yatekelezwe.
Mkuu wa Wilaya ya Mbulu, Anatory Choya, alithibitisha kutokea kwa mgomo huo na kufafanua kwamba wanaendelea kufanya mazungumzo ili kupata ufumbuzi.
Choya alisema kuwa madaktari wanaoendelea na kazi, wameelemewa kutokana na wagonjwa kuwa wengi.
Alisema kati ya madaktari 11 wanaosoma kwa vitendo hospitalini hapo, mmoja tu anayesomeshwa na hospitali hiyo, ndiye hajagoma.
KCMC
Hali katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC mkoani Kilimanjaro imezidi kuwa tete na kuwafanya ndugu kuwahamishia wagonjwa wao katika hospitali binafsi.
Mwananchi lilitembelea wodi za hospitali hiyo na kukuta vitanda vikiwa wazi.
Wakizungumza na gazeti hili, baadhi ya madaktari ambao wapo kwenye mgomo kwa sharti la kutotajwa majina, walisema hawako tayari kurudi kazini kwa kuhofia usalama wa maisha yao.
Dodoma
Wagonjwa katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma jana walijikuta wakipata taabu baada ya madaktari wa hospitali hiyo kusitisha huduma kwa takriban saa sita kuanzia asubuhi.
Muda wa mchana utoaji huduma katika hospitali hiyo uliendelea ingawa kwa kusuasua.
Tofauti na siku zote, jana chumba cha daktari kilichokuwa wazi ni kimoja tu hali iliyosababisha msongamano mkubwa.
Arusha
Mjini Arusha, madaktari wameendelea na mgomo katika Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru na kusababisha kudorora huduma huku wagonjwa kadhaa wakiondolewa hospitalini hapo.
Mgomo huo, ulianza saa 1 asubuhi hadi saa 6:00 mchana, ambapo madaktari na wauguzi,waligoma kutoa huduma wakitaka kujua hatima ya Dk Ulimboka. Walitaka pia kuzungumza na uongozi wa hospitali hiyo na waandishi wa habari, kuhusu mgogoro wao.
Askari anyimwa huduma
Askari wa Usalama Barabarani ambaye jina lake halikufahamika mara moja ambaye alipata ajali jana, alijikuta akishindwa kuhudumiwa katika hospitali ya Mount Meru na kuondolewa kutokana na mgomo huo.
Askari huyo, aliyevaa sare, alifikishwa hospitalini hapo saa 5:00 asubuhi akiwa kwenye teksi, lakini wauguzi waliokuwa zamu walishauri apelekwe sehemu nyingine.
Hata hivyo, uongozi wa hospitali ya mkoa, ukiongozwa na Mganga Mkuu wa Mkoa, Dk Omar Chande, jana ulifanya kazi ya ziada ya kuwabembeleza madaktari hao, kurejea kazini, kusubiri uamuzi wa Serikali.
Mgomo, Dk Ulimboka
vyateka Bunge
Mgomo wa madaktari na kutekwa kisha kupigwa Dk Ulimboka jana vilitawala mjadala wa Bunge hadi pale Spika Anne Makinda alipotoa mwongozo kwamba suala hilo lisijadiliwe kwani liko mahakamani.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alilazimika kutoa ufafanuzi wa hoja yake aliyoitoa juzi pale alipokuwa akizungumzia mgomo wa madaktari na kuhitimisha kwamba Serikali ilikuwa inajiandaa kutoa kauli na msimamo wake hivyo “liwalo na liwe’.
Pinda alilazimika kutoa maelezo kutokana na swali aliloulizwa na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe aliyetaka kufahamu maana ya kauli ya Waziri Mkuu ambayo aliita kuwa ni nzito na iliyozua mjadala mkali nchini.
Kadhalika, Mbowe alitaka kufahamu hatua ambazo Serikali imechukua kuhakikisha kwamba wananchi wanaendelea kupata huduma za tiba kutokana na kuwapo kwa taarifa kwamba madaktari katika hospitali kadhaa walikuwa wakiendelea na mgomo.
Kadhalika Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu alimuuliza Pinda kwamba haoni kwamba ni busara kujiuzulu wadhifa wake kutokana na ahadi yake kwamba mgomo wa madaktari usingetokea, lakini ahadi hiyo imeshindwa kutekelezeka.
Akimjibu Mbowe, Pinda alikiri kutoa kauli hiyo ndani ya Bunge juzi na kusema alifanya hivyo akiamini kuwa jambo hilo lilikuwa mahakamani na akasema asingeweza kusema jambo lolote kwa kuwa hana tabia ya kuwa na utovu wa nidhamu wa kuingilia mambo ya mahakamani.
Hata hivyo, alijitetea kuwa kabla ya kutoa kauli hiyo bungeni juzi, hakuwa na taarifa kuhusu tukio la kupigwa kwa Ulimboka na akasema kuwa, kauli yake haihusiani kabisa na Serikali kuhusika katika jambo hilo kwa namna yoyote ile.
Waziri Mkuu alisema tayari amekwishaagiza vyombo husika kufanya uchunguzi wa kina na kutoa majibu ya haraka ili wahusika waweze kuchukuliwa hatua stahiki mara moja.
“Kwanza namtakia afya njema ndugu Ulimboka, na mimi nataka Watanzania waamini kuwa tulikuwa katika mazungumzo mazuri na madaktari chini yake Ulimboka hivyo tukio hilo ambalo limetokea katika mazingira magumu limetushtua kweli, kama ni Serikali basi ingekuwa ni Serikali ya ajabu kweli,’’alisema Pinda.
Kuhusu namna ya kusaidia Watanzania wasiathirike na mgomo huo, alisema tayari Serikali imeshaagiza madaktari kutoka wizarani kutumika na kuwaomba waliostaafu kutoa huduma katika kipindi hicho kigumu.
Mkakati mwingine ni pamoja na kutumia hospitali za Jeshi ikiwamo Lugalo waanze kutoa huduma hizo wakati Serikali inaendelea kuzungumza kwa utaratibu na madaktari.
Lissu aliuliza swali la nyongeza kumtaka Pinda kuachia ngazi hali iliyosababisha mvutano kwani Waziri Mkuu alikosoa uulizaji wa swali hilo kuwa halikustahili.
Baada ya kipindi cha maswali na majibu, Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika aliomba mwongozo wa Spika kuhusu suala la madaktari akitaka taarifa ya Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii ambayo ilifanyia kazi suala la mgomo wa madaktari ijadiliwe bungeni.
Hata hivyo, Spika Makinda alisema ripoti hiyo haiwezi kujadiliwa kwani tayari Serikali ilishakabidhiwa kwa ajili ya kuifanyia kazi na kwamba mapendekezo ya Bunge kupitia ripoti hiyo yamefanyiwa kazi kwa kiasi kikubwa.
Habari hii imeandaliwa na Neville Meena na Habel Chidawali, Dodoma, Godfrey Kahango,Mbeya, Joseph Lyimo,Mbulu, Sheilla Sezzy,Mwanza, Rehema Matowo, Moshi, Masoud Masasi,Dodoma, Fidelis Butahe, Geofrey Nyang'oro Dar, Mussa Juma, Arusha, Bakari Kiango na Victoria Mhagama
ASEMA ATAANIKA KILA KITU BAADAYE, ASEMA ACHWE APUMZIKE, MKUU WA JOPO LA MADAKTARI WANAOMTIBU ASEMA ALING'OLEWA KUCHA, MENO MAWILI NA KUPATA MTIKISIKO WA UBONGO
MWENYEKITI wa Jumuiya ya Madaktari aliyetekwa nyara na kuumizwa vibaya usiku wa kumkia juzi, kisha kutupwa Msitu wa Pande, Dk Steven Ulimboka amesema atazungumza kwa kina yote yaliyomsibu baadaye na kuomba sasa aachwe auguze maumivu makali yanayomkabili.
Dk Ulimboka aliokotwa na wasamaria wema juzi asubuhi katika Msitu wa Pande nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam, baada ya kutekwa nyara na watu waliokuwa na silaha akiwa katika Viwanja vya Klabu ya Leaders, Kinondoni.
Jana, Dk Ulimboka ambaye amelazwa Hospitali ya Taifa Muhimbili huku hali yake ikiwa haijatengemaa vyema, alitoa kauli akisema ingawa ana maumivu makali anaendelea vizuri ikilinganishwa na siku ya kwanza.
