Subscribe to receive latest Updates

Online :

You Are Here: Home - - Waislamu nao watoa tamko kupinga tamko la Maaskofu. Je kuna siasa ndani ya matamko haya? (mwisho wa habari hii angalia pia maoni watu wanasemaje)

IDADI YA WATU WALIOSOMA HABARI HII: counter


Habari kwa hisani ya Mwananchi
Katibu Mkuu wa CCM taifa Yusufu Makamba

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Arusha, kinatuhumiwa kuanza mchezo mchafu wa kuufanya mgogoro wa uchaguzi wa Meya wa jiji la Arusha uliosababisha vifo vya watu watatu, kuwa wa kidini.

Habari za uhakika kutoka ndani ya chama hicho, zimebainisha kuwa katika kufanikisha njama hiyo, baadhi ya viongozi  wamefanikiwa kuwashawishi baadhi ya masheikh jijini Arusha, kutoa tamko la kulaani vurugu na kupinga kile wanachodai kuwa ni viongozi wa dini kujiingiza katika siasa.


Mpango wa kuwatumia baadhi ya Waislamu kuingilia mgogoro huo ulianza tangu juzi, siku moja baada ya umoja wa  viongozi wa dini ya kikristo, kutoa tamko la kutomtambua Meya ya jiji hilo kwa tiketi ya CCM, Gaudence Lyimo.

Maaskofu hao pia waliaani kitendo cha polisi kutumia nguvu kubwa kupita kiasi kuvunja maandamano yaliyoandaliwa na Chadema kupinga mchakato wa uchaguzi huo.

Juzi jioni baadhi ya wanaCCM waonekana wakiwa kwenye harakati za kuwaalika waandishi wa habari kuhudhuria mkutano wa mashekhe uliofanyika jana mchana jijini Arusha, kulaani tamko la maaskofu.

"Kesho mashekh wanatoa tamko....Huu ni mgogoro wa kidini, maaskofu hawamtaki Kikwete ndio sababu wanampinga hadi Meya...Hali hii itatufikisha pabaya,"alisema kiongozi mmoja wa CCM (jina tunalo).

Kama ilivyodokezwa na viongozi hao wa CCM juzi, jana baadhi ya masheikh wa Msikiti Mkuu wa Arusha, waliitisha mkutano na waandishi wa habari na kutoa tamko la kulaani vurugu, ghasia na uvunjifu wa amani uliotokea wakati wa maandamano ya Chadema.

Katika tamko hilo ambalo nakala imesambazwa kwa jeshi la polisi, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Usalama wa Taifa, Mkuu wa wilaya ya Arusha, Ofisi ya Mbunge wa Arusha Mjini, Ofisi ya Meya wa Arusha na Ofisi ya Mkurugenzi, lililosomwa na Imamu wa msikiti huo, Mohamed Hambali Waislamu hao walisema tukio hilo liliwaathiri sana.

"Tumeshindwa kufanya ibada zetu msikitini kwa amani na utulivu, uharibifu wa mali ikiwa pamoja na kuchomwa moto majengo, kutupiwa mawe msikitini na watoto na wazee kuathirika,"inasomeka sehemu ya tamko hilo.

Tamko hilo, pia lilisomeka" Sisi viongozi wa dini ya Kiislamu tunawakumbusha wenzetu kwamba hatupaswi kuingilia maswala ya kisiasa kwa kutoa matamko ambayo yatapelekea uvunjifu wa amani."

Kauli hiyo, ambayo inaungana na kauli ya Katibu wa CCM mkoa wa Arusha, Mary Chatanda, aliyoitoa juzi, inaaminika kuwa ililenga kuwasema maaskofu ambao walitoa tamko la kutomtambua Meya wa CCM kutokana na kuchaguliwa bila kufuata utaratibu.

Tamko hilo, liliendelea kusema, " sisi viongozi tunatakiwa tuwe washauri wa kiroho na kusisitiza amani iliyopo. Ni vyema watu wakafuata kanuni na sheria za nchi kama inavyosomeka katika katiba ya nchi.

