Subscribe to receive latest Updates

Online :

You Are Here: Home - - Makamba amjibu Askofu Laizer

IDADI YA WATU WALIOSOMA HABARI HII: counter
KATIBU Mkuu wa CCM, Yusuph Makamba, amesema kuwa na uelewa finyu wa biblia si jambo la ajabu kwake kwa sababu yeye siyo askofu.

Makamba aliliambia Mwananchi jana kwa simu, kuwa  licha ya uelewa finyu wa biblia, lakini amekuwa akitoa vifungu hivyo kwenye biblia.
Makamba alisema hayo kufuatia, Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Thomas Laizer kusema Makamba ana uelewa finyu wa biblia.

Laizer alisema hayo juzi mjini Arusha wakati wa kuwaaga watu wawili waliofariki kwa kupigwa risasi na polisi katika maandamano na Chadema yaliyofanyika Januari 5 mwaka huu.

 “ Ni kweli ninauelewa finyu wa biblia kwa sababu mimi siyo askofu, hata Qurani naweza kuwa siifahamu vizuri kwa sababu mimi siyo Sheikh, ndiyo maana kila ninachozungumza kuhusu dini hizo nakariri vifungu kutoka katika vitabu hivyo,” alisema. Makamba alisema alimweleza Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, kutoandamana kwa sababu serikali ilipiga marufuku maandamano hayo, wao wakapuuza.

Alimtaka Laizer kutoa tafsiri ya kitabu cha Warumi 13 sehemu ya kwanza hadi ya saba, inayosema  kuwa kila mtu hana budi kutii  serikali inayotawala kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu.
Alisema kwa hiyo anayepinga mamlaka inayotawala anapinga chombo kilichowekwa na Mungu na watu wanaoasi hujiletea hukumu.

 “ Kwa maana watawala hawatishi watu wanaotenda mema bali wale wanaotenda maovu, kama hupendi kuishi kwa kumwogopa mwenye mamlaka  basi tenda mema naye atakusifu,” alisema.

 “ Laizer anieleze ufinyu wangu katika uelewa wa biblia  upo wapi ikilinganisha na tukio lililotokea mkoani Arusha,”  alisema.  


 

Comments 

 
-1#24 UHURU. 2011-01-14 12:05
Makamba ya Kinana ndio matatizo ya CCM. Propaganda zao na siasa wanazofanya leo ni za mwaka 47. Dunia ya leo watu wanajua wanachokitaka na wanataka washirikishwe kukipata. Matumizi ya nguvu hayadumu 'its a dead end'. Hakuna aliyetumia nguvu akasonga mbele. Makamba kwa kifupi ni out dated politician. No body is scared of the ruling party any more. All that we need is respect and understanding. Tumetoka mbali. Kuna mtu ni mwanachama wa CCM na bado ni mfadhili wa CHADEMA. Dunia imebadilika sana baba Makamba.
Quote
 
 
0#23 Katiba TANGANYIKA 2011-01-14 12:01
CCM itatufikisha pabaya!!

Hivi Makamba kama msemaji mkuu, anavolumbana na maaskofu anaonyesha busara gani?
Kwa umri na uzoefu wake nilitegemea mawazo ya busara ya kujenga amani, pia angetoa nafasi wenye uchungu na nchi tulumbane kuijenga nchi!

Lkn anachokifanya Makamba ni kuonyesha ubabe wake na CCM, kwamba wamelikusudia kuzuia maendeleo ya democracy kwa hata kwa silaha za moto kama ilivyofanyika Arusha.

Badala ya kuwapa pole waliofiwa CCM kupitia Makamba wanaendeleza mzozo huo akitumia kigezo cha maaskofu, Je mbona Sheikh Alawi alikuwepo kwenye maombolezo? Udini sio tatizo, kwa hiyo CCM isiendeleze chuki za kidini.