Dk Ulimboka alitoa kauli hiyo baada ya kutakiwa aeleze mkasa huo uliomfika wa kukamatwa, kuteswa na kutupwa msituni.
Hata hivyo, hadi sasa wingu zito la nani alimteka na watekaji walitaka kujua nini kutoka kwa kiongozi huyo wa madaktari, bado limetanda.
Siri nzito
Akisimulia mkasa huo kupitia Kituo cha Redio cha Clouds FM, Dk Ulimboka alisema, akiwa katika klabu hiyo ya Leaders alipigiwa simu na rafiki yake ambaye alikuwa atokee Tandika na baada ya kumsubiri ndipo alipofika kwenye klabu hiyo, lakini, alianza kujisikia vibaya tofauti na siku nyingine na kuongeza; "Yaani sikuwa na amani."
Alisema, "Mara, katikati ya maongezi tukaona mtu anaongea na simu. Ghafla tukiwa tunasema tuagane, wakaja watu kama watano hivi na bunduki, wakasema wewe na yule bwana mko free (huru), tunakuchukua wewe (Dk Ulimboka)," alieleza na kuongeza:
"Sijakaa sawa, nikaona nimeshaburutwa nikaanguka kwenye lami, wakaniinua na kuniingiza kwenye gari nyeusi, lakini halikuwa na namba."
Hata hivyo, jana Dk Ulimboka hakuonana na mwandishi wa habari hii, badala yake alirekodiwa, na Mwananchi kupata sauti yake akijibu swali kuhusu hali yake na tukio hilo, baada ya uongozi wa Taasisi ya Mifupa Muhimbili (Moi) kuzuia watu kumwona.
Daktari huyo wa magonjwa ya binadamu, amelazwa katika chumba cha Wagonjwa Wanaohitaji Uangalizi Maalumu (ICU).
"Kidogo najisikia nafuu ikilinganishwa na nilivyokuja ingawaje, bado nina maumivu makali. Kwa hivyo, ingependeza niendelee na mapumziko na mtu yeyote anayetaka kuniona pengine hilo jambo lisifanyike sasa. Hivi sasa ni vizuri nipumzike," ilisikika sauti hiyo ya Dk Ulimboka.
Lakini, uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa wodini alikolazwa Dk Ulimboka, kuna ulinzi mkali wa madaktari na hairuhusiwi watu kumwona kiholela siyo tu kwa sababu za kutaka aachwe apumzike, bali pia kutowaamini watu ovyo.
Madaktari wanaolinda eneo hilo walisikika jana wakisema, “Huyu tunamlinda wenyewe na haiwezekani mtu asiyefahamika kuingia humu ndani, na hilo tutahakikisha sisi wenyewe,”alisikika akisema mmoja wa madaktari hao.
Kiongozi jopo la madaktari
Katika hatua nyingine, kiongozi wa jopo la madaktari wanaomuhudumia Dk Ulimboka, Profesa Joseph Kahamba aliwaambia waandishi wa habari kuwa Dk Ulimboka ana majeraha mwili mzima.
“Ingawa kwa sasa anaendelea vizuri, Dk Ulimboka ameumia sana, kwani mwili wake mzima una majeraha kutokana na kupigwa na watekaji hao,”alisema Profesa Kahamba na kuongeza:
“Aliumia mbavuni,kifuani, miguuni, mikononi ambako aling’olewa baadhi ya kucha za vidole na kichwani na kinywani, ambako aling’olewa meno mawili,”alisema.
Alifafanua kwamba, kutokana na maumivu hayo ya kichwa, Dk Ulimboka alipata tatizo la mtikisiko wa ubongo, lakini akasisitiza kuwa madaktari bingwa wanaendelea na harakati za kuokoa maisha yake.
Uongozi wa Moi watoa neno
Uongozi wa Taasisi ya Mifupa (Moi) umeeleza kuwa hali yake inaendelea vizuri ingawa bado amelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi cha taasisi hiyo.
Msemaji wa Moi, Almas Jumaa aliwaambia waandishi wa habari kuwa licha ya hali yake kuendelea vizuri, lakini haingewezekana kwa waandishi wa habari kuingia ndani ya chumba alikolazwa na kumwona Dk Ulimboka.
“Mgonjwa anaendelea vizuri ukilinganisha na jana (juzi), anaongea, anawatambua watu wanaokwenda kumwona, lakini utaratibu wa kwenda kumwona kwa ninyi imeshindikana kwa sababu yupo (ICU) ni chumba chenye utaratibu wake,”alisema Jumaa.
Jumaa aliongeza kwamba ili mtu aweze kuingia wodini analazimika kuvaa vazi maalumu na mavazi yaliyopo, yasingetosha, lakini pia wapo watu wanaoendelea kumpatia huduma ya matibabu.
Tamko la Jumuiya ya Madaktari
Wakati hali ya Dk Ulimboka ikiwa hivyo, madaktari wameipinga tume ya uchunguzi iliyoundwa na Jeshi la Polisi kuchunguza suala hilo, wakidai mazingira ya tukio hayaliondoi jeshi hilo kuhusika.
Katibu wa Jumuiya hiyo, Dk Edwin Chitage aliwaambia waandishi wa habari kuwa wangependa kuundwa kwa tume huru itakayofanya kazi ya kuchunguza tukio hilo na kutoa taarifa kwa umma.
“Madaktari kwa ujumla wetu tunalaani tukio la kutekwa nyara,kupigwa na kutupwa katika Msitu wa Pande, lakini pia hatuna imani na tume iliyoundwa na Jeshi la Polisi kwa sababu mazingira ya tukio hayaondoi kuhusika ama kutohusika kwa jeshi hilo,”alisema Dk Chitage.
Chitage alitoa msimamo wa madaktari kuwa ni kuendelea na mgomo, huku akionya Serikali kuacha vitendo vya kuwatisha, kwa madai kuwa vitendo hivyo haviwezi kuwa suluhu ya mgogoro kati ya pande hizo mbili.
“Kumekuwa na vitisho kwa madaktari katika maeneo mbalimbali nchini, hususan Dodoma, Mbeya, Arusha na Mwanza. Tunaionya Serikali kuacha mara moja na itambue kuwa mgogoro huo hauwezi kumalizwa kwa namna nyingine yoyote bali ni kwa Serikali kutekeleza madai ya madaktari,”alisema Chitega na kuongeza:
“Sisi madaktari kwa umoja wetu, tumechoka kushuhudia Watanzania wakipoteza maisha kwa magonjwa tunayoweza kuyatibu, kufanya kazi katika mazingira magumu huku kukiwa hakuna mipango ya kuboresha mazingira ya kazi, kukosekana kwa dawa na vifaa tiba.”
Mgomo huo wa madaktari leo unaingia siku ya saba tangu ulipotangazwa na mwenyekiti huyo kuwa, ungeanza rasmi Jumamosi iliyopita.
MWENYEKITI wa Jumuiya ya Madaktari aliyetekwa nyara na kuumizwa vibaya usiku wa kumkia juzi, kisha kutupwa Msitu wa Pande, Dk Steven Ulimboka amesema atazungumza kwa kina yote yaliyomsibu baadaye na kuomba sasa aachwe auguze maumivu makali yanayomkabili.
Dk Ulimboka aliokotwa na wasamaria wema juzi asubuhi katika Msitu wa Pande nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam, baada ya kutekwa nyara na watu waliokuwa na silaha akiwa katika Viwanja vya Klabu ya Leaders, Kinondoni.
Jana, Dk Ulimboka ambaye amelazwa Hospitali ya Taifa Muhimbili huku hali yake ikiwa haijatengemaa vyema, alitoa kauli akisema ingawa ana maumivu makali anaendelea vizuri ikilinganishwa na siku ya kwanza.
Dk Ulimboka alitoa kauli hiyo baada ya kutakiwa aeleze mkasa huo uliomfika wa kukamatwa, kuteswa na kutupwa msituni.
Hata hivyo, hadi sasa wingu zito la nani alimteka na watekaji walitaka kujua nini kutoka kwa kiongozi huyo wa madaktari, bado limetanda.
Siri nzito
Akisimulia mkasa huo kupitia Kituo cha Redio cha Clouds FM, Dk Ulimboka alisema, akiwa katika klabu hiyo ya Leaders alipigiwa simu na rafiki yake ambaye alikuwa atokee Tandika na baada ya kumsubiri ndipo alipofika kwenye klabu hiyo, lakini, alianza kujisikia vibaya tofauti na siku nyingine na kuongeza; "Yaani sikuwa na amani."
