Subscribe to receive latest Updates

Online :

You Are Here: Home - HABARI ZA KIMATAIFA , HABARI ZA LEO - Marekani inazungumza na Taliban

IDADI YA WATU WALIOSOMA HABARI HII: counter
Nchini Afghanistan Rais Karzai amethibitisha kuwa Marekani na mataifa mengine yanafanya mazungumzo ya awali na Taliban.




Watu walikisia kuwa Marekani ina mawasiliano na Taliban.


Lakini hilo ndio kwanza kuthibitishwa na kiongozi.


Rais Karzai amesema mazungumzo yanafanywa na Taliban, na kwamba jeshi la mataifa ya nje, hasa Marekani yenyewe, linafanya majadiliano.


Haijulikani nani wanaiwakilisha Marekani, na kama wanazungumza ana kwa ana na Taliban, au kuna mtu kati.


Kinachozungumzwa piya hakijulikani.


Msimamo rasmi wa Taliban ni kuwa majeshi ya kimataifa lazima kwanza yaondoke nchini kabla ya kujadili amani, na itazungumza na serikali ya Afghanistan tu.


Hayo hayalingani na yale aliyosema Rais Karzai.


Haifai kutaraji suluhu ya haraka kutokana na mawasiliano ya hivi sasa.


Utabiri wa pande zote, Nato, serikali ya Afghanistan na Taliban yenyewe, ni kuwa mapigano makali yataendelea kiangazi cha mwaka huu, na pengine miaka kadha ijayo.

0 comments

Post a Comment