Subscribe to receive latest Updates

Online :

You Are Here: Home - HABARI ZA KITAIFA , HABARI ZA LEO - NAZI UPUNGUZA MAKALI YA UKIMWI

IDADI YA WATU WALIOSOMA HABARI HII: counter
Vyakula vimetufanya tuamini kuwa maradhi mengi hayana tiba. Hiyo inathibitika wazi pale vyakula vinapotoa majibu ya tiba bila sisi wenyewe kujijua. Kwa mfano ni rahisi sana watu kula chakula wakashiba halafu wakawa hai na kusema dawa hii inafaa au dawa ile haifai na kusahau kukitaja chakula kama dawa ya msingi inayobeba mhimili mzima wa tiba zote. Hii ndio sababu madaktari na wauguzi wanakuwa wakali katika kuwasisitiza wagonjwa kula kabla ya kupewa dawa.


Katika ardhi ambayo binadamu hajafanya uharibifu wa mazingira, inaaminika kuwa pamelala tiba za magonjwa yote zikisubiri watu waje wazigundue.


Miaka ya 1980 ugonjwa wa AIDS ulitokea kuua wanaume, wanawake na watoto duniani kote kwa kishindo kikubwa! Watu wengi wamekufa na wengi wataendelea kufa, kitu ambacho ni tishio ulimwenguni kote mpaka hivi sasa. Wakati huo huo vyakula vimeendelea kuwa tiba na mhimili mkubwa kwa afya za waathirika wa magonjwa mbalimbali duniani kote huku gonjwa hili likizidi kuonyesha sura mbaya na ya kutisha zaidi kila kukicha.


Zipo tiba nyingi ambazo binadamu anazipata toka kwenye vyakula anavyokula bila kujua kama anajitibu. Tena kwa bahati nzuri zaidi ni kuwa tiba hizo pia zinapatikana bila gharama yoyote zaidi ya kula chakula, ukitofautisha na gharama za matibabu ya aina nyingine kama hospitali, dawa za kienyeji nk.


Unatakiwa ujue unapokula chakula chochote huwa unajitibu maradhi fulani bila kujijua. Kwa mfano unaweza kujitibu makali ya AIDS Endapo utatumia vyakula hivi vilivyoorodheshwa hapo chini, pamoja na dawa toka hospitali.


Namna ya kufanya:
Utahitaji;
1. Nazi. Yaweza kuwa nazi, mafuta ya nazi, tui la nazi, dafu n.k.
2. Chai mbichi isiyokaushwa.
3. Vyakula - mchanganyiko wa nafaka.


Nazi:
Nazi imewahi kuthibitishwa kuwa na vitu muhimu vinavyoua virusi. Lauric Acid ndiyo acid pekee kwa kuua virusi ambayo inapatikana toka katika nazi na pengine ni toka kwenye maziwa ya mamaake binadamu tu duniani kote.


Je, Ni kweli Nazi inarutubisha afya?
Acid hii ndiyo kitu pekee chenye uwezo wa kuua virusi na ni rahisi kugundua hilo kama utakuwa mtu mwenye kumbukumbu basi nakupa Uthibitisho katika maeneo matatu.
Linganisha afya mbovu za awali za watu waliohamia Dar Es Salaam kama vile wasichana wa kazi za ndani, vijana wanaokuja kusoma au kuutafuta maisha n.k. wakitokea sehemu zisipopatikana nazi. Utamkuta mtu anakuwa hajiamini, haongei sana, mwoga, ngozi yake imejikunja-kunja, miguu imepasuka na pengine hata kitambi cha kwashakoo ni kawaida kwao. Halafu angalia afya zao pale walipokula vyakula vilivyoungwa nazi kwa muda mfupi tu kama miezi mitatu tu wakiwa hapa Dar Es Salaam. Utagundua kuwa afya zao zilibadilika sana.Wananenepa, Mipasuko kwenye miguu inaondoka, Ngozi zinakuwa nyororo, kwashakoo inaondoka, wanakuwa sio waoga tena, wanaongea sana tena kwa kujiamini na kwa kusema yote ni kuwa wanachangamka kiafya.