Alisema, "Mara, katikati ya maongezi tukaona mtu anaongea na simu. Ghafla tukiwa tunasema tuagane, wakaja watu kama watano hivi na bunduki, wakasema wewe na yule bwana mko free (huru), tunakuchukua wewe (Dk Ulimboka)," alieleza na kuongeza:
"Sijakaa sawa, nikaona nimeshaburutwa nikaanguka kwenye lami, wakaniinua na kuniingiza kwenye gari nyeusi, lakini halikuwa na namba."
Hata hivyo, jana Dk Ulimboka hakuonana na mwandishi wa habari hii, badala yake alirekodiwa, na Mwananchi kupata sauti yake akijibu swali kuhusu hali yake na tukio hilo, baada ya uongozi wa Taasisi ya Mifupa Muhimbili (Moi) kuzuia watu kumwona.
Daktari huyo wa magonjwa ya binadamu, amelazwa katika chumba cha Wagonjwa Wanaohitaji Uangalizi Maalumu (ICU).
"Kidogo najisikia nafuu ikilinganishwa na nilivyokuja ingawaje, bado nina maumivu makali. Kwa hivyo, ingependeza niendelee na mapumziko na mtu yeyote anayetaka kuniona pengine hilo jambo lisifanyike sasa. Hivi sasa ni vizuri nipumzike," ilisikika sauti hiyo ya Dk Ulimboka.
Lakini, uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa wodini alikolazwa Dk Ulimboka, kuna ulinzi mkali wa madaktari na hairuhusiwi watu kumwona kiholela siyo tu kwa sababu za kutaka aachwe apumzike, bali pia kutowaamini watu ovyo.
Madaktari wanaolinda eneo hilo walisikika jana wakisema, “Huyu tunamlinda wenyewe na haiwezekani mtu asiyefahamika kuingia humu ndani, na hilo tutahakikisha sisi wenyewe,”alisikika akisema mmoja wa madaktari hao.
Kiongozi jopo la madaktari
Katika hatua nyingine, kiongozi wa jopo la madaktari wanaomuhudumia Dk Ulimboka, Profesa Joseph Kahamba aliwaambia waandishi wa habari kuwa Dk Ulimboka ana majeraha mwili mzima.
“Ingawa kwa sasa anaendelea vizuri, Dk Ulimboka ameumia sana, kwani mwili wake mzima una majeraha kutokana na kupigwa na watekaji hao,”alisema Profesa Kahamba na kuongeza:
“Aliumia mbavuni,kifuani, miguuni, mikononi ambako aling’olewa baadhi ya kucha za vidole na kichwani na kinywani, ambako aling’olewa meno mawili,”alisema.
Alifafanua kwamba, kutokana na maumivu hayo ya kichwa, Dk Ulimboka alipata tatizo la mtikisiko wa ubongo, lakini akasisitiza kuwa madaktari bingwa wanaendelea na harakati za kuokoa maisha yake.
Uongozi wa Moi watoa neno
Uongozi wa Taasisi ya Mifupa (Moi) umeeleza kuwa hali yake inaendelea vizuri ingawa bado amelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi cha taasisi hiyo.
Msemaji wa Moi, Almas Jumaa aliwaambia waandishi wa habari kuwa licha ya hali yake kuendelea vizuri, lakini haingewezekana kwa waandishi wa habari kuingia ndani ya chumba alikolazwa na kumwona Dk Ulimboka.
“Mgonjwa anaendelea vizuri ukilinganisha na jana (juzi), anaongea, anawatambua watu wanaokwenda kumwona, lakini utaratibu wa kwenda kumwona kwa ninyi imeshindikana kwa sababu yupo (ICU) ni chumba chenye utaratibu wake,”alisema Jumaa.
Jumaa aliongeza kwamba ili mtu aweze kuingia wodini analazimika kuvaa vazi maalumu na mavazi yaliyopo, yasingetosha, lakini pia wapo watu wanaoendelea kumpatia huduma ya matibabu.
Tamko la Jumuiya ya Madaktari
Wakati hali ya Dk Ulimboka ikiwa hivyo, madaktari wameipinga tume ya uchunguzi iliyoundwa na Jeshi la Polisi kuchunguza suala hilo, wakidai mazingira ya tukio hayaliondoi jeshi hilo kuhusika.
Katibu wa Jumuiya hiyo, Dk Edwin Chitage aliwaambia waandishi wa habari kuwa wangependa kuundwa kwa tume huru itakayofanya kazi ya kuchunguza tukio hilo na kutoa taarifa kwa umma.
“Madaktari kwa ujumla wetu tunalaani tukio la kutekwa nyara,kupigwa na kutupwa katika Msitu wa Pande, lakini pia hatuna imani na tume iliyoundwa na Jeshi la Polisi kwa sababu mazingira ya tukio hayaondoi kuhusika ama kutohusika kwa jeshi hilo,”alisema Dk Chitage.
Chitage alitoa msimamo wa madaktari kuwa ni kuendelea na mgomo, huku akionya Serikali kuacha vitendo vya kuwatisha, kwa madai kuwa vitendo hivyo haviwezi kuwa suluhu ya mgogoro kati ya pande hizo mbili.
“Kumekuwa na vitisho kwa madaktari katika maeneo mbalimbali nchini, hususan Dodoma, Mbeya, Arusha na Mwanza. Tunaionya Serikali kuacha mara moja na itambue kuwa mgogoro huo hauwezi kumalizwa kwa namna nyingine yoyote bali ni kwa Serikali kutekeleza madai ya madaktari,”alisema Chitega na kuongeza:
“Sisi madaktari kwa umoja wetu, tumechoka kushuhudia Watanzania wakipoteza maisha kwa magonjwa tunayoweza kuyatibu, kufanya kazi katika mazingira magumu huku kukiwa hakuna mipango ya kuboresha mazingira ya kazi, kukosekana kwa dawa na vifaa tiba.”
Mgomo huo wa madaktari leo unaingia siku ya saba tangu ulipotangazwa na mwenyekiti huyo kuwa, ungeanza rasmi Jumamosi iliyopita.
WAZIRI wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo amemkaanga mtangulize wake akisema baadhi ya madudu aliyoyakuta katika wizara hiyo ni makubwa ambayo hawezi kuyasema hadharani.Profesa Muhongo ni miongoni mwa Mawaziri wapywa walioteuliwa Mei 3, mwaka huu kushika wadhifa katika baraza jipya la mawaziri ambapo kabla ya uteuzi huo aliteuliwa kuwa mbunge kupitia viti maalum na Rais.
Profesa Muhongo mwenye taaluma ya Jiolojia alitoa kauli hiyo juzi, alipokuwa akizunguza na wafanyakazi wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) wa mikoa ya Dar es Salaam na Pwani katika mkutano wao uliofanyika katika viwanja vya makao makuu ya Shirika hilo jijini Dar es Salaam.
Katika mkutano huo wafanya kazi walitaja mambo kadhaa yanayolifanya shirika hilo kushindwa kujiendesha kuwa ni pamoja na mikataba mibovu iliyoingiwa na Serikali kwa Kampuni ya kufua umeme na vitendo vya baadhi ya watendaji wizarani ambao hujihusisha na hujuma dhidi ya shirika hilo.
Akijibu hoja mbalimbali za wafanya kazi alisisitiza kuwa, suala la mikataba mibovu iliyoingia na Serikali inajulikana na wananchi wote lakini akasema hata yeye alipoingia wizarani amekuta mambo mabaya ambayo hawezi kuyasema hadharani.
“Ninyi mnazunguzia mikataba mibovu na mnataka tuifute,wafanyakazi wa Tanesco ni watu waliokwenda shule tuongee vitu vinavyowezekana,ile ni mikataba….siyo kwamba mimi natetea mikataba mibovu yapo mambo niliyoyakuta huku ni makubwa hata mimi siwezi kuyasema hadharani”alisema Muhongo na kuongeza:
“Suala la mikataba huwezi kulibadilisha kwani imeshatufunga , Serikalini nne zimeingia mikataba,awamu ya kwanza ya pili ya tatu na hata ya nne, sisi katika awamu yetu tunawaahidi hatuwezi kuingia mikataba mibovu ndio sababu nikagusia kuwa mimi kama waziri siwezi kusaini mkataba wowote unaohusu umeme bila kushirikisha Tanesco,TPDC” alisema Muhongo.
