Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya tawi la CCM Moscow-URUSI ilimaliza kikao chake cha masaa 3, jioni ya tarehe 23 /02/2012 Mjini Moscow, chini ya Uenyekiti wa Mwenyekiti wa Tawi, Dr Alfred Kamuzora ambapo 80% ya wajumbe wote wa kamati ya Siasa walihudhuria . Kikao hicho cha dharula kiliitishwa kwa Ajenda moja kuu ya utekelezaji wa Maagizo ya HALMASHAURI KUU TAIFA ya CCM “NEC” kuhusu Uchaguzi wa viongozi wa chama cha mapinduzi katika ngazi mbalimbali mwaka 2012,
Kwa Muhtasari huo, Pamoja na mambo mengine Kamati ya siasa ya tawi imeagiza utekelezaji wa mambo yafuatayo, yanayohusu;
1.UCHAGUZI WA VIONGOZI WA JUMUIYA WANAWAKE TAWI LA CCM MOSCOW.
Kwa kuwa Jumuiya ya wanawake tawi ilifanya Uchaguzi , mwezi May 2011 ,na kwa kuwa Uchaguzi huo ulizingatia vigezo vya Uchaguzi kwa wagombea na wanachama wa Jumuiya husika na kuufanya uchaguzi huo kuwa Huru na Haki na Viongozi wapya kuchaguliwa, Kamati ya siasa ya tawi imeridhia KUTOFANYIKA UCHAGUZI MWINGINE NDANI YA JUMUIYA YA WANAWAKE TAWI LA CCM MOSCOW- 2012.
Aidha Kamati ya siasa ya tawi imewataka viongozi wote wapya wa UWT waliochaguliwa , kujaze form maalumu iliyotolewa na NEC ili kukamilisha mchakato huo na kuweka kumbukumbu sahihi ya kiofisi ya viongozi wa chama cha mapinduzi –Makao Makuu , Dodoma Tanzania.
2.UCHAGUZI WA VIONGOZI WA JUMUIYA YA VIJANA YA TAWI (UVCCM)
Kamati ya siasa ya tawi, imeiagiza Jumuiya ya Vijana ya tawi chini ya mwenyekiti wake Bw. Mahomoud Mbarouk , Kuhakikisha Uchaguzi wa Viongozi wapya wa Jumuiya hiyo uwe UMETEKELEZWA ifikapo tarehe 25/3/2012. Aidha kamati ya Siasa imeanisha nafasi za kugombea Uongozi ndani ya Jumuiya hiyo ni kama ifuatavyo:-
i) Mwenyekiti wa Jumuiya ya Vijana ,Tawi la CCM Moscow.
ii) Katibu wa Jumuiya ya Vijana ,Tawi la CCM Moscow.
iii) Katibu wa Fedha na Uchumi wa Jumuiya ya Vijana , Tawi la CCM Moscow.
iv) Katibu wa Uhamasishaji wa Jumuiya ya Vijana , Tawi la CCM Moscow.
v) Wajumbe 15 wa Baraza la Vijana la Jumuiya ya Vijana wa CCM Moscow.
Form za Kugombea Nafasi tajwa hizo za Uongozi wa UVCCM ,zinapatikana kwa Katibu wa Jumuiya ya Vijana wa tawi Bw.OCTAVIAN NYALALI.
3. UCHAGUZI MKUU WA VIONGOZI, NGAZI YA TAWI LA CCM MOSCOW- 2012.
Kwa kuzingatia maagizo na malekezo ya kalenda ya Uchaguzi wa Viongozi wa CCM ngazi ya Matawi iliopitishwa na NEC , kilele cha chaguzi hizo ni tarehe 28/4/2012. Kwa zingatio la kalenda hiyo, kamati ya siasa ya tawi imepanga Utaratibu stahiki kuhakikisha zoezi hilo la Uchaguzi linafanyika katika mazingira mapana ya huru na haki na kukuza Demokrasia ndani ya chama cha mapinduzi kama ifuatavyo:
Tarehe 15-22/4/2012:- Zoezi la Uchukuaji na Urejeshwaji wa FOM ZA WAGOMBEA kwa ngazi mbalimbali za Uongozi wa CCM, Tawi la Moscow Urusi.
