Uganda itamenyana na wenyeji Tanzania Bara katika nusu fainali ya Kombe la Cecafa siku ya Alhamisi, baada ya timu zote mbili kushinda katika mechi za robo fainali siku ya Jumanne mjini Dar es salaam.
Uganda Cranes waliishinda Zimbabwe 1-0 katika mechi ya kwanza, nao Kilimanjaro Stars wakawafurahisha mashabiki wa nyumbani kwa kuifunga Malawi 1-0 katika robo fainali ya mwisho.
Bao lao la Tanzania Bara la ushindi lilifungwa na Nurdin Bakari katika dakika ya 35, kwa kukamilisha pasi kutoka Mrisho Ngasa.
Tanzania Bara ndio mabingwa watetezi wa kombe hilo.
Zimbabwe waliudhibiti mchezo dhidi ya Uganda lakini wakakosa bahati ya kufunga.
Hamis Kiiza ndiye aliyefungia Uganda bao hilo moja.
Nusu fainali nyingine siku ya Alhamisi itakuwa kati ya Sudan na Rwanda.
Uganda Cranes waliishinda Zimbabwe 1-0 katika mechi ya kwanza, nao Kilimanjaro Stars wakawafurahisha mashabiki wa nyumbani kwa kuifunga Malawi 1-0 katika robo fainali ya mwisho.
Bao lao la Tanzania Bara la ushindi lilifungwa na Nurdin Bakari katika dakika ya 35, kwa kukamilisha pasi kutoka Mrisho Ngasa.
Tanzania Bara ndio mabingwa watetezi wa kombe hilo.
Zimbabwe waliudhibiti mchezo dhidi ya Uganda lakini wakakosa bahati ya kufunga.
Hamis Kiiza ndiye aliyefungia Uganda bao hilo moja.
Nusu fainali nyingine siku ya Alhamisi itakuwa kati ya Sudan na Rwanda.
Matokeo ya mpira wa miguu katika kombe la club bingwa barani Ulaya kama yanavyoonekana katika chati hiyo hapo juu
Kilimanjaro Stars imefanikiwa kuingia nusu fainali ya mashindano hayo baada ya kuifunga Malawi goli1-0 katika kipindi cha Kwanza, lililofungwa na Nurdin Bakari. Leo Kilimanjaro Stars imeonyesha mchezo mzuri ukiacha makosa madogo madogo yaliyojitokeza.
*Yapigwa 2-1 na Rwanda
*Sudan hiyoo nusu fainali baada ya kuilaza Burundi 2-0
SHUTI lililopigwa nje ya eneo la hatari dakika ya 86 na mshambuliaji nyota wa timu ya Taifa ya Rwanda 'Amavubi',
Kagere Meddie lilizima ndoto za Zanzibar 'Zanzibar Heroes' kucheza nusu fainali ya Kombe la Chalenji kwa kuiwezesha timu hiyo kuibuka na ushindi wa mabao 2-1.
Mchezo huo uliokuwa wa kusisimua na wa aina yake kutokana na kiwango kilichooneshwa na Zanzibar Heroes, ulipigwa jana kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kabla ya mchezo huo, ulitanguliwa na robo fainali nyingine ambayo iliwakutanisha timu ya Burundi iliyooneshana kazi na Sudan ambapo Sudan ilitinga nusua fainali kwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-0.
Wachezaji wa Zanzibar Heroes hususani waliocheza katika safu ya ushambuliaji iliyoongozwa na Ali Badr, watajutia nafasi nyingi walizipata katika vipindi vyote lakini hawakuwa makini kukwamisha mpira wavuni.
Kipindi cha kwanza, Zanzibar Heroes walitawala mchezo kwa kiasi kikubwa kutokana na kucheza kwa kujiamini na kupigiana pasi zenye uhakika ambapo dakika ya 15, Badr alitoa pasi safi kwa Abdulhalim Humud lakini shuti alilopiha Humud lilitoka nje.
Zanzibar Heroes iliendelea kutawala mchezo hasa katika kiungo kilichokuwa chini ya Humud na kumpa wakati mgumu kiungo machachari wa Rwanda, Haruna Niyonzima ambaye hakuonekana kama anavyojulikana.