Profesa Muhongo pia alitaja mambo mengine aliyodai ameyakuta wizarani na kuyafanyia kazi katika kipindi kifupi cha siku 18 alizokaa kwenye wadhifa huo kuwa ni pamoja na suala la uhusiano mbovu baina ya wafanya kazi wa wizara hiyo,Samico, Tanesco na TPDC ambapo kila upande unafanya kazi kivyake na kushutumu upande mwingine.
“Nimekuta hakuna ushirikiano baina ya Wizara,TPDC,Samico na ninyi Tanesco,mbaya zaidi kila upande unatupia lawama upande mwingine,nimenza kwa kulifanyika kazi hilo na kuanzia sasa sisi wote ni timu moja kazi yetu ni kuhakiksha tunatoa huduma bora ya umeme kwa watanzania”alisema Muhongo.
Muhongo alisema yeye ameshaanza kazi na moja ya mambo aliyoyafanya ni kurejesha rasimu ya mapendekezo ya muswada wa kurekebisha sheria ya umeme iliyokuwa imeandaliwa bila kushirikisha pande zote zinazohusika na masuala ya umeme ikiwamo Tanesco na TPDC.
“Kuanzia sasa pale wizarani kila kitu kitakuwa wazi,mimi sitasaini mkataba wowote bila kuwashirikisha ninyi,sitaruhusu vitendo vya hujuma na mtu yeyote wala kuruhusu kutungwa kwa sheria bila ya kuwashirikisha”alisema Muhongo.
Kuhusu jitihadi za kutafuta ufumbuzi suala la umeme alisema, kesho Jumanne Maofisa kutoka TPDC,Tanesco na Wazara ya Madini wanatarajia kukutana na Naibu waziri wa Nishati ya umeme , George Simbachewene kujadili na kuandaa mkakati wa kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa tatizo la umeme nchini.
Alitaka wataalamu wa umeme kujadili namna ya kulitoa Taifa katika mtindo wa kutegemea chanzo kimoja cha umeme wa maji na badala yake kuangazia vyanzo vingine ambavyo ni makaa ya mawe na gesi.
Pia waziri huyo alitaja vyanzo vingine kuwa ni umeme wa upepo,Jiothramu na jua ambao alisema vyanzo hivi vikitumika vizuri vitalisaidia taifa.
Katika mkutano huo pia Waziri huoaliwatangazia neema ya kupatikana kwa gesi katika shirika hilo aliposema bombo la kusafirisha gesi linalojengwa kwa sasa ni mali ya serikali.
“Ninachotaka mimi tuache yote yaliyopita kwani tukijikita kushughulika na hayo tunaweza kushindwa kutekeleza hii mipango tuliyojiwekea,hivi sasa bomba la gesi linalojengwa ni mali ya serikali lakini pia Mgodi wa Kiwira taratibu za kuurejesha serikalini zimekamilika na utakuwa chini ya Samico”alisema Muhongo.
Kuhusu mikataba alisema hatua za kufanyia marekebisho mikataba hiyo, zinaendelea ndani ya wizara kama ilivyofanyika kwa ile ya madini ambayo kwa sasa inalipa asilimia 4 ya mirabaha badala ya asilimia tatu ya awali.
Waziri huyo alitaja pia hatua ambazo wizara imefanya kwa sasa kuwa ni kupitia na kubaini namna Kampuni zilivyoingia na kufanya kazi ya kusafirisha gesi ambapo alisema, kuna kampuni nyingi zinazofanya kazi hiyo.
Wafanya kazi na wizara
Wafanya kazi katika mkutano huo walitaja mambo waliyodai ni kero kwao na yanayoangamiza Shirika hilo ikiwamo mikataba ya kuuziana umeme kwa bei kubwa na kuuza kwa bei ndogo.
Mmoja wa wafanyakazi hao, Kamil Mwalangwa kutoka kituo cha kuzalisha umeme wa Mega watts 100 alisema:
”Katika kituo cha Mg 100 kuna makundi manne yanayonunua gesi kwa ajili ya kuzalisha umeme,Kampuni ya Tegeta,Simbion, Songas na sisi Tanesco,lakini sisi bei tunayouziwa ni kubwa tofauti na wenzetu,nini sababu inayotufanya tununue kwa bei ya juu?alihoji na kuongeza:
“Mheshimiwa Waziri pamoja na kununua kwa bei hiyo wakati mwingine sisi huamuriwa kuzima mashine zote ili kampuni nyingine ziweze kuzalisha na kuuza umeme na maagizo haya hutoka ngazi za juu”alisema Mwalangwa huku akishangiliwa na wafanya kazi wengine.
Alisema kwa sasa muda wa matengezo wa injini zinazofanya kazi katika eneo hilo umepita na shirika halina vifaa vya ziada (spea)wala fedha za kununulia jambo alilodai ni hatari na wakati wowote mitambo hiyo inaweza kuzima na kuongeza tatizo la umeme nchini.
Mwalangwa litaja tatizo jingine litakalolikumba Shirika hilo kuwa ni kuharibika kwa mitambo kutokana na kuwasha na kuzima kila wakati kwa lengo la kupisha mitambo ya kampuni nyingine kuwasha mitambo yao na kuuza umeme.
Alison Mwambaga mmoja wa wafanyakazi wa Tanesco , alipendekeza kwa waziri huyo mwenye dhamana kufuta mikataba yote mibovu ukiwamo wa IPTL kwa kuwa ndiyo inayoliangamiza shirika hilo na Taifa kwa jumla.
SAKATA la Mbunge wa Maswa Mashariki, John Shibuda kutangaza nia ya kuwania urais ndani ya Kikao cha Halmashauri Kuu (Nec) ya CCM, sasa linaitikisa Chadema baada ya Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la chama hicho (Bavicha), Joliana Shonza kupingana hadharani na bosi wake, John Heche.
Wakati Heche akiwa tayari ametoa tamko kumshambulia Shibuda akisema chama hicho hakitaruhusu mgombea wake urais atangaze nia kwenye vikao vya CCM, Shonza ameibuka na kusema tamko hilo la bosi wake siyo la Bavicha ila ni lake binafsi.
Jana, Shonza akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam, alilikana tamko la Heche wiki iliyoipita akisema hakuna kikao ambacho baraza hilo lilikaa na kutoa kauli moja kumjadili Shibuda.
Hii ni mara ya tatu kwa Shibuda kusababisha mgongano ndani ya Chadema. Aliwahi kupinga msimamo wa kutotambua matokeo ya urais wa Jakaya Kikwete na badala yake, alishiriki tafrija Ikulu ndogo Chamwino, baada ya mkuu huyo wa nchi kuzindua Bunge la 10 na pia, aliwahi kupinga msimamo wa chama hicho kukataa posho bungeni badala yake alitaka ziongezwe hadi Sh500,000 huku akiziita ni, “ujira wa mwiha” na kuwarushia makombora baadhi ya viongozi wake akisema ni wabunge wafanyabiashara.
Katika sakata hilo la sasa, Shonzi alisema: “Naomba ifahamike kwamba tamko alilolitoa Heche siyo la Baraza, bali ni lake kama Heche. Alipokuwa akitoa tamko hilo hakukuwa na kikao chochote cha Baraza cha viongozi wa kitaifa wala Sekretarieti ya Baraza la Vijana la Chadema ili kulijadili suala hili kwa kina bali, alitumia mwamvuli wa vijana kuhalalisha hoja yake.”
Shonza alisema tamko alilolitoa dhidi ya Shibuda liliandaliwa na kuandikwa na Ofisa Habari wa Chadema Makao Makuu, kitu ambacho ni kinyume na utaratibu na kanuni za Bavicha.
“Bavicha tumejikamilisha kwa maana ya kwamba, tuna uongozi wetu kamili wa taifa. Tuna ofisi zetu ambazo ni nje ya ofisi za makao makuu sasa iweje tamko hilo likaandaliwe makao makuu tena na mtu ambaye hahusiki na Bavicha?”
Shonza alisema kama utaratibu huo alioutumia Heche ungekuwa unatumiwa na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa na Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe kufanya uamuzi binafsi pasipo kuyajadili na sekretarieti ya chama, wasingeweza kufikia matunda yanayoonekana hivi sasa.
Msimamo wa Heche
Wakati Makamu huyo akimrushia makombora bosi wake, jana Heche naye alitoa tamko akisema: “Natoa taarifa kwa umma kwamba baada ya mashauriano, Katibu wa Bavicha, Deogratias Siale ameitisha kikao cha sekretariati taifa Alhamisi, Mei 24, 2012, kwa ajili ya kujadili na kuwasilisha mapendekezo kwenye vikao halali vya chama kwa ajili ya hatua zaidi.”