Kwa wale tuliosoma “Old schools” mtakumbuka tulisoma vitabu vingi vikiwemo Alfu lela Ulela ambavyo vilijumuisha Safari saba za Sindbad Baharia. Katika safari zake aliwahi kutekwa akiwa na wenzie saba baada ya chombo chao kugonga mwamba na kuvunjika. Watekaji waliwafungia ndani na kuwalisha “wali ulioungwa nazi” ili wanenepe kisha wawachinje! Sindbad kwa kujua hilo hakula kiasi kikubwa na baada ya muda mfupi wenzie walinenepa sana na walichinjwa wakaliwa! Yeye alikuwa akikonda siku baada ya siku na kuwafanya maharamia hao kumfungulia atembee tembee awe huru ili aimarike kiafya na ndipo alipopata mwanya wa kutoroka….


Uthibitisho wa mwisho ni pale mtoto mchanga anapofiwa na mama yake basi huwa anaikosa lauric acid toka ziwa la mama na afya yake nadhani wote mmeshuhudia inavyoathirika. Kifupi ni kuwa anatakiwa pamoja na maziwa ya wanyama anayolishwa inatakiwa apate walau kijiko kimoja cha tui la nazi kila siku ili kuilinda afya yake isiporomoke.


Hivyo kama wewe ni muathirika wa maradhi ya aina yoyote, basi tumia dawa za hospitali, halafu ili kuthibitisha hili jaribu kula vyakula vilivyoungwa nazi kwa kiasi kikubwa, au chakula kilichokaangwa kwa mafuta ya nazi, au jenga mazoea ya kutafuna nazi mbichi na pengine ni vizuri zaidi ukaacha tabia ya kunywa soda na kuanza kunywa maji ya madafu pale unaposikia kiu.


Je Nazi yoyote inatibu?
Kama kawaida ya uhusiano wa mmea na udongo ulivyo, zipo nazi ambazo ukizipeleka katika maabara utazikuta zina kiwango kikubwa cha lauric acid au ukakuta lauric acid ipo kidogo au pengine ukakuta nazi haina kabisa lauric acid kwa vile udongo ulipooteshwa nazi kuna kemikali ambazo zinasababisha udongo huo kuwa sio sahihi kuzalisha acid hiyo katika nazi. Kwa kutambua hilo tafiti nyingi zimefanyika na nazi zenye dawa hapa duniani zipo japo chache na zinapatikana kwa kupiga simu no 0768 215 956 au email rotion@live.com Pia mpaka sasa yapo makampuni ya kusindika nazi ambayo yanakamua nazi zenye lauric acid ya kutosha na kuuza kama dawa. Nazi hizo zimeingizwa nchini na ninazitumia kutoa tiba kwa waathirika na hakika zinapunguza idadi ya watu wenye afya mbovu. Lakini mpaka sasa hakuna taarifa zilizowafikia wawekezaji wa ndani hasa katika sekta ya afya ambao ningeweza kushirikiana nao kuitafiti bidhaa hii nchini watu wale na wapone.


Je, Nazi zinapatikana?
Upande wa pili wa shilingi una sura ya nazi kuwa bidhaa ya wenye nazo tu mara baada ya habari hii kuenea. Sasa Vile vile ni vema kwa wizara za kilimo na chakula pamoja na wizara ya afya kukaa chini na kuangalia namna ya kukabiliana na changamoto hii ya kupungua kwa nazi masokoni pamoja na kupanda kwa bei ya bidhaa hiyo ambayo inaweza kufikia shilingi elfu tatu kwa nazi moja endapo theluthi moja tu ya watanzania wataamua kuitumia nazi kama dawa ya kurutubisha afya zao.


Wakati naendelea kukuletea habari hii, ni vema ukaituma email hii kwa watu ishirini au wote katika address book yako ili tupunguze idadi ya watu wenye matatizo ya kiafya. Tusifiche tiba maana kuwa na taifa lenye wagonjwa ni UMASIKINI. Tafadhali tuma sasa.

1 comments

  1. Very nice post....very nice article....

    Regards
    Biranchi

Post a Comment