Kwa nini Makamba ananukuu kutoka bibilia na sio HUMAN RIGHT ACT? Ama anatufanya wa Tz [NENO BAYA] sio? kama CCM wamesahau wapitia vifungu vya:

-Right to liberty and security
-Freedom of expression
-Freedom of assembly and association
-Prohibition of abuse of rights
-Right to free elections
-Limitation on use of restrictions on rights

Tusishabikie u[NENO BAYA] wa Makamba kutupumbaza na malumbano yake na Maaskofu!

Serikali,CCM na Police wapitie vipengele hivyo vya Human Right Act na watueleze maana ni nini?
Quote
 
 
0#22 Happy 2011-01-14 12:00
Wee Makamba kwani nani kaichagua hiyo serikali? si mmejiweka wenyewe hapo?? sio serikali iliyochaguliwa nqa Mungu katu!! wezi wa kura wakubwa nyie na sasa mnajiongezea na sifa nyingine wauaji wakubwa!! Hivi wee makamba unawatia aibu na kuwapotezea chance ya utawala wanao wazuri akina January. unaaribu jina la wanao!! funga mdomo wako kila ukiufungua unatoa maneno kama kinyesi!!
Quote
 
 
-1#21 Bilauri 2011-01-14 11:50
MH..........Kumbe na wao inawauma, wakipigwa CUF kimyaaa lakini CHADEMA watasema mapadri wote,,!!!! muje muda wa "funika kombe mwanaharamu apite" sasa hivi tutaenda ngoma droo, ikizidi turtapambana, Bravo MAKAMBA
Quote
 
 
-1#20 Keddy 2011-01-14 11:45
Angalua, Mlay na wengine ambao mnaingalia nchi kwa macho ya huruma kama mimi mnaweza ona ni jinsi gani nchi inateketea. Hawa Jamaa wanaotanguliza udini, Jazi na kalubandika wana mawazo mafupi, tena mafupi sana. Laiti nchi hii wakristo wangekua na mawazo kama yenu ninyi mnaokumbatia udini kila wakati panapokuwa na hoja ya msingi eti kwasababu mtawala ni muislam na katibu mkuu wake vile vile, sidhani hii leo kikwete na makamba wangekua hapo walipo. Ukweli usiopingika ni kwamba CCM ya leo, haina mwelekeo kwa kuwa uongozi wake umejaa majungu, haupendi wasema ukweli, wako pale kula njama na wezi wa pesa na rasilimali za nchi hii, hawana huruma hata kidogo na walala hoi. Kwanza, hivi kweli ukimwangalia Makamba, na mdogo wake Tambwe Hiza, hapo kweli hilo gari moshi la CCM litatupeleka pazuri kweli, no way!
Quote
 
 
-1#19 lapa 2011-01-14 11:40
Makamba amekosa heshima kwa ukristo..dini yake na biblia ni imani mbili tofauti kabisa sasa sijui yeye anatafuta nini humo wakati hamtambui yesu ni nani ktk biblia.


UKISIKIA UDINI NDIO HUU SASA
Quote
 
 
0#18 Ndele 2011-01-14 11:31
Makamba amepwaya sana kwenye nafasi ya ukatibu mkuu, wala haihitaji shahada ya kutunukiwa kuelewa hilo. Bosi wake ametunukiwa shahada chungu nzima lakini bado hajang'amua kwamba Makamba anaipeleka CCM kuzimu. Nadhani kamati kuu yote wana uelewa finyu. Looh! Nimemkumbuka Super Admininstrator Philip Mangula!!!
Quote
 
 
0#17 samwel mwanga 2011-01-14 11:24
MAKAMBA KWELI [NENO BAYA] HANA JIPYA KWA SASA HAWEZI KUBISHANA NA ASKOFU LAIZEIR TATIZO ANAJIFANYA KILA KITU ANAJUA KUMBE HAELEWI CHOCHOTE
Quote
 