Aliongeza, “Wakati huohuo, nimejulishwa kuwa Makamu wangu (Shonza), leo amezungumza na vyombo vya habari na kukanusha taarifa niliyotoa kwa niaba ya Bavicha. Itambulike kuwa majukumu na mamlaka ya mwenyekiti na kiongozi mwingine yeyote wa Baraza yanabainishwa na Kanuni za Baraza letu kifungu 5.4.1, ambayo mwenyekiti ndiye msemaji mkuu wa Baraza na pia ndiye kiongozi mkuu wa Baraza katika ngazi husika.”
Alisema kifungu cha 5.4.2 kinabainisha majukumu ya makamu mwenyekiti ambaye anapaswa kufanya kazi chini ya mwenyekiti na ndiye msaidizi wake.
Alisema Katiba ya chama ambayo ndiyo msingi mama wa shughuli za Baraza katika kanuni zake kifungu cha 7.7.1, inabainisha kazi za mwenyekiti na pia anaweza kufanya nini na wakati gani kwa kushauriana na nani.
“Kwa kutumia kifungu hiki, nilipokea ushauri kutoka kwa viongozi mbalimbali wa Bavicha, akiwemo makamu mwenyekiti na kushauriana na Katibu na kuona haja ya kutoa kauli na mwongozo wa nini kitafuata kwa niaba ya baraza kama hatua ya kwanza,” alisema na kuongeza:
Bavicha Shinyanga
Bavicha Mkoa wa Shinyanga nalo jana limetoa tamko na kumkosoa Shibuda. Tamko hilo lililotolewa na Mwenyekiti wake, Nzemo Renatus, lilisema: “Tatizo letu na Shibuda ni kutoa kauli hii huku katiba ya Chadema na taratibu zake anazifahamu.
Lakini mbaya zaidi anakidhalilisha chama kwa kutoa kauli nzito katika kikao cha mahasimu wetu wakuu wa kisiasa, CCM huku akiwa mwanachama wetu. Ni sawa na mvuvi anayetoboa mtumbwi wake mwenyewe akiwa katikati ya Ziwa au Bahari.”
“Kwa niaba ya Bavicha Mkoa wa Shinyanga, naungana na kauli ya Mwenyekiti wa Bavicha Taifa. Tunaomba aitishe kamati ya utendaji ya Taifa haraka iwezekanavyo tuweze kupitisha maazimio ya kauli tatanishi za Mbunge Shibuda.”
WAZIRI wa Ushirikiano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Samwel Sitta amesema taifa linakabiliwa na viongozi wenye sura mbili ambao ni wale wasio waadilifu wanaofikiri kwa kutumia matumbo kwa kujilimbikizia mali na viongozi wachache wanaofikiri kwa ajili ya kuwatumikia wananchi.
Sitta alisema hayo alipokuwa akitoa mada katika katika maadhimisho ya Siku ya Sheria kwa wanafunzi wa vyuo vikuu nchini, alipozungumza na Jumuiya ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Tumaini, mjini Iringa (IUCo) jana.
Mada hiyo ilihusu mbinu za kisheria na utoaji wa huduma za kisheria Tanzania, ambapo Sitta alisema matatizo ambayo yanayolikabili taifa yanatokana na sura za viongozi wanaoliongoza.
Akifafanua, alisema wapo baadhi ya viongozi wabinafsi na wasio waadilifu ambao mara zote wamekuwa wakifikiri namna ya kujilimbikizia mali badala ya kuwatumikia watanzania.
“Msishangae, tuna viongozi wenye sura mbili, wapo wanaofikiri kwa kutumia matumbo yao jinsi ambavyo wataneemeka na kujinufaisha wenyewe, hawa ni wale wabinafsi lakini wapo viongozi ambao wanatumia ubongo katika kufikiri jinsi ambavyo watatumia uwezo wao wote katika kuwatumikia wananchi, mimi ni miongoni mwa hawa,” alisema Sitta.
Alisema taifa lina kazi kubwa ya kufikiri jinsi ya kumpata Rais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, kwa madai kuwa ana kazi kubwa ya kuliondoa taifa mahali ambako limefikia kwa sasa sambamba na kuvunja makundi yote yaliyopo.
Alidai kuwa imefika wakati ambao lazima viongozi waweke bayana mali wanazomiliki ili wananchi wazitambue na kuwapima viongozi hao kulingana na kipato chao.
Aliongeza kuwa viongozi wengi wamesahau falsafa ya ‘Utu na Usawa’ iliyoanzishwa na hayati Mwalimu Julius Nyerere wakati wa uhai wake, jambo ambalo limesababisha kuwepo kwa tabaka kubwa miongoni mwa jamii.
Alisema wakati akiwa Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, anajivunia jinsi ambavyo Bunge hilo liligeuka la wananchi na kuwajibika pale lilipotakiwa kufanya hivyo.
Kuhusu azimio la Arusha, Sitta alisema kuwa lilikuwa na umuhimu wake kwani lilionyesha namna kiongozi anapaswa kuwajibika, kwa ajili ya kuwatumikia wananchi.
Akizungumzia Jumuiya ya Afrika Mashariki, Sitta aliwataka watanzania kuondoa hofu juu ya kuwepo kwa soko la pamoja la jumuiya hiyo kwa madai kuwa tayari yameandaliwa mazingira mazuri ambayo yatawawezesha wananchi kuwepo katika soko hilo bila wasiwasi.
Alisema wapo katika majadiliano juu ya kuanzishwa kwa shirikisho la kisiasa ambapo tayari baadhi ya wanasheria wameajiriwa kwa ajili ya kushughulikia jambo hilo.
Aidha aliwataka vijana kujiamini na kutoogopa kuomba kazi katika nchi yoyote ndani ya jumuiya hiyo, badala ya kuendelea kunung'unika juu ya kukosekana kwa ajira.
Kwa upande wake, Mkuu wa Kitivo cha Sayansi ya Jamii, Profesa Seth Nyagawa alisema njia pekee ya kuwakomboa watanzania katika umaskini ni kuwanoa ili waweze kuingia kiuhakika katika soko la pamoja la Afrika Mashariki, ikiwemo kuwaandaa kielimu.
Awali, mmoja wa wakufunzi wa Sheria chuoni hapo, Edward Nduguru alisema matatizo mengi yanayowakabili watanzania kwa sasa yanaweza kumalizwa na watanzania wenyewe pale watakaposhirikishwa katika maamuzi huku akiishauri Tume ya Katiba mpya kuhakikisha inakusanya maoni kwa makundi yote.
Sitta alisema hayo alipokuwa akitoa mada katika katika maadhimisho ya Siku ya Sheria kwa wanafunzi wa vyuo vikuu nchini, alipozungumza na Jumuiya ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Tumaini, mjini Iringa (IUCo) jana.
Mada hiyo ilihusu mbinu za kisheria na utoaji wa huduma za kisheria Tanzania, ambapo Sitta alisema matatizo ambayo yanayolikabili taifa yanatokana na sura za viongozi wanaoliongoza.
Akifafanua, alisema wapo baadhi ya viongozi wabinafsi na wasio waadilifu ambao mara zote wamekuwa wakifikiri namna ya kujilimbikizia mali badala ya kuwatumikia watanzania.
“Msishangae, tuna viongozi wenye sura mbili, wapo wanaofikiri kwa kutumia matumbo yao jinsi ambavyo wataneemeka na kujinufaisha wenyewe, hawa ni wale wabinafsi lakini wapo viongozi ambao wanatumia ubongo katika kufikiri jinsi ambavyo watatumia uwezo wao wote katika kuwatumikia wananchi, mimi ni miongoni mwa hawa,” alisema Sitta.
Alisema taifa lina kazi kubwa ya kufikiri jinsi ya kumpata Rais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, kwa madai kuwa ana kazi kubwa ya kuliondoa taifa mahali ambako limefikia kwa sasa sambamba na kuvunja makundi yote yaliyopo.
Alidai kuwa imefika wakati ambao lazima viongozi waweke bayana mali wanazomiliki ili wananchi wazitambue na kuwapima viongozi hao kulingana na kipato chao.
Aliongeza kuwa viongozi wengi wamesahau falsafa ya ‘Utu na Usawa’ iliyoanzishwa na hayati Mwalimu Julius Nyerere wakati wa uhai wake, jambo ambalo limesababisha kuwepo kwa tabaka kubwa miongoni mwa jamii.