Tarehe 25/4/2012:- Taarifa kwa wanachama wa CCM tawi kuhusu MAJINA ya Wanachama wa CCM, wanaomba ridhaa ya kuongoza TAWI LA CCM MOSCOW.
Tarehe 28/4/2012:- Uchaguzi Mkuu wa Viongozi NGAZI YA TAWI LA CCM MOSCOW.
Kamati ya siasa ya Tawi, imeanisha nafasi za Kugombea Uongozi ngazi ya Tawi kama ifuatavyo:
i) Mwenyekiti wa Tawi la CCM Moscow.
ii) Katibu wa Tawi la CCM Moscow.
iii) Katibu wa Fedha na Uchumi wa Tawi la CCM Moscow
iv) Katibu wa Sera na Uenezi wa Tawi la CCM Moscow
v) Wajumbe 5 wa kamati ya Siasa ya Tawi.
vi) Wajumbe 12 wa Halmashauri kuu ya Tawi la CCM Moscow.
Form za Kugombea nafasi hizo tajwa zinapatika toka kwa Katibu wa Sera na Uenezi wa Tawi la CCM Moscow Ndg. KOLOA KASSIM, (+79260327055).
4. Kamati ya Siasa Imeaigiza Sekretarieti ya Tawi chini ya idara yake ya SERA NA UENEZI, kusimamia na kuhamasisha wanachama wa chama cha mapinduzi kujitokeza kwa wingi kushiriki zoezi hili muhimu la Uchukuaji form na Uchaguzi wa Viongozi wa Tawi letu kwa kuzingatia misingi ya CCM.
5. Kamati ya Siasa ya Tawi inawakumbusha wana chama wote ambao hawajapata Kadi za Uanachama , wakamilishe mchakato wa kujaza form ya kuomba Uanachama na Picha 2 “passport size” , na kumkabidhi Ndg Kassim Koloa – Katibu wa Sera na Uenezi wa Tawi , ili waweze kupatiwa kadi ya Chama na ya Umoja wa Vijana UVCCM.
Mwisho, Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya CCM Tawi inatarajiwa kukutana wakati wowote kipindi cha Mwezi April 2012 ambapo pamoja na mambo mengine itatathimini utekelezaji wa maamuzi yake.
Imethibitishwa na kutolewa na Ofisi ya Katibu wa Tawi;
MAKAO MAKUU, TAWI LA CCM MOSCOW.
SHIRIKISHO LA URUSI.
Email: ccmmoscow@gmail.com . Website: ccmmoscow.blogspot.com.
Kwa Muhtasari huo, Pamoja na mambo mengine Kamati ya siasa ya tawi imeagiza utekelezaji wa mambo yafuatayo, yanayohusu;
1.UCHAGUZI WA VIONGOZI WA JUMUIYA WANAWAKE TAWI LA CCM MOSCOW.
Kwa kuwa Jumuiya ya wanawake tawi ilifanya Uchaguzi , mwezi May 2011 ,na kwa kuwa Uchaguzi huo ulizingatia vigezo vya Uchaguzi kwa wagombea na wanachama wa Jumuiya husika na kuufanya uchaguzi huo kuwa Huru na Haki na Viongozi wapya kuchaguliwa, Kamati ya siasa ya tawi imeridhia KUTOFANYIKA UCHAGUZI MWINGINE NDANI YA JUMUIYA YA WANAWAKE TAWI LA CCM MOSCOW- 2012.
Aidha Kamati ya siasa ya tawi imewataka viongozi wote wapya wa UWT waliochaguliwa , kujaze form maalumu iliyotolewa na NEC ili kukamilisha mchakato huo na kuweka kumbukumbu sahihi ya kiofisi ya viongozi wa chama cha mapinduzi –Makao Makuu , Dodoma Tanzania.
2.UCHAGUZI WA VIONGOZI WA JUMUIYA YA VIJANA YA TAWI (UVCCM)
Kamati ya siasa ya tawi, imeiagiza Jumuiya ya Vijana ya tawi chini ya mwenyekiti wake Bw. Mahomoud Mbarouk , Kuhakikisha Uchaguzi wa Viongozi wapya wa Jumuiya hiyo uwe UMETEKELEZWA ifikapo tarehe 25/3/2012. Aidha kamati ya Siasa imeanisha nafasi za kugombea Uongozi ndani ya Jumuiya hiyo ni kama ifuatavyo:-
i) Mwenyekiti wa Jumuiya ya Vijana ,Tawi la CCM Moscow.
ii) Katibu wa Jumuiya ya Vijana ,Tawi la CCM Moscow.
iii) Katibu wa Fedha na Uchumi wa Jumuiya ya Vijana , Tawi la CCM Moscow.
iv) Katibu wa Uhamasishaji wa Jumuiya ya Vijana , Tawi la CCM Moscow.
v) Wajumbe 15 wa Baraza la Vijana la Jumuiya ya Vijana wa CCM Moscow.