Taarifa hiyo, ilinukuu ibara ya 19(2) inayosomeka,"Kazi ya kutangaza dini kufanya ibada na kueneza dini itakuwa ni huru na jambo la hiari la mtu binafsi na shughuli za uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya mamlaka ya nchi"

Tamko hilo la kwanza la aina yake kwa Waislamu wa Arusha ambao kwa miaka mingi wamekuwa na misuguano na serikali ilieleza kuwa, waislamu watatii mamlaka iliyochaguliwa kwa mujibu na kanuni za nchi .

"Tunatambua ibara 107(1) mamlaka yenye  kauli ya mwisho ya utoaji haki katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, itakuwa ni Mahakama." ilisomeka taarifa hiyo.

Mwisho taarifa hiyo, ilitoa pole kwa wote walioathirika katika maandamano hayo yaliyofanyika juma iliyopita jiji Arusha ikiwamo familia za watu waliofariki dunia kwa kupigwa risasi za moto.

Hata hivyo mwenyekiti wa Kamati ya Msikiti Mkuu wa Arusha, Abdulaziz Mkindi, alikanusha tamko hilo kutolewa kwa shinikizo la CCM.

"Hili ni tamko letu sisi hatutumiwi na CCM wala serikali....Sisi waislamu wa Arusha Mjini tumeathirika sana na hizo vurugu na tunataka amani,"alisema Mkindi ambaye alikuwa pamoja na Imamu Hambali.



Comments 





0#23 lee 2011-01-10 12:44
Inaeleka taaluma ya uandishi Tanzania inazidi kudidimia kwani inaonyesha wazi mwandishi wa makala hii amevitwa zaidi na jazba ama utashi wa nafsi yake na kuweka pembeni wadhifa wake kama mwanidhsi, hivi udini ni waislamu tu kutoa kauli? jamani si kila mmoja ana haki ya kueleza kile yeye anachoona kuwa ni sahihi? vipi Maaskfou watoe kauli iwe sawa na Waislamu wakisema waonacho iwe udini?
Quote
0#22 mpiganaji 2011-01-10 12:33
Waislamu nchi hii wanashangaza sana,kila mara hukimbilia kwenye hoja ya udini ambayo kiasili haipo Tanzania.Kama udini ungekuwepo basi ni dhahiri waislamu wangekuwa kwenye hali ngumu sanan kimaisha.Ukweli ni kwamba wakristu ni asilimi 66 ya watu wote Tanzania,pia ndio waliosoma sana kuliko waislamu,zaidi ya hapo taasisi za kikristo ndio zinazotegemewa na watu wote including serikali ktk kuboost maendeleo ya nchi,mfano,maho spitali,vyuo,sh ule nk.Kwa habari zilizopo hata kikwete anategemea sana msaada wa taasisi za kikristo ili kufanikisha malengo yake.Waislamu wa nchi hii ni dhaifu sana,kielimu,kiuchumi,kijamii, lakini hayo hayaonekani kwa sababu ya umoja na mshikamano tuliyo nao kama watanzania,hivy o hoja ya udini haina nafasi ktk nchi yetu bali inatumiwa na kikwete na makamba kwa ajili ya kufanikisha matakwa yao ya kisiasa.
Quote
+1#21 mkweli 2011-01-10 12:28
ndgu mwandishi tamko lililotolewa na maaskofu u didnt say lna mkono wa chadema bt la masheikh ndo lna mkono wa ccm?,ofcoz pande zote mbili hazko sawa kuingilia siasa(siasa ni mchezo mchafu)
Quote
+1#20 Lawa 2011-01-10 12:03
MASHEHE SOMENI NA ELIMU YA DUNIA. ACHENI KUPINGA KILA KITU ANACHOSEMA ASKOFU. KUNA MTOA MAONI MMOJA SI WA GAZETI HILI, AKITOA MAONI YAKE KUHUSU MAUAJI YA ARSHA ALISEMA(NAMNUKU U)' SISI WASILAMU TUMEFARIJIKA KWA MUISLAMU MWENZETU KUWAUA WAKRISTO'.... ALIENDELEA..'WAKATI KAFIRI MKAPA ANAWAUA WAISLAM PEMBA WAKRISTO WALIKAA KIMYA, BILA SHAKA WALIFURAHI'..MWISHO WA KUNUKUU.