 
+2#16 kivuli fimbo 2011-01-14 11:20
MZEE MAKAMBA INAMAANA UNAFUFURAIA MAUAJI YANAYOFANYWA NA POLISI? KUMBUKA WALIOUWAWA NI WATANZANIA NA WAPIGA KURA WALIOMPELEKA ANAEKUVUMILIA KWENYE MADUDU YAKO UNAYOFANYA IKULU.IKIWA KUTAFSIRI MISAAFU YA DINI HUJUI KAA KIMYA USITUTIE HASIRA...............
Quote
 
 
+2#15 Fredrick Mlay 2011-01-14 10:31
Quoting Keddy:
Makamba, hukurupuka tu, you cant argue with bishops. Kwani Makamba ni nani? amechangia nini katika maendeleo ya nchi hii kama sio kuinyonya tu? Ana elimu gani, kama sio basic certificate ya ualimu. Ni aibu kwa CCM kuongozwa na mtendaji ambaye hana management and administrative skills. Hata kwenye ukuu wa mkoa alikua hana muelekeo katika maamuzi yake. Roho za watanzania zinaumia kwa sababu ya huyu mtu anaitwa Makamba. Ana mwisho wake, sijui atajificha wapi baada ya kutoka kwennye majengo ya kijani. Na bahati mbaya sana, maamuzi yake mabovu yatatufanya tusiamini mtu yoyote mwenye surname ya Makamba!!


Kennedy usihofu, hiyo ndio advantage kwa wanamageuzi.. udhaifu wa makamba kiutendaji ndio utakaotunufaish a japo damu imemwagika lakini tuvumilie ifikapo 2015 ccm itagundua ilikuwa na wrong person to the wrong position..
Quote
 
 
+1#14 Fredrick Mlay 2011-01-14 10:26
Ninapendezwa sana na jinsi makamba anavyo jichanganya kila kukicha na kuzidi kukididimiza chama chake ccm, japo mengine yanaudhi lakini tujue hiyo ni advantage kwa wanamageuzi, songa mbele makamba umalize kazi uliyoianza.. 2015 ninahakika kwa jinsi ulivyo ccm itakuwa imechoka
Quote
 
 
0#13 ikingili ntuware 2011-01-14 10:09
wewe na makamba wote kamba tu. makamba anacheza na moto na wewe unayemshabikia ni m[NENO BAYA] mwenzio hivyo tukuache tu. ya Askofu yamewagusa mpaka utosini shenzi taipu.
Quote
 
 
0#12 john simon 2011-01-14 10:09
anayeiua ccm ni Makamba,JK mpumzishe
Quote
 
 
0#11 muhammed 2011-01-14 10:06
hayo yakalubandika sidhani kama ni kweli kama kuna mwengine naomba afafanue kwa kituo watu waelewe na atokee askofu sijui wa kanisa gani aongozwe na roho wa kweli afafanue hizo aya zilizotajwa na wachache kwa faida ya wazalendo wananchi.
Quote
 
 
0#10 Malosha 2011-01-14 10:05
HIVIU KATIKA SIASA ZA NCHI HII UNAWEZA KUSEMA MAKAMBA NAYE KIONGOZI?????? KAMA MWL NYERERE NDO ANGEKUWA RAIS ASINGEWEZA KUMWEKA MAKAMBA KWENYE CHEO KAMA HICHO. LAKINI KWA KUWA TUMEWEKA MBELE USWAHILI NDO MAANA NAYE KAPATA ULAJI HUKU UMRI WAKE UKIYOYOMA. MAKAMBA HAFAI KUWA HATA BALOZI WA NYUMBA KUMI