Alisema wakati akiwa Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, anajivunia jinsi ambavyo Bunge hilo liligeuka la wananchi na kuwajibika pale lilipotakiwa kufanya hivyo.
Kuhusu azimio la Arusha, Sitta alisema kuwa lilikuwa na umuhimu wake kwani lilionyesha namna kiongozi anapaswa kuwajibika, kwa ajili ya kuwatumikia wananchi.
Akizungumzia Jumuiya ya Afrika Mashariki, Sitta aliwataka watanzania kuondoa hofu juu ya kuwepo kwa soko la pamoja la jumuiya hiyo kwa madai kuwa tayari yameandaliwa mazingira mazuri ambayo yatawawezesha wananchi kuwepo katika soko hilo bila wasiwasi.
Alisema wapo katika majadiliano juu ya kuanzishwa kwa shirikisho la kisiasa ambapo tayari baadhi ya wanasheria wameajiriwa kwa ajili ya kushughulikia jambo hilo.
Aidha aliwataka vijana kujiamini na kutoogopa kuomba kazi katika nchi yoyote ndani ya jumuiya hiyo, badala ya kuendelea kunung'unika juu ya kukosekana kwa ajira.
Kwa upande wake, Mkuu wa Kitivo cha Sayansi ya Jamii, Profesa Seth Nyagawa alisema njia pekee ya kuwakomboa watanzania katika umaskini ni kuwanoa ili waweze kuingia kiuhakika katika soko la pamoja la Afrika Mashariki, ikiwemo kuwaandaa kielimu.
Awali, mmoja wa wakufunzi wa Sheria chuoni hapo, Edward Nduguru alisema matatizo mengi yanayowakabili watanzania kwa sasa yanaweza kumalizwa na watanzania wenyewe pale watakaposhirikishwa katika maamuzi huku akiishauri Tume ya Katiba mpya kuhakikisha inakusanya maoni kwa makundi yote.
MARA baada ya Rais Jakaya Kikwete mwishoni mwa wiki iliyopita kulisuka upya baraza lake la mawaziri kwa kuwatosa…
Aliyekuwa Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo.
Aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige.
Na Elvan Stambuli
MARA baada ya Rais Jakaya Kikwete mwishoni mwa wiki iliyopita kulisuka upya baraza lake la mawaziri kwa kuwatosa mawaziri sita kati ya wanane waliokuwa wametajwa kwa kashfa mbalimbali katika ripoti ya Mdhibiti Mkuu na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG), mawaziri wawili wamo mbioni kushitakiwa kortini.
Habari kutoka ndani ya serikali zinasema tayari maofisa wa serikali wanaandaa makabrasha ya kuwafikisha mahakamani maofisa kadhaa akiwemo aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige na aliyekuwa Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo.
Habari kutoka ndani ya serikali zinasema tayari maofisa wa serikali wanaandaa makabrasha ya kuwafikisha mahakamani maofisa kadhaa akiwemo aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige na aliyekuwa Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo.
MUSTAFA MKULO
Mkulo ndiye aliyekuwa waziri wa kwanza kutakiwa na wabunge ajiuzulu kwa kutuhumiwa kuvunja Bodi ya Shirika Hodhi la Mashirika ya Umma (CHC) ili kuficha tuhuma zake ikiwamo uuzaji wa kiwanja Na.10 kwa Kampuni ya Mohamed Enterprises (MeTL).
Ukaguzi wa CAG ulibaini kuwa Ofisi ya Msajili wa Hazina na Wizara ya Fedha zilihusika moja kwa moja katika uuzwaji wa kiwanja hicho Na.10 kilichopo kando ya Barabara ya Nyerere bila kuishirikisha bodi ya CHC.
Aidha, CAG alibaini kuwapo kwa matatizo katika hati ya madai ya Shilingi bilioni 2.4 kutoka katika Kampuni ya DRTC kama gharama za ulinzi na tozo la matumizi ya barabara ya kuingilia kwenye Kiwanja Na.192 kando ya Barabara ya Nyerere.
Upungufu pia ulionekana kwenye uuzwaji wa jengo la Kampuni ya Tanzania Motors (TMC) lililopo kiwanja Na.24 kilichopo katika eneo la viwanda la Chang’ombe kwa Kampuni ya Maungu Seed.
Mkulo ndiye aliyekuwa waziri wa kwanza kutakiwa na wabunge ajiuzulu kwa kutuhumiwa kuvunja Bodi ya Shirika Hodhi la Mashirika ya Umma (CHC) ili kuficha tuhuma zake ikiwamo uuzaji wa kiwanja Na.10 kwa Kampuni ya Mohamed Enterprises (MeTL).
Ukaguzi wa CAG ulibaini kuwa Ofisi ya Msajili wa Hazina na Wizara ya Fedha zilihusika moja kwa moja katika uuzwaji wa kiwanja hicho Na.10 kilichopo kando ya Barabara ya Nyerere bila kuishirikisha bodi ya CHC.
Aidha, CAG alibaini kuwapo kwa matatizo katika hati ya madai ya Shilingi bilioni 2.4 kutoka katika Kampuni ya DRTC kama gharama za ulinzi na tozo la matumizi ya barabara ya kuingilia kwenye Kiwanja Na.192 kando ya Barabara ya Nyerere.
Upungufu pia ulionekana kwenye uuzwaji wa jengo la Kampuni ya Tanzania Motors (TMC) lililopo kiwanja Na.24 kilichopo katika eneo la viwanda la Chang’ombe kwa Kampuni ya Maungu Seed.
EZEKIEL MAIGE
Maige akiwa Waziri wa Maliasili na Utalii ripoti ya CAG ilieleza kuwa ofisi yake ilipoteza Shilingi 874,853,564 baada ya kufanya uamuzi wa upendeleo wa kutoa kiwango cha chini cha mrahaba kwa mauzo ya misitu.
Katika kipindi cha ukaguzi wa hesabu za Shirika la Hifadhi ya Taifa Tanzania (Tanapa) ilibainika kuwa shirika liliingia katika mkataba na Kampuni ya CATS Tanzania LTD unaohusiana na matengenezo ya kawaida, ufungaji wa vifaa vya mawasiliano na vifaa vingine katika mkataba wa jumla ya dola milioni moja za Marekani.
Alishutumiwa kwa kutengeneza mazingira ya rushwa katika ugawaji wa vitalu vya uwindaji, ugawaji ambao inadaiwa ulitawaliwa na dosari nyingi ikiwa ni pamoja na kutangaza majina ya waliopata vitalu bila kuonyesha ni vitalu vipi walivyopewa. Aidha, Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi na Maliasili ilieleza kuwa kampuni 16 zilizopewa vitalu hivyo hazikuomba na kwamba vitalu hivyo vilikuwa vya daraja la kwanza na la pili.
Mbali na tuhuma hizo, Maige hivi karibuni alidaiwa kununua nyumba kwa Dola za Marekani 700,000 iliyopo Mbezi Beach jijini Dar es Salaam, tuhuma ambazo alizipinga na kusema kuwa nyumba hiyo ameinunua kwa Dola 410,000, (sawa na zaidi ya shilingi milioni 600 za Kitanzania).
Habari za ndani kutoka serikalini zilizotufikia zinasema mara baada ya Rais Kikwete kutoa tamko la wahusika wa ubadhirifu huo ‘washughulikiwe’, tayari nyaraka mbalimbali zimeanza kushughulikiwa na vyombo vya dola ili kuona nani aliiba na nani hahusiki. Waliokuwa mawaziri na kutemwa nao wanamulikwa na vyombo vya sheria.
WOTE KUSHITAKIWA
Mwenyekiti wa Democratic Party, (DP), Christopher Mtikila amesema hivi sasa anaandaa mashitaka kwa mawaziri wote wanane walioonekana na Bunge kuliingiza taifa katika hasara kubwa.
“Mbona Amatus Liyumba aliyekuwa Mkurugenzi wa Utawala wa Benki Kuu ya Tanzania alishitakiwa kwa matumizi mabaya ya ofisi, hawa wote tutawashitaki, tuache tabia ya kipumbavu ya kupendeleana,” alisema Mtikila jana alipoongea na mwandishi wetu.
Maige akiwa Waziri wa Maliasili na Utalii ripoti ya CAG ilieleza kuwa ofisi yake ilipoteza Shilingi 874,853,564 baada ya kufanya uamuzi wa upendeleo wa kutoa kiwango cha chini cha mrahaba kwa mauzo ya misitu.