NGUGU MHARIRI NAKUOMBA UCHAPISHE MAONI HAYA KATIKA SAFU HII YA MAONI ILI WATANZANIA WAONE UPEO WA BAADHI YA WAISLAM, NA BAADHI YAO NI VIONGOZI KAMA HAO MASHEHE WA ARUSHA. INASIKITISHA KIONGOZI WA DINI KUFURAHIA MAUAJI.
Quote
0#19 ELISANTE KIFUMU 2011-01-10 11:48
kauli ya viongozi wa dini siyo ya kubeza kama walivyofanya viongozi wa ccm, kwani kilichofanyika arusha anayekikubali hana akili timamu kabisa. serikali ikae chini itafakari na kuwaomba radhi maaskofu kwa kauli yao ya kuwakashfu eti wavue majoho, mwenye mamlaka juu yao ni Mungu kwani ndiye aliyewaweka na si ccm au mtu yeyote.
Quote
+1#18 ELISANTE KIFUMU 2011-01-10 11:39
VIONGOZI WA CCM KUWAKASHFU VIONGOZI WA DINI ARUSHA NI SAWA NA KUMKASHFU MUNGU. NATOA TAHADHARI KWANI HAWAKUKURUPUKA KUMKATAA MEYA WA MKOA HUO BALI TARATIBU ZILIZOTUMIKA NI BATILI NA WAO KAMA VIONGOZI WA KIROHO HAWATAKIWI KUFUMBIA MACHO U[NENO BAYA] KAMA HUO. HII NI CHANGAMOTO KWA SERIKALI YA CCM KUKAA CHINI NA KUBADILIKA KWANI WATANZANIA WA SASA SI WALE WA MWAKA 47 WANA AKILI TIMAMU KABISA KUJUA LIPI JEMA NA BAYA.
Quote
+1#17 mlay 2011-01-10 11:25
Hivi tumefikia mahali ambapo watu wanaanzisha machafuko alafu wanasema kuwa atakayeamua ni mahakama??. Kwa hiyo inawezekana kuwa matokeo ya uchaguzi uliyopita haukuwa sahihi ila wanasubiri mtu asiyeridhika aende mahakamani?? UPUZI GANI HUU??
Quote
+3#16 assenga 2011-01-10 11:16
kwa mtu mwenye akili timamu anafahamu vyema tanzania ya leo HAKUNA UDINI tusipokua makini watu kama Kikwete na Makamba wanaweza kutupeleka kwenye machafuko kauli aliyoitoa mkuu wa nchi dhidi ya alichokiita udini ni uongo kwani ata asasi binafsi zilizoshiriki katika uangalizi wa upigaji kura walishtushwa na kauli hiyo na kukiri hakukuwa na udini katika mchakato wote uchaguzi iweje udini huo auone Kikwete pekee ni aibu kwa kiongozi kupenda sifa kuliko utendaji hakuna serikali mbovu kama hii ya JK Watanzania tuamke tusigawanywe kwa misingi ya dini, kabila wala rangi ila tujue tu sisi ni Watanzania
Quote
+1#15 Onyango 2011-01-10 11:08
Mimi nadhani aliye andika habari hii hapaswi kuwa journalist. Habari kama hii ni mbaya na hayatakiwi.
Quote
+1#14 Kahamba 2011-01-10 11:04
Ni vigumu kuamini. Mtu anakosoa waliokemea uvunjaji wa sheria kwamba wanaingilia mambo ya siasa ilhali yeye akizungumzia suala hilo hilo na bado anajiita kiongozi wa dini. Ngoja tuwasome!!!
Quote
+10#13 Bern. 2011-01-10 10:24
Assalam aleykum ndugu zangu waislamu? Naomba niwataazalishe na hao ccm. Nyinyi kama kweli ni wacha mungu na mnasoma vizuri hadithi za Mtume,basi kwa kitendo cha maaskofu kukemea uovu wa ccm Arusha mngeunga mkono. Mimi si zini kama JK alichaguliwa na waislamu tu,Kikwete mwenyewe amekuwa akipata msaada mkubwa kutoka kwa hao maaskofu mpaka kufika hapo alipo,kama hamjui. Tujenge nchi yetu tuachane na fikra potofu kama hizi za udini,tusibagua ne,tukisubutu tu basi tumekwisha,ccm na mafisadi wake watatomia upenyo huo kutumaliza. Kwa taarifa yako ile pesa ya dowansi hata nyinyi waislamu mtailipa. Na nyinyi ndio mtakuwa wa kwanza kukosewa adabu na huyo meya kwani atakuwa anajivunia kwamba kawekwa hapo kwa nguvu za ccm tu.
