Subscribe to receive latest Updates

Online :

You Are Here: Home - HABARI ZA KIMATAIFA , HABARI ZA LEO - Maandamano Misri kupinga utawala wa kijeshi wa nchi hiyo.

IDADI YA WATU WALIOSOMA HABARI HII: counter
Mamia ya waandamanaji nchini Misri wameivamia tena medani ya Tahrir katika mji mkuu wa Cairo hata baada ya polisi na wanajeshi kutumia nguvu kuwaondoa.


Chini ya muda wa saa moja baada ya kuondolewa Tahrir,waandamanaji walirudi tena mahali hapo huku wakitoa matamshi dhidi ya utawala wa kijeshi wa Misri.
Katika makabiliano hayo mengine ya siku ya Jumapili, watu 11 wameripotiwa kuuwawa.Kutokana na vifo hivyo jumla ya idadi ya watu waliouwawa tangu siku ya Jumamosi imefikia 13.
Kwa mujibu wa madaktari watu wengine wapatao 900 wamejeruhiwa wakiwemo maafisa wa usalama 40.
Awali, waandamanji walilazimika kutoroka baada ya maafisa wa usalama kuwarushia gesi ya kutoa machozi na kisha kuwapiga kwa marungu.
Machafuko mengine pia yalishuhudiwa katika miji mingine ikiwemo , Alexandria, Suez na mji wa Aswan.
Wandamanaji hao ambao walikuwa wameziba nyuso zao ili gesi ya kutoa machozi isiwadhuru wanalalamika kuwa watawala wa kijeshi walikuwa na njama za kunyakuwa uongozi wa nchi hiyo.
Machafuko hayo yametokea kukiwa kumesalia wiki moja tu kabla ya uchaguzi wa maeneo bunge kuanza ambao utakuwa wa kwanza tangu Rais Hosni Mubarak kupinduliwa mwezi wa Februari.
Mwandishi wa BBC Helena Merriman amesema kuwa hali sio nzuri sana kwa sababu mara kunashuhudiwa hali ya utulivu na baadaye tena hali inabadilika na kuwa ya taharuki na watu kuanza kukimbia.
Katika kipindi cha wiki kadhaa zilizopita makundi wa Kiiislamu pamoja na wakereketwa wengine wamekuwa wakifanya maandamano nchini Misri huku waandamanaji wakidai kuwa kuna njama za kubadilisha katiba ili kuruhusu baraza la kijeshi kuendelea kuwa na uwezo mkubwa.

0 comments

Post a Comment