Katika kipindi cha ukaguzi wa hesabu za Shirika la Hifadhi ya Taifa Tanzania (Tanapa) ilibainika kuwa shirika liliingia katika mkataba na Kampuni ya CATS Tanzania LTD unaohusiana na matengenezo ya kawaida, ufungaji wa vifaa vya mawasiliano na vifaa vingine katika mkataba wa jumla ya dola milioni moja za Marekani.
Alishutumiwa kwa kutengeneza mazingira ya rushwa katika ugawaji wa vitalu vya uwindaji, ugawaji ambao inadaiwa ulitawaliwa na dosari nyingi ikiwa ni pamoja na kutangaza majina ya waliopata vitalu bila kuonyesha ni vitalu vipi walivyopewa. Aidha, Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi na Maliasili ilieleza kuwa kampuni 16 zilizopewa vitalu hivyo hazikuomba na kwamba vitalu hivyo vilikuwa vya daraja la kwanza na la pili.
Mbali na tuhuma hizo, Maige hivi karibuni alidaiwa kununua nyumba kwa Dola za Marekani 700,000 iliyopo Mbezi Beach jijini Dar es Salaam, tuhuma ambazo alizipinga na kusema kuwa nyumba hiyo ameinunua kwa Dola 410,000, (sawa na zaidi ya shilingi milioni 600 za Kitanzania).
Habari za ndani kutoka serikalini zilizotufikia zinasema mara baada ya Rais Kikwete kutoa tamko la wahusika wa ubadhirifu huo ‘washughulikiwe’, tayari nyaraka mbalimbali zimeanza kushughulikiwa na vyombo vya dola ili kuona nani aliiba na nani hahusiki. Waliokuwa mawaziri na kutemwa nao wanamulikwa na vyombo vya sheria.
WOTE KUSHITAKIWA
Mwenyekiti wa Democratic Party, (DP), Christopher Mtikila amesema hivi sasa anaandaa mashitaka kwa mawaziri wote wanane walioonekana na Bunge kuliingiza taifa katika hasara kubwa.
“Mbona Amatus Liyumba aliyekuwa Mkurugenzi wa Utawala wa Benki Kuu ya Tanzania alishitakiwa kwa matumizi mabaya ya ofisi, hawa wote tutawashitaki, tuache tabia ya kipumbavu ya kupendeleana,” alisema Mtikila jana alipoongea na mwandishi wetu.
BAADA ya kufanya mabadiliko kwenye Baraza lake la Mawaziri, Rais Jakaya Kikwete sasa anatarajia kuifumua sekretarieti ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Tanzania Daima Jumatano imebaini.
Vyanzo vya habari kutoka ndani ya CCM, vilisema kuwa Rais Kikwete ambaye ni mwenyekiti wa chama hicho taifa, ameamua kuitisha vikao vya chama ghafla pamoja na mambo mengine, kufanya mabadiliko kwenye sekretarieti yake.
Duru za kisiasa kutoka ndani ya chama hicho tawala, zilisema kuwa mabadiliko hayo yanatokana na mmoja kati ya wajumbe wa sekretarieti, Januari Makamba, kuteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Sayansi Teknolojia na Elimu ya Juu.
“Kama utakumbuka mara ya mwisho Rais Kikwete aliamua kuwaondoa mawaziri wote kwenye sekretarieti ya chama ili wajumbe hao waweze kufanya kazi muda wote. Alimwondoa Waziri Bernard Membe, Nape akalazimika kuachia u-DC. Kwa vile Makamba amekuwa waziri ni wazi kwamba ataachia nafasi hiyo na Rais ataijaza kwa kumteua mjumbe mwingine,” kilisema chanzo chetu cha habari.
Wajumbe wengine wa sekretarieti hiyo ni pamoja na Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, Mhasibu Mkuu, Mwigulu Nchemba, Martin Shigela, Amina Makilage, Katibu Mkuu Jumuiya ya Wazazi, Katibu wa Wabunge wa CCM, Jenister Mhagama, John Chiligati, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Vuai Ali Vuai, Asha Juma na Katibu Mkuu, Willson Mkama.
Katika kujaza nafasi hiyo, Rais Kikwete anaweza kuwagusa wajumbe wengine kama ataona kuna ulazima wa kufanya hivyo.
Ukiachia mabadiliko hayo, vikao hivyo vya CCM ambavyo vinaanza Mei 11 hadi 14, vinajadili mambo mbalimbali, ikiwemo hali ya kisiasa ndani ya chama hicho hasa kipindi hiki ambapo kinakabiliwa na kukimbiwa na wimbi la wanachama wake.
“Kuna mambo mazito ya kujadili. Kasi ya CHADEMA na ushindi wake Arumeru imeibua hofu, wimbi la wanahama wa CCM kuhamia CHADEMA, mpasuko ndani ya chama, suala la uchaguzi wa chama na mjadala wa Katiba ni baadhi ya mambo yatakayoibua mjadala mzito,” alisema mtoa habari wetu.
Mtoa habari wetu alisema kuwa kikao hicho pia kinaweza kuwaweka kiti moto wabunge wa CCM walioungana na wenzao wa upinzani kutia saini za kutokuwa na imani na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
Kwa mujibu wa ratiba ya vikao hivyo kuanzia jana hadi Mei 11 kutakuwa na vikao vya maandalizi, Kamati ya Maadili kukutana Mei 12 asubuhi na Kamati Kuu (CC) chini ya Rais Kikwete itakutana siku hiyohiyo jioni.
Mei 12 kutakuwa na semina maalumu kwa wajumbe wote wa CC na NEC na Mei 14 itakuwa siku ya NEC.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma, Nape alisema kuwa vikao hivyo ni maalumu kwa ajili ya wajumbe kujadili mjadala wa Katiba mpya.
Alipoulizwa kama kuna hatua zozote ambazo zitachukuliwa na kwa baadhi ya wabunge waliosaini fomu ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu, Nape alisema hoja hiyo haipo na haiwezi kuwepo kwani wabunge hao walitoa haki yao Kikatiba kuwawakilisha wananchi wao.
“Kwanza ikumbukwe kuwa Rais akiwa Tanga aliwapongeza wabunge kwa kuonyesha msimamo wao leo itakuwaje Rais tena awageuke na kuanza kuwawajibisha? Hilo halipo kabisa!” alisema.
Katika hatua nyingine, Nape alisema mawaziri wote waliotuhumiwa wawajibishwe kwa uzito wa makosa yao kama watabainika kuhusika.
“Hakuna mtu aliye juu ya sheria, kama mawaziri wanaotuhumiwa kufanya ubadhirifu wako ndani ya Baraza la Mawaziri au wale walioachwa ni lazima kila mmoja achukuliwe hatua kadiri ya kosa lake, kama leo hii Rais mstaafu Benjamin Mkapa kafikishwa mahakamani kwa ajili ya kutoa ushahidi itakuwa Baraza la Mawaziri?” alihoji Nape.
Vyanzo vya habari kutoka ndani ya CCM, vilisema kuwa Rais Kikwete ambaye ni mwenyekiti wa chama hicho taifa, ameamua kuitisha vikao vya chama ghafla pamoja na mambo mengine, kufanya mabadiliko kwenye sekretarieti yake.
Duru za kisiasa kutoka ndani ya chama hicho tawala, zilisema kuwa mabadiliko hayo yanatokana na mmoja kati ya wajumbe wa sekretarieti, Januari Makamba, kuteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Sayansi Teknolojia na Elimu ya Juu.
“Kama utakumbuka mara ya mwisho Rais Kikwete aliamua kuwaondoa mawaziri wote kwenye sekretarieti ya chama ili wajumbe hao waweze kufanya kazi muda wote. Alimwondoa Waziri Bernard Membe, Nape akalazimika kuachia u-DC. Kwa vile Makamba amekuwa waziri ni wazi kwamba ataachia nafasi hiyo na Rais ataijaza kwa kumteua mjumbe mwingine,” kilisema chanzo chetu cha habari.
Wajumbe wengine wa sekretarieti hiyo ni pamoja na Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, Mhasibu Mkuu, Mwigulu Nchemba, Martin Shigela, Amina Makilage, Katibu Mkuu Jumuiya ya Wazazi, Katibu wa Wabunge wa CCM, Jenister Mhagama, John Chiligati, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Vuai Ali Vuai, Asha Juma na Katibu Mkuu, Willson Mkama.