 
0#10 Malosha 2011-01-14 10:05
HIVIU KATIKA SIASA ZA NCHI HII UNAWEZA KUSEMA MAKAMBA NAYE KIONGOZI?????? KAMA MWL NYERERE NDO ANGEKUWA RAIS ASINGEWEZA KUMWEKA MAKAMBA KWENYE CHEO KAMA HICHO. LAKINI KWA KUWA TUMEWEKA MBELE USWAHILI NDO MAANA NAYE KAPATA ULAJI HUKU UMRI WAKE UKIYOYOMA. MAKAMBA HAFAI KUWA HATA BALOZI WA NYUMBA KUMI
Quote
 
 
+1#9 MILELA 2011-01-14 09:54
Kalubandika na Jazi hamjakosea kuonyesha mitizamo yenu juu ya hoja za Ndg Makamba na Maaskofu LAKINI naona nyinyi si watu wazuri kwa taifa hili. Hoja zenu zimejaa UDINI mkubwa jambo ambalo ni hatari kwa mustakabali wa Taifa letu kipenzi la Tanzania. Ningekuwa na mamlaka nyinyi mlitakiwa mkamatwe na ku[NENO BAYA] ndani maana mnaonyesha kila dalili ya kuwa wachochezi hatari na mnaweza kulitia Taifa ktk mtafaruku wa KIDINI.

Kama kweli ninyi ni wapenda amani na ni wazalendo, na mchango wenu juu ya suala la yupi ni sahihi kati ya Maaskofu au Makamba hautawaliwi na hisia za kidini, ingekuwa VEMA kama mgefanya tafakali ya kina juu ya jambo hili. Na tafakali yenyewe haiwezi kufanywa kwa kuanza kuangalia nyuma yalifanyika yapi.
Sitaki kuamini kuwa Chadema ni CHAMA cha kikristo, wala CUF (maana hoja zenu zinaonyesha kuwa CUF wakifanya jambo, Masheikh ndo wanatetea, na CHADEMA wakifanya, Maaskofu wanatetea). Ninayo mengi ya kuhoji lakini itoshe kujiuliza haya, Nini chimbuko la mgogoro wa Arusha? Nini hoja za msingi zinazolalamikiwa? Je walalamika wanawatuhu maaskofu ama masheikh? Je maandamano yalihusisha wakristo au waislam tu? Waliokufa kwenye maandamano walikuwa wakristo pekee au waislam pekee? Je viongozi wa kidini wa aina zote sio sehemu ya jamii? Na iweje kuhubiri mema bila kukemea maovu?

Chonde watanzania, hii nchi ni yetu sote, likitokea la kutokea haliangalii dini ya mtu, cheo cha mtu wala anakotoka. Acheni kuwa na hisia za udini. Ni mbaya sana!!!
Quote
 
 
-8#8 Kalubandika 2011-01-14 08:22
Asante Makamba japo csapoti mauaji lkn ww ni mwalimu lkn mbona hamuwakumbushi kuwa walio uwawa mwembe chai,zanzibar kuwa ni bnaadamu pia.wamesahau kuwa wao ndio waliosema polisi wana haki ya kujilinda pia,na baba yao pengo alisema hata jiwe linaua pia ama cvyo hivyo?au leo jiwe limebadilika hali ui acheni unafiki semeni ukweli.nahata wale wnao sema maaskofu waombwe radhi ni washenzi wakubwa kwani ni mara ngapi mashekh wameambiwa wavue kanzu wapende kwenye majukwa?ni vp sheikh mbukuzi aliwekwa rumande lkn hawa kusikika wakisema mashekh waombwe radhi,au ndio walipo kuwa wakiambiwa nyoka huyo wanasema naapite kwa kuwa walikuwa hawapitii ss yupo kwao ndio wanaruka.au kwakuwa chadema ni chama chao,na baadhi ya wanasiasa wa ccm mchana wanakuwa ccm ucku chadema,hata huyo sebodo ni mnafiki na mbeya anaye jikomba kwa chadema akitegemea kunasiku wataingia madarakani wampe nafasi,kama ni ubinadamu inamaana chadema ni watu peke yao?cuf,waislamu walikuwa wanyama mbona hawakuwasidia waliwaachia waislamu wakapiga kelele pekeyao,ama kweli nyani haoni [NENO BAYA]le asante makamba.waambie nao wavae makombati wawe chadema rasmi.
Quote
 
