Subscribe to receive latest Updates

Online :

You Are Here: Home - - Dr. Bilal aomba viongozi wa dini kisaidia kufichua Mafisadi

IDADI YA WATU WALIOSOMA HABARI HII: counter
Image
KATIKA kuhakikisha vita dhidi ya rushwa nchini inafanikiwa, Makamu wa Rais Dk. Mohamed Gharib Bilal, amewataka Watanzania kuhakikisha mwaka huu wanafichua viongozi wanaoendekeza vitendo vya rushwa. 

Aidha, amewataka viongozi wa dini kuendelea kukemea uozo wa rushwa na mmomonyoko wa maadili kwa jumla, huku akionya kwamba, nguvu ya pamoja isipotumika, kuna hatari ya wananchi kukosa haki zao za msingi. 

Dk. Bilal alisema hayo usiku wa kuamkia jana wakati wa Mkesha wa Dua Maalamu kwa Taifa uliofanyika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam kwa ajili ya kuuaga mwaka 2010 na kuukaribisha mwaka 2011. 

Alisema hatua ya wananchi kushiriki kufichua viongozi wala rushwa, itasaidia kupambana na tatizo sugu la rushwa ambalo ni miongoni mwa matatizo yanayotoa changamoto kwa Serikali kuimarisha amani, utulivu na mshikamano. 

"Watu wengi wamekuwa wakihoji upungufu wa maadili miongoni mwa watu wengi, ni kweli kuwa unaotokana na rushwa ambayo ni moja ya changamoto dhidi ya amani, utulivu na mshikamano. 

Serikali imedhamiria kwa dhati kupambana na tatizo hilo kwa kuendelea na mikakati madhubuti yenye lengo la kuitokomeza. 

Image
Makamu wa Rais, Dk Mohammed Gharib Bilal (kushoto) akipokewa na Askofu Godfrey Malassy wakati wa ibada ya mkesha maalumu wa Mwaka Mpya iliyoandaliwa na Umoja wa Kikristu kuombea Amani ya Tanzania iliyofanyika Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam, juzi. Katikati ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Jordan Rugimbana. (Picha na Robert Okanda).

Habari Zaidi:
  • JK apongezwa kuridhia Katiba
  • Bilal ataka mafisadi wafichuliwe
  • Karume: Kanisa halina haki umiliki wa kiwanja
  • Wakala pembejeo, wenzake mbaroni
  • Mbunge akunwa na hotuba ya JK
  • Wataka wahanga ukatili wa jinsia wajumuishwe
  • Mbunge ajitolea kusomesha 680 Masasi
  • Nyangwine apigia hesabu majimbo ya wapinzani 2015
  • Aliyekeketwa na mumewe aomba msaada wa kisheria
  • Kilimanjaro yaaswa kutozika kwenye mibuni
  • Ajiua Mkesha wa Mwaka Mpya kwa ugumu wa maisha
  • Mama afukua mwili wa mwanawe, azika upya
  • Mbunge Bahi awatangazia kiama wakandarasi `uchwara'
  • Wazazi waondoa kero ya vyoo sekondari
  • Barabara Iramba zatafuna milioni 660/
  • JK aridhia Katiba Mpya
  • Majambazi wamfanyia unyama mtoto mchanga
  • Bili yamponza aliyejirusha ghorofani
  • Wazanzibari watakiwa kuwajibika
  • Damu chafu yagundulika kwenye zahanati

  • Habari zinazosomwa zaidi:
  • Balaa lingine kwa Chenge
  • Salama: Jasiri aliyetangaza kuishi na virusi vya Ukimwi
  • Dina Marius, mrithi wa Amina Chifupa
  • 'Housigeli' anataka kuniharibia ndoa
  • Vatican yamvua jimbo Askofu
  • Kikwete achekecha wakuu wa wilaya
  • Waliochaguliwa kujiunga kidato cha tano waongezeka kwa 22%
  • Interpol yatumika kusaka wenye zeutamu
  • Orijino Komedi, Jay Dee waitwa Iringa
  • JK apigilia msumari wa mwisho Dowans
  • KATIKA kuhakikisha vita dhidi ya rushwa nchini inafanikiwa, Makamu wa Rais Dk. Mohamed Gharib Bilal, amewataka Watanzania kuhakikisha mwaka huu wanafichua viongozi wanaoendekeza vitendo vya rushwa. 

