Subscribe to receive latest Updates

Online :

You Are Here: Home - HABARI ZA KIMATAIFA , HABARI ZA LEO - Mkuu wa mashtaka wa Zuma akataliwa. Afukuza mawaziri waandamizi

IDADI YA WATU WALIOSOMA HABARI HII: counter
Mahakama moja ya Afrika Kusini imeharamisha hatua ya Rais Jacob Zuma ya kumteua Menzi Simelane kuwa mkuu wa mashtaka.
Mahakama hiyo imesema kuwa kuna mambo fulani kumhusu Simelanea ambayo yanatilia dosari sifa yake, kwani kuna wakati alitoa ushahidi wa uongo.
Chama cha Upinzani cha Democratic Alliance (DA) kilikuwa kimewasilisha kesi ikidai kuwa Bwana Simelane ni kibaraka wa Bwana Zuma.
Chama hicho kiliambia mahakama kuwa Simelane angeliwalinda watu fulani mashuhuri kutokana na kushitakiwa
Lakini Rais Zuma amekuwa akikanusha madai hayo huku akishikilia kuwa Bwana Simelane alikuwa ana sifa na uwezo wa kishikilia wadhifa huo wa mkuu wa mashitaka wa Afrika Kusini. Zuma pia alisema kuwa ilikuwa haki yake kama rais kuamua ni nani anastahili kuwa mkuu wa mashitaka na hiyo sio kazi ya mahakama.
Jaji wa Mahakama ya juu zaidi ya Rufaa Mahomed Navsa amesema kuwa kuteuliwa kwa Simelane kuwa Mkurugenzi wa Mashitaka ilikuwa kinyume cha katiba ya nchi.
Kiongozi wa chama cha upinazi cha DA Helen Zille ametaja uamuzi wa mahakama kama ushindi kwa demokrasia.
Amesema katika siku za hivi karibuni rais Zuma amekuwa akifanya uteuzi uliojaa utata ukiwemo uteuzi wa jaji Mkuu.
She said Mr Zuma had made several controversial appointments recently - including that of chief justice wa Afrika kusini.

Rais Zuma awafukuza mawaziri waandamizi
Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amewafukuza kazi mawaziri wawili wanaohusishwa na kashfa za rushwa.
Bw Zuma amewafukuza kazi waziri wa serikali za mitaa Sicelo Shiceka-anayeshutumiwa kutumia fedha ambazo hazijaidhinishwa kisheria na waziri wa kazi za umma Gwen Mahlangu-Nkabinde.
Rais huyo pia amemsimaisha mkuu wa polisi Bheki Cele ambaye pamoja na Bi Mahlangu-Nkabinde wamehusishwa na madai ya kuuza majengo kinyume cha sheria.
Wote watatu wamekataa kuhusika na kufanya jambo lolote kinyume cha sheria.
Mchunguzi maalum wa Afrika kusini, aliyeteuliwa kuchunguza malalamiko dhidi ya maafisa wa serikali, alitoa wito kwa Bw Zuma kuwachukulia hatua.
'Bei zilizopanda sana'
Lakini Thuli Madonsela- mchunguzi maalum anayejulikana Afrika Kusini kama mwendesha mashtaka mkuu- aligundua kuwa Bw Shiceka alitumia zaidi ya dola za kimarekani 68,000 za serikali kwa safari za kifahari na malipo ya hoteli bila idhini.
Gharama hizo ni pamoja na safari za kumtembelea mpenzi wake aliyekuwa amefungwa Switzerland kwa makosa ya kufanya magendo ya dawa za kulevya.
Katika ripoti iliyotolewa mwezi uliopita, Bi Madonsela alisema vitendo vya Bw Shiceka vilikuwa "kinyume cha sheria na matumizi mabaya ya madaraka, kukosa uaminifu kwa fedha za umma."
Alimshutumu pia kwa kusafiri nchi ya jirani ya Lesotho wakati akiwa likizo kutokana na kuumwa kwa gharama za walipa kodi' akitumia jina la uongo.
Kwa wakati huo, Bw Shiceka alikana madai hayo akisema "hayana msingi" na kuahidi kusafisha jina lake mahakamani.
Alielezea baadhi ya gharama zake za hoteli ni kutokana na nyumba aliyopewa kutokana na wadhifa wake kujaa mbu.
Katika uchunguzi tofauti, Bi Madonsela aliamua kwamba Bi Mahlangu-Nkabinde na Jenerali Cele- mshirika mkuu wa Bw Zuma- waliidhinisha mpango wa majengo yenye thamani ya mamilioni ya dola za kimarekani.
Bw Zuma alisema Jenerali Cele atasimamishwa kazi huku akilipwa mshahara wote, na uchunguzi ukiendelea dhidi yake.
Rais huyo alisema, uchunguzi huo utaongozwa na Jaji wa mahakama ya katiba Yvonne Mokgoro.

0 comments

Post a Comment