Subscribe to receive latest Updates

Online :

You Are Here: Home - HABARI ZA KIMATAIFA , HABARI ZA LEO - Raia wa Tripoli waandamana kupinga waasi

IDADI YA WATU WALIOSOMA HABARI HII: counter
Maelfu ya raia wa Libya wameandamana katika jiji kuu Tripoli kulalamikia makundi ya waasi ambao walisaidia kumuondoa madarakani Kanali Muammar Gaddafi.
Raia hao waliopeperusha bendera walikusanyika katika medani ya Martyrs ambapo walitaka utawala wa sasa kuwapokonya silaha wapiganaji wote ambao wamekuwa wakidhibiti maeneo kadhaa ya jiji kuu.
Kumekuwa na makabiliano kati ya makundi hasimu na serikali iliwataka wapiganaji hao kuondoka Tripoli katika muda wa wiki mbili.
Waliandamana baadhi wakipeperusha bendera, wengine matawi ya zeituni. Kundi moja la watoto walikuwa wamebeba mabango yaliyosema "usiangamize mustakabali wetu". "hatutaki silaha," walisema.
Waasi ambao mwezi wa Agosti walipigana vita hadi wakafika jijini Tripoli na kumuondoa madarakani Muammar Gaddafi sasa hawakaribishwi tena hapa baada ya kuzuka makabiliano kati ya makundi hasimu ya wapiganaji
Na katika jiji lisilo na kikosi rasmi cha jeshi wala maafisa wa polisi , huku silaha zikiwa mikononi mwa wengi raia wa eneo hili wamekerwa na kuzorota kwa hali ya usalama.
Mapema leo, majaji na mawakili waliandamana baada ya wapiganaji waliojihami kwa silaha kujaribu kumlazimisha mwendesha mashtaka kutia saini karatasi za kuwaachilia huru wapiganaji wenzao waliofungwa jela.
Nao madaktari na wauguzi waliangalia tu wasijue la kufanya baada ya wapiganaji wawili waliojihami na bunduki kuvunja milango na kumtoa nje kwa nguvu aliyesimamia hospitali , wakipinga vile mgonjwa mmoja alihudumiwa.
Na katika chumba cha wagonjwa mahututi kumejaa watu ambao wa majeraha ya risasi. Hali katika hospitali imezidi kuwa mbaya baada ya baada ya madaktari kutoroka wakitaka kuhakikishiwa usalama wao na serikali.

0 comments

Post a Comment