Subscribe to receive latest Updates

Online :

You Are Here: Home - - Mbunge David Kafulila adai viongozi serikalini hawana msimamo wa pamoja

IDADI YA WATU WALIOSOMA HABARI HII: counter
MBUNGE wa Kigoma Kusini, David Kafulila amesema  kauli zinazopingana kutoka kwa viongozi wa serikali kuhusu madai ya katiba mpya zinaonyesha kwamba serikali ni dhaifu na kwamba viongozi hao hawana msimamo wa pamoja.

Amesema  kitendo cha kauli ya Waziri wa Katiba na Sheria, Celina Kombani pamoja na ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji  Frederick Werema kupishana na tamko la Rais Jakaya Kikwete ambaye amebariki kuanza kwa mchakato wa kuandikwa katiba mpya ni dosari kubwa ndani ya serikali na taifa.

Kombani ambaye ndiye waziri mwenye dhamana ya Katiba alisema kuundwa kwa Katiba mpya kwa sasa hakutawezekana  kwani sio muhimu na kwamba serikali haina bajeti ya kushughulikia katiba mpya. 
Waziri huyo aliyeingia madarakani kuiongoza wizara hiyo kwa mara ya kwanza,  alisema serikali itaendelea kufanya marekebisho ya sheria hiyo mama wakati wowote inapolazimika.

Wakati Kombani akitoa kauli hiyo Jaji Frederick Werema alisema  haitawezekana kuandikwa kwa katiba mpya  bali linalowezekana ni  kufanya marekebisho kwa kuondoa au kuongeza mambo fulani kwenye katiba inayotumika hivi sasa ambayo watu wa kada mbalimbali nchini wanataka ibadilishwe.

Lakini jana akizungumza na Mwananchi  Kafulila alisema, “ Kitendo cha Waziri wa sheria,  Mwansheria mkuu na Rais Kikwete  ambao wapo ndani ya  serikali moja kutofautiana hadharani kwenye suala  nyeti kama la Katiba ni kielelezo kwamba tuna serikali dhaifu,”

Aliongeza, “Serikali sio moja ndio maana hakuna msimamo mmoja, hali hii inatia mashaka  na kuongeza wasiwasi katika mchakato mzima wa  ufanisi wa utendaji kazi wa serikali, “.

Alifafanua kuwa hivi karibuni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta  pamoja na Waziri wa Nishati na Madini, William Ngereja  nao walitoa msimamo tofauti kuhusu  hoja nyeti ya  kesi ya Dowans na Tanesco. 

Kafulila  ambaye ametangaza  kuwasilisha hoja binafsi bungeni kuhoji sababu zinazoifanya serikali isiwajibike kwa kuliingizia taifa hasara ya mabilioni ya fedha kwenye sekta ya nishati ya umeme alisema

“Ngereja alisema maoni ya waziri Sitta ni sawa na maoni ya Watanzania wa kawaida, akasahau kuwa wote ni wajumbe wa cabinet (Baraza), hiki ni kilelezo kuwa serikali hii ina mgongano mkubwa wa kiuongozi,”.
Tags:

0 comments

Post a Comment