Form za Kugombea Nafasi tajwa hizo za Uongozi wa UVCCM ,zinapatikana kwa Katibu wa Jumuiya ya Vijana wa tawi Bw.OCTAVIAN NYALALI.
3. UCHAGUZI MKUU WA VIONGOZI, NGAZI YA TAWI LA CCM MOSCOW- 2012.
Kwa kuzingatia maagizo na malekezo ya kalenda ya Uchaguzi wa Viongozi wa CCM ngazi ya Matawi iliopitishwa na NEC , kilele cha chaguzi hizo ni tarehe 28/4/2012. Kwa zingatio la kalenda hiyo, kamati ya siasa ya tawi imepanga Utaratibu stahiki kuhakikisha zoezi hilo la Uchaguzi linafanyika katika mazingira mapana ya huru na haki na kukuza Demokrasia ndani ya chama cha mapinduzi kama ifuatavyo:
Tarehe 15-22/4/2012:- Zoezi la Uchukuaji na Urejeshwaji wa FOM ZA WAGOMBEA kwa ngazi mbalimbali za Uongozi wa CCM, Tawi la Moscow Urusi.
Tarehe 25/4/2012:- Taarifa kwa wanachama wa CCM tawi kuhusu MAJINA ya Wanachama wa CCM, wanaomba ridhaa ya kuongoza TAWI LA CCM MOSCOW.
Tarehe 28/4/2012:- Uchaguzi Mkuu wa Viongozi NGAZI YA TAWI LA CCM MOSCOW.
Kamati ya siasa ya Tawi, imeanisha nafasi za Kugombea Uongozi ngazi ya Tawi kama ifuatavyo:
i) Mwenyekiti wa Tawi la CCM Moscow.
ii) Katibu wa Tawi la CCM Moscow.
iii) Katibu wa Fedha na Uchumi wa Tawi la CCM Moscow
iv) Katibu wa Sera na Uenezi wa Tawi la CCM Moscow
v) Wajumbe 5 wa kamati ya Siasa ya Tawi.
vi) Wajumbe 12 wa Halmashauri kuu ya Tawi la CCM Moscow.
Form za Kugombea nafasi hizo tajwa zinapatika toka kwa Katibu wa Sera na Uenezi wa Tawi la CCM Moscow Ndg. KOLOA KASSIM, (+79260327055).
4. Kamati ya Siasa Imeaigiza Sekretarieti ya Tawi chini ya idara yake ya SERA NA UENEZI, kusimamia na kuhamasisha wanachama wa chama cha mapinduzi kujitokeza kwa wingi kushiriki zoezi hili muhimu la Uchukuaji form na Uchaguzi wa Viongozi wa Tawi letu kwa kuzingatia misingi ya CCM.
5. Kamati ya Siasa ya Tawi inawakumbusha wana chama wote ambao hawajapata Kadi za Uanachama , wakamilishe mchakato wa kujaza form ya kuomba Uanachama na Picha 2 “passport size” , na kumkabidhi Ndg Kassim Koloa – Katibu wa Sera na Uenezi wa Tawi , ili waweze kupatiwa kadi ya Chama na ya Umoja wa Vijana UVCCM.
Mwisho, Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya CCM Tawi inatarajiwa kukutana wakati wowote kipindi cha Mwezi April 2012 ambapo pamoja na mambo mengine itatathimini utekelezaji wa maamuzi yake.
Imethibitishwa na kutolewa na Ofisi ya Katibu wa Tawi;
MAKAO MAKUU, TAWI LA CCM MOSCOW.
SHIRIKISHO LA URUSI.
Email: ccmmoscow@gmail.com . Website: ccmmoscow.blogspot.com.