Quote
+8#12 MAYUMA PASKALI 2011-01-10 10:20
hivi kweli Tanzania kungekuwa na udini, kuna mwislamu ambaye angeshika uraisi! for quick fact Tanzania ina zaidi 66% ya wakristo..swali je kungekuwa na huo udini wanaousema kikwete angeingia madarakani! ninakumbuka sana kwenye kampeni ya mwaka 2005 ambapo kikwete alishinda kwa takribani asilimia 80 wakristo especially wachungaji walichangia ushindi wake kwa kusema alitumwa na MUNGU! hebu ccm waone haya na waache kuintroduce hoja za kizamani yaani"divide and rule" mimi nadiriki kusema Tanzania hakuna udini hata kidogo, na kama wanataka kuuanzisha wajue mwisho wake ni mbya na watawajibishwa
Quote
+7#11 kivuli fimbo 2011-01-10 10:13
amani ya nchi ni furaha kwa wote bila kujali dini,kabila,ran gi wala jinsia,nafikiri ni busara kila mmoja wetu kukemea ishara yoyote ya uvunjifu amani na utulivu wa nchi bila kujali dini yake au chama chake.Waislam wenzangu mmeridhikaje na uchaguzi wa meya wa Arusha hadi kujitokeza hadharani kusema kuna kuna dalili za udini?hivi mnafikiri kupitia watu kupokonywa haki kwa kisingizio cha udini pakinuka misikitini pataingilika? tumieni busara waambieni waumini ukweli ili haki itendeke.
Quote
+8#10 Optatus NCHIMBI 2011-01-10 10:13
Busara itumike katika kusema ukweli na siyo kuupotosha. Waislamu wana haki ya kusema kile wanachokiona kwa mtazamo wao kuwa ni sawa na hapo ndipo tunapaswa kutenga pumba na mchele. Mwislamu akisema upotofu anaidhalilisha dini ya Uislamu kwa kuwa watu wanaosoma wana upeo wa kuchambua pumba na mtama. Iwapo hayo yaliyosemwa na na Imamu wa msikiti wa Arusha, Mohamed Hambali ndiyo msimamo wa Viongozi wa Waislamu Mkoani Arusha basi mwenye macho haambiwi tazama na wenye masikio asiambiwe asikie utashi na busara za wachunga Kondoo wa Mtume. Sina hakika kama hayo ni matamshi yaliyotokana na Kahawa, bhagia am aina nyingine ya rushwa lakini ninachokiona hapa ni upeo wa wahusika katika kuchambua maswala ya kidunia na kiimani. Madudu hayakubaliki hata kama wanazuoni ama watu wa dini wakiyaunga mkono yatabaki kuwa ni madudu tu. Shime watanzania tusikubali kuyumbishwa na misimano ya kupandikizwa kwa kisingizio cha Udini bali tuuangalie ukweli wa yaliyotokea na tuyaweke sawa. Pima imani yako na iruhusu dhamira yako ya dhati ikuukumu juu ya kile unachokiamini na kukisema. Rushwa ipo na ukweli utabaki kuwa ukweli hata kama akili yako imechakachuliwa na rushwa ya aina yoyote. Imesemwa kuwa, "Utaujua ukweli na ukweli utakuweka huru".
Quote
+7#9 Zalendo 2011-01-10 10:08
Hata mie nilikuwa najiuliza: "KWA NINI MAKAMBA ATUMIE BIBLIA (AKINUKUU KITABU CHA WARUMI) KULAANI MAANDAMANO YA KUDAI HAKI ARUSHA? KWANI MAANDAMANO YALIKUWA YA WAKRISTO AMA YA RAIA WOTE WENYE KUPENDA HAKI ARUSHA????