Katika kujaza nafasi hiyo, Rais Kikwete anaweza kuwagusa wajumbe wengine kama ataona kuna ulazima wa kufanya hivyo.
Ukiachia mabadiliko hayo, vikao hivyo vya CCM ambavyo vinaanza Mei 11 hadi 14, vinajadili mambo mbalimbali, ikiwemo hali ya kisiasa ndani ya chama hicho hasa kipindi hiki ambapo kinakabiliwa na kukimbiwa na wimbi la wanachama wake.
“Kuna mambo mazito ya kujadili. Kasi ya CHADEMA na ushindi wake Arumeru imeibua hofu, wimbi la wanahama wa CCM kuhamia CHADEMA, mpasuko ndani ya chama, suala la uchaguzi wa chama na mjadala wa Katiba ni baadhi ya mambo yatakayoibua mjadala mzito,” alisema mtoa habari wetu.
Mtoa habari wetu alisema kuwa kikao hicho pia kinaweza kuwaweka kiti moto wabunge wa CCM walioungana na wenzao wa upinzani kutia saini za kutokuwa na imani na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
Kwa mujibu wa ratiba ya vikao hivyo kuanzia jana hadi Mei 11 kutakuwa na vikao vya maandalizi, Kamati ya Maadili kukutana Mei 12 asubuhi na Kamati Kuu (CC) chini ya Rais Kikwete itakutana siku hiyohiyo jioni.
Mei 12 kutakuwa na semina maalumu kwa wajumbe wote wa CC na NEC na Mei 14 itakuwa siku ya NEC.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma, Nape alisema kuwa vikao hivyo ni maalumu kwa ajili ya wajumbe kujadili mjadala wa Katiba mpya.
Alipoulizwa kama kuna hatua zozote ambazo zitachukuliwa na kwa baadhi ya wabunge waliosaini fomu ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu, Nape alisema hoja hiyo haipo na haiwezi kuwepo kwani wabunge hao walitoa haki yao Kikatiba kuwawakilisha wananchi wao.
“Kwanza ikumbukwe kuwa Rais akiwa Tanga aliwapongeza wabunge kwa kuonyesha msimamo wao leo itakuwaje Rais tena awageuke na kuanza kuwawajibisha? Hilo halipo kabisa!” alisema.
Katika hatua nyingine, Nape alisema mawaziri wote waliotuhumiwa wawajibishwe kwa uzito wa makosa yao kama watabainika kuhusika.
“Hakuna mtu aliye juu ya sheria, kama mawaziri wanaotuhumiwa kufanya ubadhirifu wako ndani ya Baraza la Mawaziri au wale walioachwa ni lazima kila mmoja achukuliwe hatua kadiri ya kosa lake, kama leo hii Rais mstaafu Benjamin Mkapa kafikishwa mahakamani kwa ajili ya kutoa ushahidi itakuwa Baraza la Mawaziri?” alihoji Nape.
MKURUGENZI Mkuu Shirika la Umeme nchini(Tanesco), Mhandisi William Mhando amesema kuwa ikigundulika kama kuna ubadhirifu wowote uliofanyika katika shirika hilo kutokana na Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG) basi atakuwa tayari kujiuzulu.
Mhando alisema hayo jana wakati akijibu maswali ya waandishi wa habari katika mkutano wa kutoa ufafanuzi juu ya taarifa iliyotolewa na Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma(POAC) kwamba shirika hilo lilifanya ununuzi wa kati ya Sh300 bilioni hadi Sh600 bilioni kitu ambacho alidai si kweli na kimeleta matatizo.
Mhando alisema, shirika hilo limekuwa likipata hati safi baada ya ukaguzi na kwamba kama kuna chochote kitagundulika kuwa ni ubadhirifu basi atakuwa tayari kujiuzulu.
"Kama nimekosea niko tayari kujiuzulu na mwajiri akiamua kunihamisha sina tatizo na ninawaambia mimi sina miaka miwili kazini na shirika lina pata hati safi hilo muelewe na mliseme," alisema Mhando.
Kuhusu Jenereta ambalo liliagizwa litolewe nyumbani kwake alisema , mkataba wake wa kazi unaeleza kuwa anatakiwa kuwa na kifaa hicho hivyo alimwambia mwajiri wake hivyo na alimruhusu kuendelea kuwa nalo.
Akizungumzia ripoti ya POAC kuhusu matumizi ya fedha, Mhando alisema taarifa zilizotolewa kwa baadhi ya vyombo vya habari kuhusu Tanesco hazikuwa sahihi kwani kilichotolewa na kamati na kilichoandikwa kwenye vyombo vya habari si sahihi.
"Nimemwomba Mwenyekiti wa POAC, Zitto Kabwe atoe ufafanuzi kuhusu hilo kwa kuwa limetuletea matatizo kwenye sekta ya fedha ambayo tunaitegemea kufanya shughuli zetu," alisema Mhando.
Akizungumzia suala hilo, Zitto alisema kuhusiana na matumizi hayo ya Sh300 bilioni na Sh600 bilioni ambayo imesemekana yalifanyika ununuzi kinyume cha sheria imeleta matatizo kwani taarifa hizo zilizoenda kwenye umma hazikuwa sahihi.
"Hiyo imeleta shida kwenye taarifa ya kamati kwani hanzard za kamati taarifa haisemi hivyo na imewaletea shida Tanesco kwa kuwa wanahitaji mikopo kwenye taasisi za fedha," alisema Zitto.
Akitoa ufafanuzi alisema Tanesco walifanya ununuzi wa Sh258 bilioni na ni makubwa zaidi kuliko mashirika yote ya umma.
"Hawakufanya ununuzi kinyume cha sheria kwani kiasi hicho cha fedha tulichokitaja awali tulikuwa tunatoa mfano," alisema Zitto.
Mhando alisema hayo jana wakati akijibu maswali ya waandishi wa habari katika mkutano wa kutoa ufafanuzi juu ya taarifa iliyotolewa na Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma(POAC) kwamba shirika hilo lilifanya ununuzi wa kati ya Sh300 bilioni hadi Sh600 bilioni kitu ambacho alidai si kweli na kimeleta matatizo.
Mhando alisema, shirika hilo limekuwa likipata hati safi baada ya ukaguzi na kwamba kama kuna chochote kitagundulika kuwa ni ubadhirifu basi atakuwa tayari kujiuzulu.
"Kama nimekosea niko tayari kujiuzulu na mwajiri akiamua kunihamisha sina tatizo na ninawaambia mimi sina miaka miwili kazini na shirika lina pata hati safi hilo muelewe na mliseme," alisema Mhando.
Kuhusu Jenereta ambalo liliagizwa litolewe nyumbani kwake alisema , mkataba wake wa kazi unaeleza kuwa anatakiwa kuwa na kifaa hicho hivyo alimwambia mwajiri wake hivyo na alimruhusu kuendelea kuwa nalo.
Akizungumzia ripoti ya POAC kuhusu matumizi ya fedha, Mhando alisema taarifa zilizotolewa kwa baadhi ya vyombo vya habari kuhusu Tanesco hazikuwa sahihi kwani kilichotolewa na kamati na kilichoandikwa kwenye vyombo vya habari si sahihi.
"Nimemwomba Mwenyekiti wa POAC, Zitto Kabwe atoe ufafanuzi kuhusu hilo kwa kuwa limetuletea matatizo kwenye sekta ya fedha ambayo tunaitegemea kufanya shughuli zetu," alisema Mhando.
Akizungumzia suala hilo, Zitto alisema kuhusiana na matumizi hayo ya Sh300 bilioni na Sh600 bilioni ambayo imesemekana yalifanyika ununuzi kinyume cha sheria imeleta matatizo kwani taarifa hizo zilizoenda kwenye umma hazikuwa sahihi.
"Hiyo imeleta shida kwenye taarifa ya kamati kwani hanzard za kamati taarifa haisemi hivyo na imewaletea shida Tanesco kwa kuwa wanahitaji mikopo kwenye taasisi za fedha," alisema Zitto.
Akitoa ufafanuzi alisema Tanesco walifanya ununuzi wa Sh258 bilioni na ni makubwa zaidi kuliko mashirika yote ya umma.
"Hawakufanya ununuzi kinyume cha sheria kwani kiasi hicho cha fedha tulichokitaja awali tulikuwa tunatoa mfano," alisema Zitto.

