![]() |
| Baraza la Mawaziri |
Boniface Meena
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimemtaka Rais Jakaya Kikwete kulivunja Baraza la Mawaziri kwa maelezo kwamba limeshindwa kumshauri hivyo kusababisha hali ngumu ya maisha na kuyumba kwa uchumi wa nchi huku, migogoro ikiendelea kushamiri.Tamko hilo la Chadema linakuja kipindi ambacho tayari madaktari wametoa siku tatu kwa Serikali wakitaka kung'olewa kwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hadji Mponda na naibu wake, Dk Lucy Nkya kutokana na kushindwa kusimamia sekta ya afya nchini.
Akisoma maazimio ya kikao cha Kamati Kuu (CC) ya chama hicho iliyoketi juzi jijini Arusha, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa chama hicho, John Mnyika, alisema Chadema pia kinamtaka Rais Kikwete kufumua maeneo mengine ya Serikali yake kwa kuwa mfumo wake ni mbovu usiokidhi haja ya kutekelezwa kwa majukumu yake.
Mnyika akisoma maazimio hayo jijini Dar es Salaam jana alisema, "Kamati Kuu haijaridhishwa na jinsi Serikali inavyoshughulikia suala la uchumi na hali tete ya kisiasa ikiwa ni pamoja na migogoro mbalimbali na hiyo inatokana na uwezo mdogo wa mawaziri wa JK."
Alisema CC ya Chadema haijaridhishwa na jinsi Serikali ya Rais Kikwete inavyoshughulikia mambo mbalimbali nchini na hilo linatokana na mkuu huyo wa nchi kukosa washauri wazuri katika baraza lake la mawaziri.
Mnyika ambaye pia ni mbunge wa Ubungo alisisitiza, "Rais aanze na baraza lake la mawaziri kwa kulivunja kisha aende kwenye ngazi mbalimbali ambazo ameteua viongozi wabovu, awaondoe."
Alisisitiza, "Na hii inatokana na katiba tuliyonayo kumpa nafasi ya kuchagua watu kadri anavyotaka."
Mnyika alifafanua kwamba ili kupunguza makali na machungu kwa wananchi yanayosababishwa na uongozi huo mbovu, ni lazima Rais aanzie kwenye chombo chake kinachomshauri ili aweze kurekebisha mfumo mbovu uliopo.
"CC imezungumzia suala la migogoro inayotokea nchini na kuona kuwa Serikali inashindwa kushughulikia vyanzo vya migogoro hiyo. Hivyo ni lazima ishughulikie vyanzo vya migogoro na kuacha masihara kwenye hilo,"alisema Mnyika.
Mnyika alisema kutokana na hali ya uchumi na siasa kuwa tete CC imeamua kuwa Baraza Kuu la Chadema litakalokaa Aprili mwaka huu lijadili hali hiyo na kutoa mapendekezo kwa Serikali jinsi ya kurekebisha mambo kama Rais hatalivunja baraza hilo ambalo limekuwa mzigo kwa nchi.
Kuhusu Katiba
Akizungumzia msimamo wa CC kuhusu utoaji wa maoni ya marekebisho ya Katiba, Mnyika alisema wametambua kuwa marekebisho yaliyofanyika kwenye mkutano wa Bunge wa ulioisha Februari 10 mwaka huu kama ni ya awali hivyo CC inataka Serikali kuendelea na awamu ya pili ya mchakato huo.
"Taarifa kuhusu suala la katiba CC inatambua kuwa marekebisho yaliyofanyika kwenye mkutano wa Bunge ni ya awali hivyo inataka Serikali kuendelea na awamu ya pili na marekebisho yake kufanyika Bunge lijalo la Aprili mwaka huu,"alisema Mnyika.
Alisema CC imeamua kuwa Chadema itaendelea kutoa elimu ya marekebisho ya katiba kwenye mikutano yake, ili kuwafungua wananchi waweze kutoa maoni kikamilifu katika mchakato wa kupata Katiba mpya.
Mnyika alisema kutokana na wito wa Rais Kikwete kutaka majina kutoka kwa vyama ya watu watakaoingia katika tume ya mchakato wa katiba, Chadema imekaribisha maombi na mapendekezo ya watakaotaka kuingia kwenye tume hiyo.