hIVI MASHEHE; TUKIACHA KUWA NI MWANASIASA WA CCM; KWA MATHALANI; MKIWA KAMA RAIA WA KAWAIDA BILA CHEO CHENU CHA DINI; HUO UCHAGUZI ULIKUWA HALALI KWA KATIBA IPI?? IBARA GANI INASEMA DIWANI ANACHAGULIWA NA UPANDE MMOJA WA CHAMA BILA YA KUWEPO UPANDE WA PILI BILA YA KUWA NA KIZUIZI HALALI KISHERIA?? YAAAANI, HAO WANANCHI WALIOCHAGUA MADIWANI WA CHADEMA HAWANA HAKI YA KUWAKILISHWA KWENYE KUCHAGUA MEYA WA MJI WA ARUSHA?? MNAWEZA UKANIELIMISHA KWA HILO???
Quote

+3#8 Philemon 2011-01-10 10:04
WATANZANIA LAZIMA TUJIFUNZE KUWA WA TAMBUZI WA ALAMA ZA NYAKATI. NCHI YETU IMEKUWA SHAMBA LA BIBI NA KILA MTU ANAJIFANYA ANA MAMLAKA. KUHUSU SUALA LA ARUSHA CCM NA SERIKALI YAKE WANAPASWA KUBEBA MZIGO WA LAWAMA KWANI NDIO WANOTUMIA NGUVU YA DORA KATIKA KUKANDAMIZA HAKI ZA RAIA WA TAIFA LETU. MAOSKOFU KUSEMA NI HAKI YAO NA WANAHOJA ZA MSINGI, NA HAO MASHEKHE NAO PIA WANAHAKI YAO KIKATIBA LAKINI MAELEZO YAO YANATIA MASHAKA KWANI YANASHINIKIZO LA KISIASA ZAIDI, KUHUSU KATIBU WA CCM WALA SIWEZI KUMLAUMU KWANI YEYE NA CHAMA CHAKE WAMEOZA KIMAADILI NA HATA KIIMANI, KWA AKILI YA KAWAIDA HUWEZI KUNYANYUA KINYWA CHAKO NA KUWAAMNIA VIONGOZI WA DINI WAKAGOMBEE UDIWANI, VIONGOZI WA DINI WAPO KATIKA JAMII KUKEMEA MAOVU NA MAONEVU KATIKA JAMII. NAWAOMBA WATANZANIA TUAMKE KWANI KUNA WATU WANATUMIA UDINI ILI KUTAKA KUJINUFAISHA WAO BINAFSI.


