Subscribe to receive latest Updates

Online :

You Are Here: Home - HABARI ZA KIMATAIFA , HABARI ZA LEO - Ufaransa imewapa waasi wa Libya silaha

IDADI YA WATU WALIOSOMA HABARI HII: counter
Ufaransa imewarushia silaha waasi wanaopigana na majeshi ya Kanali Gaddafi magharibi mwa Libya, jeshi la Ufaransa limethibitisha.


Silaha na risasi zilipelekwa kwa wapiganaji wa kikabila wa Berber katika milima ya Nafusa.


Awali, ripoti iliyotolewa na gazeti la Le Figaro lilisema silaha hizo ni pamoja na roketi na makombora.


Ufaransa, nchi inayoongoza harakati za kijeshi za umoja wa nchi za kujihami za Ulaya Nato, haikuwaeleza washirika wao kuhusu hatua hiyo, limesema gazeti la Le Figaro.


Msemaji wa jeshi la Ufaransa, Kanali Thierry Burkhard alisema, " Tulianza kwa kurusha msaada wa kibanadamu: chakula, maji na vifaa vya matibabu".


Aliliambia shirika la habari la AFP, " Wakatai wa harakati hizi, hali ya raia ilizidi kuwa mbaya. Tuliwarushia silaha na vifaa vya kujilinda, hasa risasi.

0 comments

Post a Comment