"Kama Serikali ilivyotamgaza kuanza kwa tume hiyo kila chama kimetakiwa kuwa na wawakilishi watatu, Chadema inakaribisha maombi na mapendekezo na mwisho wa kupokea maombi hayo ni Machi 11 mwaka huu ili tuweze kufanya utaratibu,"alisema Mnyika.
Uchaguzi wa chama, Arumeru
Mnyika alisema Baraza Kuu la Chadema litakaa Aprili 29 mwaka huu na kutangaza tarehe za kufanyika kwa uchaguzi wa ndani wa chama kuanzia ngazi ya chini hadi taifa.
Alisema pia Baraza Kuu litapitisha bajeti ya mpango mkakati wa muda mrefu wa chama hivyo viongozi wote wa chama walioko katika ngazi mbalimbali wajiandae kuwasilisha maoni yao.
"Kuhusu uchaguzi wa ndani ya chama CC imeamua Baraza Kuu lifanyike Aprili 29 mwaka huu na kwamba nafasi mbalimbali za uongozi kuanzia ngazi ya mtaa, kijiji, kitongoji, kata kwenda juu zitawaniwa,"alisema Mnyika.
Kuhusu bajeti ya uchanguzi mdogo wa ubunge jimbo la Arumeru Mashariki, Mnyika alisema chama kimeamua kuwa kampeni za uchaguzi huo ziendeshwe kwa nguvu ya umma bila kutegemea ruzuku za chama.
Alisema chama kimejipanga kupata misaada kutoka kwa wananchi wa Arumeru na wananchi wengine nchini katika kuhakikisha hakitumii ruzuku ya chama kwenye uchaguzi huo.
"Kampeni za Arumeru zitaendeshwa kwa nguvu ya umma ikiwa ni pamoja na kupata fedha za wananchi kote nchini na si kutegemea ruzuku za chama bali za wananchi kwa ujumla na hasa Arumeru,"alisema Mnyika.
Alisema chama kimeteua watu kadhaa wa kuangalia jinsi gani ya kupata fedha hizo za nguvu ya umma na kile kiasi ambacho kitahitajika kuongezeka chama kitatangaza kiasi gani kitatumika.
a
The escalating conflict around Iran should be contained by common effort, otherwise the promising Arab Spring will grow into a “scorching Arab Summer,” says Dmitry Rogozin, Russia’s deputy prime minister and former envoy to NATO.
“Iran is our close neighbor, just south of the Caucasus. Should anything happen to Iran, should Iran get drawn into any political or military hardships, this will be a direct threat to our national security,” stressed Rogozin.
Dmitry Rogozin, who served as Russia’s special envoy to NATO in 2008-2011, was appointed deputy prime minister by Vladimir Putin in December. On Friday he was bidding farewell to his NATO colleagues in the alliance’s headquarters in Brussels.
As for Syria, if NATO persists in interfering in its affairs, a catastrophe will be hard to avoid, said Rogozin, talking to journalists on the premises of the Russian mission to the alliance.
“The example of Libya should have cooled everybody down in matters dealing with foreign civil wars,” he said, stressing that this is his personal point of view.
“Syria must be left alone and the sides to the conflict must be assisted in breaking the stand-off and starting negotiations. No one must interfere with Syria. This is dangerous,” added Rogozin.
The West’s attempts to improve democracy in the Middle East and North Africa have resulted in Islamists coming to power. It is now up to the West to decide how comfortable they feel with neighbors who determine their politics with Sharia law, says Rogozin.
“If we add the escalating tensions around Iran to the situation in Syria and the consequences of the Libyan war, then the upcoming 'scorching' Arab Summer, which is following the Arab Spring, will hardly be to anyone’s taste.”
Russia’s response will make AMD ‘a waste of money’
Despite his recent promotion, Rogozin is still in charge of Russia-NATO discussions on anti-missile defense (AMD) issues.
A legal binding that the European and American missile defense systems will not target Russia has not been taken off the table, Rogozin pointed out.
“It seems strange that it is Russia who is required to show flexibility. This is not our project. If an architect is building a house, it is up to him to offer a design which would not violate property rights, area design and neighbors’ interests. So it is our US colleagues who should demonstrate miraculous flexibility to ensure that their AMD system does not violate the interests of other countries if it is to be located in Europe.”
Rogozin also called on European leaders to stop being “political puppets” in the AMD game, adding that everyone should stand for their own interests, not for some “Atlantic solidarity.”