 
-12#7 jazi 2011-01-14 08:13
mgosi makamba nena, hao wanaotaka kuabudiwa kwa sababu ya majoho yao ya kiroho nchi hii haina nafasi hiyo, kwani wasijifanye kana wanajua kila kitu na kua ni watakatifu, watulie, wasiipeleke nchi puta, ukitaka siasa vua joho la kiroho vaa la siasa, maana katika siasa watu wanapeana kali, sasa nyie mkipewa kali mnasema mnavunjiwa heshima , ukitaka usivunjiwe heshima basi usivunje heshima
Quote
 
 
+4#6 Asante Mungu 2011-01-14 07:59
Makamba hiyo ni kunikuu tuu lakini maaana yake halisi hauijiu na kuambiwa kuwa unauelewa finyu ni vema ukaenda mbele na sio kuchukua moja kwa moja toka kwenye bibilia.
Quote
 
 
+2#5 mashingo 2011-01-14 07:54
Makamba akae kimya .Asibishane na Maasikofu.
Quote
 
 
+5#4 mashingo 2011-01-14 07:51
Mzee makamba kweli umeshakuwa zee. mambo unayoongea ni tofauti na ilivyo. sauti ya Mungu ni ile sauti ya watu wengi. pia na yale makubaliano ya katiba ya nchi yetu. nakuomba ukae kimya mzee.
Quote
 
 
+3#3 Keddy 2011-01-14 07:11
Makamba, hukurupuka tu, you cant argue with bishops. Kwani Makamba ni nani? amechangia nini katika maendeleo ya nchi hii kama sio kuinyonya tu? Ana elimu gani, kama sio basic certificate ya ualimu. Ni aibu kwa CCM kuongozwa na mtendaji ambaye hana management and administrative skills. Hata kwenye ukuu wa mkoa alikua hana muelekeo katika maamuzi yake. Roho za watanzania zinaumia kwa sababu ya huyu mtu anaitwa Makamba. Ana mwisho wake, sijui atajificha wapi baada ya kutoka kwennye majengo ya kijani. Na bahati mbaya sana, maamuzi yake mabovu yatatufanya tusiamini mtu yoyote mwenye surname ya Makamba!!
Quote
 
 
-8#2 Nduli-la-Mizimwi 2011-01-14 06:19
Asante Makamba mpe dozi huyo Padre ambaye mwenyewe ana uelewa finyu wa Biblia. LAU tu Raisi wetu angekuwa na ujasiri wa Makamba leo tusingefikia umwagaji huu wa damu na vurumai inayoendelea kisiasa. JK mwambie Makamba akupe somo. Nawatakia maangamizi ya haraka wewe na Katibu wako.
Quote
 
 
+1#1 MWANADEMOCRASIA 2011-01-14 03:20
HII INAMAANA MAUAJI YA WATU MKOANI ARUSHA NI YA KIMAKUSUDI. YALIPANGWA NA TANZANIA IMESHAKUWA NCHI YA KIJESHI NA DEMOCRASIA IMEKUFA... WANACHOAMUA WACHACHE SERIKALINI NDICHO KINADUMU NA KISIPINGWE... SIJUI TUNAPOELEKEA SASA HIVI kama nchi ni wap? ILA NINACHOJUA NI KWAMA MSIMAMO HUU UNATISHA NA KAMA MAKAMBA ATAACHIWA KUENDELEA NA MANENO YAKE NA YAKADUMISHWA NA CCM BASI HAKI ZA BINADAMU ZITAENDELEA KUVUNJWA NCHINI. WASOMI HII KWELI IMEKAAJE??
Quote
 
Tags:

0 comments

Post a Comment