Hatimaye lile bonge la Tamasha linalokwenda kwa jina la Straight Music Klimax limesababishwa usiku wa kuamkia leo ndani ya viwanja vya Golf vya GYMKHANA Jijini Dar es Salaam, na kuandika historia ya kipekee kutokana na kuporomoshwa kwa shoo ya maana kutoka kwa wasanii kibao wa kimataifa na kitaifa.
Ilikuwa ni full shangwe wakati wasanii walipoanza kusababisha jukwaani ambapo aliyefungulia ni Mchizi kutoka pande za East Zuu Albert Mangwea ‘Cow Boy’, kiasha akapanda Joh Makini ‘Mwamba wa Kaskazini’ na kufuatiwa na Mr.Blue ‘Kabaizer’ halafu Prof Jizey kisha upande wa wasanii wa Bongo ulihitimishwa na maswahiba wawili AY na Mwana FA.
Baada ya kimya cha muda mrefu, jana umma ulimshuhudia aliyekuwa kiongozi wa kundi la East Coast Team (ECT) King Crayz GK alitokea jukwaani kama mzimu na kuungana na machizi wake ambapo liliibuka bonge la shangwe kwa mchizi huyo.
Baada ya hapo alifuata jukwaani mwanadada EVE ambaye alitikisa kisawasawa kabla ya kumpisha FAT JOE a.k.a THE DON ambaye alikimbiza vilivyo na kuwapisha P-Square kutoka Nigeria ambao walihitimisha mzuka wa KLIMAX 2008.
Zama chini ucheki mapicha jinsi mzuka ulivyokuwa.
Picha zote na Christopher Lissa na Richard Bukos GPL.
| ||||
NI KAMA NGOMA...
|
Usiku wa kuamkia leo, katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam, Rais wa Jakaya alibariki sherehe za kutimiza miaka mitatu ya kikundi cha muziki nchini, Tanzania House of Talent (THT), sherehe ambazo zilienda pamoja na burudani na risala iliyosomwa na mwanamuziki Lady Jaydee kwa Rais kwa niaba ya wasanii wa Bongo Flava. Pamoja na mambo mengine, katika risala yao wasanii wameiomba Serikali iwasaidie kujenga 'Professional Mastering Studio', ombi ambalo Rais ameahidi kulitekeleza.
|
Sasa ni dhahiri Serikali ya awamu ya nne inakabiliwa na dhoruba kubwa na Rais Jakaya Kikwete itabidi achukue maamuzi mazito ili kuhakikisha analifikisha Taifa kwenye kile kinachoitwa Demokrasia ya Kweli inayoheshimu Utawala wa Sheria na maadili ya Umma na zaidi kurejesha imani ya wapiga kura kwa serikali yake... |



0 comments