    Aidha, amewataka viongozi wa dini kuendelea kukemea uozo wa rushwa na mmomonyoko wa maadili kwa jumla, huku akionya kwamba, nguvu ya pamoja isipotumika, kuna hatari ya wananchi kukosa haki zao za msingi. 

    Dk. Bilal alisema hayo usiku wa kuamkia jana wakati wa Mkesha wa Dua Maalamu kwa Taifa uliofanyika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam kwa ajili ya kuuaga mwaka 2010 na kuukaribisha mwaka 2011. 

    Alisema hatua ya wananchi kushiriki kufichua viongozi wala rushwa, itasaidia kupambana na tatizo sugu la rushwa ambalo ni miongoni mwa matatizo yanayotoa changamoto kwa Serikali kuimarisha amani, utulivu na mshikamano. 

    "Watu wengi wamekuwa wakihoji upungufu wa maadili miongoni mwa watu wengi, ni kweli kuwa unaotokana na rushwa ambayo ni moja ya changamoto dhidi ya amani, utulivu na mshikamano. 

    Serikali imedhamiria kwa dhati kupambana na tatizo hilo kwa kuendelea na mikakati madhubuti yenye lengo la kuitokomeza. 

    "Rushwa ni adui wa haki, kwani ni tatizo linaloleta dhuluma, uonevu, uhasama, utengano, umasikini miongoni mwa jamii. 

    Zipo sheria za nchi zinazokataza hili, lakini kuondoka kwake kutatokana na kwa kila mmoja wetu kulipiga vita. 

    "Kipindi hiki cha Mwaka Mpya tusipokuwa makini kuna hatari ya wananchi kukosa haki zao, hivyo ni vema wananchi wakafichua viongozi wanaoendeleza rushwa kwa njia mbalimbali." 

    Aliongeza: "Serikali yetu inathamini mchango wa viongozi wa dini wa kukemea rushwa na vitendo viovu vinavyowafanya wananchi kukosa haki na kuhatarisha amani, hivyo endeleeni na mapambano hayo." 

    Akizungumzia umasikini unaowakabili wananchi wengi, alisema Serikali imechukua hatua kadhaa ikiwamo ya kuanzisha mpango wa Mkukuta (wa Kupambana na Kuondoa Umasikini). 

    "Tunazipongeza jumuiya za dini kwa kusaidia kuhamasisha waumini katika jitihada za kuondokana na umasikini kwa kuendesha na kuendeleza miradi ya kujikwamua kimaisha, kwani hakuna njia ya mkato, bali ni kila mmoja kufanya kazi kwa bidii na maarifa." 

    Alikemea pia tabia ya baadhi ya watu kugeuza vyama vingi kuwa mapambano na kujenga chuki na uhasama na utengano kati ya wananchi dhidi ya Serikali na wao wenyewe. 

    Bilal alisema uchaguzi si jambo la mapambano wala si fursa ya watu kujenga na kupandikiza chuki, uhasama na utengano miongoni mwa wananchi au dhidi ya Serikali. 

    Hata hivyo, Bilal ambaye aliingia uwanjani hapo saa 5.30 usiku alitoa mwito kwa Watanzania kujenga utamaduni wa kushindana kwa sera na fikra badala ya kuendeleza chuki, fitna, uhasama na utengano miongoni mwa Watanzania. 

    Mbali na Dar es Salaam pia mkesha kama huo ulifanyika Zanzibar, Kilimanjaro, Arusha, Tabora, Dodoma, Kagera, Ruvuma, Mbeya, Iringa, Tanga, Mwanza na Mtwara. 

    Mwenyekiti wa Taifa wa Kamati ya Maandalizi ya Mkesha huo, Askofu Godfrey Malasi alisema pamoja na Mungu kuibariki Tanzania katika maliasili, lakini imekuwa inakabiliwa na matatizo ya umasikini, rushwa, magonjwa, matendo maovu, kugawanyika kwa familia, uonevu dhidi ya watoto, uchawi, ushirikina, ushoga na usagaji.

    Tags:

    0 comments

    Post a Comment