Pamoja na kubanwa huko, Rwanda ambayo ilikuwa kama simba mwenda pole, ilifanya shambulizi la kushtukiza dakika ya 38 na kupata kona ambayo ilizaa matunda baada ya Mugiraneza Baptist kufunga bao kwa kichwa akiunganisha mpira wa kona uliopigwa na Niyonzima.
Baada ya kufunga bao hilo, Rwanda ilionekana kama imeamka usingizi ambapo dakika ya 43, nusura Baptist afunge bao la pili lakini alichelewa kupiga kichwa mpira uliopigwa na Kagere kutokana na pasi ndefu ya Niyonzima.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi na dakika moja baada ya mpira kuanza, Zanzibar Heroes walisawazisha bao lililofungwa na Abdulrahman Mohd dakika chache baada ya kuingia badala ya Suleiman Kassim aliyeumia akiunganisha krosi ya Juma Othman.
Baada ya kufunga bao hilo, timu hiyo iliendelea kuliandama lango la Rwanda huku kwa wapinzani wao wakionekana kuzuia zaidi na mbele kumuacha mshambuliaji wao Olivier Kalekezi ambaye katika mchezo huo hakuwa na madhara kutokana kuwekwa chini ya ulinzi na Nadir Haroub 'Canavaro'.
Zanzibar Heroes dhahiri walionekana kuwa na kiu kubwa ya kucheza nusu fainali tofauti na ilivyotarajiwa na mashabiki wengi, dakika 82 nusura Badr awainua mashabiki wake baada ya kukosa bao la wazi kwa kupiga shuti lililotoka nje akiunganisha pasi ya Mohd.
Mashabiki wengi wakijua timu hizo zitamaliza ubishi katika hatua ya matuta baada ya kuonekana zitatoka sare lakini, Kagere alibadili fikra hizo kwa kupiga shuti nje ya eneo la hatari lililotinga moja kwa moja wavuni na kumuacha kipa Mwadini Ali akiruka bila mafanikio.
Katika mchezo wa kwanza, mabao ya washindi Sudan yalifungwa na Amir Abdenabi dakika ya 40 kwa kichwa akiunganisha krosi ya Khalifa Nakhit na la ushindi lilifungwa na Mohamed Osman kwa shuti kali.
Dakika ya 64, Sudan ilipata pigo baada ya mchezaji wake Nagmeldin Abdallah kutolewa nje kwa kadi nyekundu baada ya kurudishia rafu na mwamuzi Ronnie Kalema kutoka Uganda alimtoa nje.
Robo fainali ya michuano ya 35 ya Kombe la CECAFA Tusker Challenge inaanza leo (Desemba 5) kwa mechi mbili zitakazochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mechi ya kwanza itakayochezwa saa 8.00 mchana itazikutanisha Burundi na Sudan wakati ya pili itakayoanza saa 10.00 jioni itakuwa kati ya Zanzibar (Zanzibar Heroes) dhidi ya Rwanda.
Kesho (Desemba 6) mechi ya kwanza ya robo fainali itakuwa kati ya Uganda na Zimbabwe wakati ya pili itakayoanza saa 10.00 jioni itawakutanisha mabingwa watetezi Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars) na Malawi (The Flames). Mechi zote zitaoneshwa moja kwa moja kupitia SuperSport 9.
Viingilio kwa mechi zote za robo fainali ni sh. 2,000 kwa viti vya kijani na bluu, sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, sh. 10,000 kwa VIP C na B na sh. 15,000 kwa VIP A.
Kesho (Desemba 6) mechi ya kwanza ya robo fainali itakuwa kati ya Uganda na Zimbabwe wakati ya pili itakayoanza saa 10.00 jioni itawakutanisha mabingwa watetezi Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars) na Malawi (The Flames). Mechi zote zitaoneshwa moja kwa moja kupitia SuperSport 9.
Viingilio kwa mechi zote za robo fainali ni sh. 2,000 kwa viti vya kijani na bluu, sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, sh. 10,000 kwa VIP C na B na sh. 15,000 kwa VIP A.

Mwekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema, Freeman Mbowe, akiwapa hai, mashabiki kabla ya kuanza kuchana mistari.
Wasanii wa kizazi kipya waliowahi kutamba zamani waliounda kundi la Vinega wakiongozwa na Mkurugenzi wa Deiwaka Entertainment, Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ (pichani juu) usiku wa kuamkia leo wamefanya onesho lililohudhuriwa na maelfu ya watu katika Viwanja vya Chuo cha Ustawi wa Jamii jijini Dar es Salaam. Yafuatayo ni baadhi ya matukio yaliyojiri kiwanjani hapo:.
...sehemu ya yomi iliyokuwepo
Sister P akikamua.
...Zay B jukwaani
..Daz baba na makamuzi yake
Dj Sox wa Mabaga Fresh
Mkoloni akiwajibika
Mkoloni akiwajibika
Mr. Simple, ambaye pia ni Diwani kwa tiketi ya Chadema
...Kinadada wakifuatilia makamuzi
...Mashabiki wakiwa na mzuka
...Sugu anapoweka pembeni uheshimiwa na kukamata Mic
Kikosi cha Kilimanjaro Stars.
TIMU ya soka ya Taifa ya Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Stars’ jana iliangukia ‘pua’ baada ya kuchapwa bao 1-0 na timu ya taifa ya Rwanda, Amavubi katika mechi ya michuano ya Kombe la Chalenji iliyofanyika kwenye uwanja wa Taifa Dar es Salaam.
PREMIER LEAGUE 2011-2012 - FULL TABLE
| Pos. | Team | Pl | W | D | L | GF | GA | +/- | Pts |
|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
| 1 | Manchester City | 12 | 11 | 1 | 0 | 42 | 11 | 31 | 34 |
| 2 | Manchester United | 12 | 9 | 2 | 1 | 29 | 12 | 17 | 29 |
| 3 | Newcastle United | 12 | 7 | 4 | 1 | 18 | 11 | 7 | 25 |
| 4 | Chelsea | 12 | 7 | 1 | 4 | 25 | 17 | 8 | 22 |
| 5 | Tottenham Hotspur | 10 | 7 | 1 | 2 | 21 | 15 | 6 | 22 |
| 6 | Liverpool | 12 | 6 | 4 | 2 | 16 | 11 | 5 | 22 |
| 7 | Arsenal | 12 | 7 | 1 | 4 | 25 | 22 | 3 | 22 |
| 8 | Aston Villa | 11 | 3 | 6 | 2 | 16 | 15 | 1 | 15 |
| 9 | Queens Park Rangers | 12 | 4 | 3 | 5 | 13 | 22 | -9 | 15 |
| 10 | West Bromwich Albion | 12 | 4 | 2 | 6 | 11 | 17 | -6 | 14 |
| 11 | Norwich City | 12 | 3 | 4 | 5 | 17 | 20 | -3 | 13 |
| 12 | Everton | 11 | 4 | 1 | 6 | 13 | 16 | -3 | 13 |
| 13 | Swansea City | 12 | 3 | 4 | 5 | 12 | 16 | -4 | 13 |
| 14 | Stoke City | 12 | 3 | 3 | 6 | 10 | 22 | -12 | 12 |
| 15 | Sunderland | 12 | 2 | 5 | 5 | 14 | 13 | 1 | 11 |
| 16 | Fulham | 12 | 2 | 5 | 5 | 14 | 15 | -1 | 11 |
| 17 | Wolverhampton Wanderers | 12 | 3 | 2 | 7 | 13 | 20 | -7 | 11 |
| 18 | Bolton Wanderers | 12 | 3 | 0 | 9 | 19 | 29 | -10 | 9 |
| 19 | Blackburn Rovers | 12 | 1 | 4 | 7 | 16 | 27 | -11 | 7 |
| 20 | Wigan Athletic | 12 | 1 | 3 | 8 | 10 | 23 | -13 | 6 |






