USHAURI WANGU SIJAWAHI KUONA JESHI LA POLISI DHAIFU KAMA LA KWETU KWANI HUWEZA KUYUMBISHWA KAMA PIA. NDUGU ZETU POLISI AMBAO MMEPEWA DHAMANA KUBWA NA TAIFA LETU TUTUMIKIENI PASIPO MAONEVU KWANI MKITUUUWA SISI NI SAWA UMEMUUA NDUGU YAKO.
Quote
+2#7 wakunyumba 2011-01-10 09:13
Tafakuri twice kweli tunataka mabadiliko bt the problem is the way we are going through.
Quote
+6#6 mjenzi 2011-01-10 09:09
Uchochezi wa kidini umekuwa ni staili ya Kikwete na mpambe wake Makamba kwa maslahi yao na chama chao. Mheshimiwa Warioba aliwahi kunukuliwa na Gazeti la Raia Mwema Toleo la 163 kwamba "Udini unaotajwa ni Ulaji wa Wakubwa." Kauli hii inatufumbua macho Watanzania ili tusiwe kondoo wa kupelekwa machinjioni. Tuchambue mchele na pumba. Tushikamane kama Watanzania kudumisha umoja na mshikamano wetu kwa kuzingatia mambo yanayotuuungani sha kuliko yanayotutengani sha. Mimi ni Mkristo lakini nina ndugu na marafiki wengi Waislamu. Tunalaani yale yanayozungumzwa aidha na viongozi wa dini au wa serikali kwa lengo la kutuchochea ili tugawanyike kwa maslahi yao!
Quote
-2#5 Cash 2011-01-10 09:06
Wakisema maaskofu sawa,wakisema ma sheikh udini.That means tanzania kuna dini moja tu ya Kiislam
Quote
-5#4 Kibavu 2011-01-10 09:05
Mwandishi epuka jazba katika kazi yako, hili ni tamko la waislamu wa Arusha, usichanganye mambo,na wao wana haki sawa na wengine kutoa maoni yao vipi leo uufanye uislamu ni tawi la CCM? haiwi na kamwe haitokuwa
Quote
+4#3 Kashinde Mugeza 2011-01-10 08:54
Hivyo sisi waTanzania hatutumi akili wala Busara.......Jamani Uchochezi utatuponza na kutufikisha njia panda!!
Wapambe wana agenda zao. Rai wa kawaida ana chapa kazi Lakini maendeleo haya onekani milele.Sababu siasa inaongoza na kuwaficha waliyo wajanja.TUWE MACHO waBongo....
Quote
+2#2 maharagejuma 2011-01-10 08:02
NYIE MNAOJIITA SIJUI MASHEHE WA ARUSHA AU TUSEMA VIONGOZI WA KIISALAM ARUSHA SASA NI KIPI BORA ANAEPEWA RUSHWA NA CCM NA KUAMBIWA NENDENI MKAPINGE AU MKASEME KUWA JAMBO HILI NI LA KIDINI. HIVI KWA AKILI YENU NYIE VIONGOZI WA WAISALAMU ARUSHA KITENDO CHA UCHAGUZI WA UMEYA WA ARUSHA KWENU MNAONA NI SAWA? KUNA SHIDA GANI NANYI MKISEMA AU WAKRISTO KUSEMA HAMTAMBUI MEYA ALIYECHAGULIWA BILA KUFUATA SHERIA. NAWAMBIA NYIE VIONGOZI WA WAISLAMU ARUSHA HIVI KAMA WAKRISTO WANGEKUWA HAMPENDI KIKWETE UNAFIKIRI KIKWETE ANGEKUWA MADARAKANI HADI LEO. ACHENI PROPAGANDA BAADA YA KUPEWA KAHAWA MNASHINDWA HATA KUONGEA UKWELI. KWANZA NI NYIE NDIO MNAOLETA VURUGU PASIPO KUSEMA UKWELI, NI NYIE NDIO MNAOLETA VURUGU KILA MARA MNAPOPEWA HONGO NA KUPINDISHA KUSEMA UKWELI KWA KUMTETEA KIKWETE. KIKWETE ANAFANYA MADUDU YAKE HALAFU ANAWAITA NYIE WAISLAMU NA KUSEMA WAZEE WA DAR ES SALAAM NA KUWAONGOPEA NA KUUNGA MKONO. INATAKIWA MUWE NA MSIMAMO MSIENDESHWE KWA RUSHWA MNAJUA FIKA KUWA UONGOZI WA KIKWETE IMEJAA RUSHWA NA HATA YEYE MWENYEWE AMESHIRIKI KUTULETEA RICHMOND/DOWANS TUTAKAOWALIPA MABILION NA HUKU UMEME HAKUNA LAKINI NYIE VIONGOZI WA KIISLAMU HATA SIKU MMOJA KUUKEMEA SERIKALI HAKUNA. KAMA NI MADUDU ANAYOFANYA KIKWETE NI LAZIMA MKEMEE ACHENI HIZO POROJO ZENU KWA VILE KIKWETE NI MUISLAMU KWAHIYO HATA AKIFANYA MADUDU NYIE MNAMBEBA TU. ALIPOKUWA MKAPA MBONA VIONGOZI WA KIKRISTO WALIKUWA WANAMSEMA NYIE MNASHINDWA NINI KUMKEMEA MUISLAMU MWENZENU. KUPANDA KWA UMEME HAIMUUMIZI MKRISTO PEKEE HATAA WEWE MNAUMIA ACHENI POROJO BAADA YA KUONGWA KAHAWA NA BHAJIA. TETEENI UKWELI MSIMAMO WA VIONGOZI WA KIKRISTO UTABAKI PALEPALE YA KUMTAMBUA MEYA WA ARUSHA ALIECHAKACHULIW A HATA MUONGEZEWE VITUMBUA NA KUANDIKA TENA. LAKINI UKWELI UTABAKI PALEPALE.
Quote
-1#1 mary 2011-01-10 08:01
???
Quote



Related Article:

0 comments:

Tags:

0 comments

Post a Comment