Subscribe to receive latest Updates

Online :

You Are Here: Home - HABARI ZA LEO - Misa ya Ijumaa Kuu ilivyofana

IDADI YA WATU WALIOSOMA HABARI HII: counter

Kiongozi  wa  kanisa  Katoliki  Baba Benedict wa 16  hapo jana aliongoza siku takatifu ya Ijumaa kuu  inayoadhimishwa na  wakristo kote ulimwenguni.
Kiongozi huyo wa dini ambaye ni mzaliwa wa Ujerumani, aliongoza msafara wa msalaba kama ilivyofanyika siku za kale, na akawakumbusha waumini jinsi matamanio ya dunia, kama vile hamu ya kufanikiwa, yanaweza kuwafanya watu kupoteza utu wao. Katika sala yake ya ufunguzi, Baba Benedict  pia alitaja mateso yanayowakabili vijana na wanyonge, pasi na  kutaja moja kwa moja hali  ya  kufichuka kwa  kashfa  ya  unyanyasaji watoto kingono uliokuwa ukifanywa  na mapadri uliozuka katika miaka ya hivi karibuni.
Maelfu ya watu, wengi wakiwa wamebeba mishumaa, walilizunguka eneo la Colosseum, kupitia vituo 14 vya msafara wa msalaba.

0 comments

Post a Comment