If Moscow’s position is ignored and the range of the US anti-missile defense system covers the European part of Russia, this will be considered a situation requiring defensive action.
“I will certainly ensure Russia will give a corresponding technical response if the AMD system endangers our national interests. This will result in the American AMD being considered a waste of money,” said Rogozin.
Russia has everything needed to annihilate any attempt “to strip” its strategic potential, he added. This also means the era of imported weapons is coming to an end.
In a farewell gesture, Rogozin said he was considering planting a tree in the alliance’s headquarters. Symbolically enough, this would be a poplar, or “topol” in Russian, which brings up associations with Russia’s modern intercontinental ballistic missiles Topol-M.
But NATO replied that planting a tree within the headquarters perimeter “is not possible,” so the tree will have to be planted nearby.
“Iran is our close neighbor, just south of the Caucasus. Should anything happen to Iran, should Iran get drawn into any political or military hardships, this will be a direct threat to our national security,” stressed Rogozin.
Dmitry Rogozin, who served as Russia’s special envoy to NATO in 2008-2011, was appointed deputy prime minister by Vladimir Putin in December. On Friday he was bidding farewell to his NATO colleagues in the alliance’s headquarters in Brussels.
As for Syria, if NATO persists in interfering in its affairs, a catastrophe will be hard to avoid, said Rogozin, talking to journalists on the premises of the Russian mission to the alliance.
“The example of Libya should have cooled everybody down in matters dealing with foreign civil wars,” he said, stressing that this is his personal point of view.
“Syria must be left alone and the sides to the conflict must be assisted in breaking the stand-off and starting negotiations. No one must interfere with Syria. This is dangerous,” added Rogozin.
The West’s attempts to improve democracy in the Middle East and North Africa have resulted in Islamists coming to power. It is now up to the West to decide how comfortable they feel with neighbors who determine their politics with Sharia law, says Rogozin.
“If we add the escalating tensions around Iran to the situation in Syria and the consequences of the Libyan war, then the upcoming 'scorching' Arab Summer, which is following the Arab Spring, will hardly be to anyone’s taste.”
Russia’s response will make AMD ‘a waste of money’
Despite his recent promotion, Rogozin is still in charge of Russia-NATO discussions on anti-missile defense (AMD) issues.
A legal binding that the European and American missile defense systems will not target Russia has not been taken off the table, Rogozin pointed out.
“It seems strange that it is Russia who is required to show flexibility. This is not our project. If an architect is building a house, it is up to him to offer a design which would not violate property rights, area design and neighbors’ interests. So it is our US colleagues who should demonstrate miraculous flexibility to ensure that their AMD system does not violate the interests of other countries if it is to be located in Europe.”
Rogozin also called on European leaders to stop being “political puppets” in the AMD game, adding that everyone should stand for their own interests, not for some “Atlantic solidarity.”
If Moscow’s position is ignored and the range of the US anti-missile defense system covers the European part of Russia, this will be considered a situation requiring defensive action.
“I will certainly ensure Russia will give a corresponding technical response if the AMD system endangers our national interests. This will result in the American AMD being considered a waste of money,” said Rogozin.
Russia has everything needed to annihilate any attempt “to strip” its strategic potential, he added. This also means the era of imported weapons is coming to an end.
In a farewell gesture, Rogozin said he was considering planting a tree in the alliance’s headquarters. Symbolically enough, this would be a poplar, or “topol” in Russian, which brings up associations with Russia’s modern intercontinental ballistic missiles Topol-M.
But NATO replied that planting a tree within the headquarters perimeter “is not possible,” so the tree will have to be planted nearby.
SAKATA la kuvuliwa uanachama kwa mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila limezidi kuibua mjadala baada ya Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi Samuel Ruhuza kumjibu Msajili wa Vyama vya Siasa, John Tendwa kwa kusema anatoa kauli za kukurupuka.
Kwa upande wake, Kafulila amesisitiza kuwa yeye bado ni mbunge, licha ya chama chake kutangaza kumvua uanachama, mwishoni mwa wiki iliyopita na kwamba anakamilisha taratibu za kwenda jimboni kwake kwa ajili ya ziara ya kikazi.Kauli hizo ni mwendelezo wa mjadala kuhusu hatma ya mbunge huyo, baada ya chama chake cha NCCR - Mageuzi, kumvua uanachama hatua ambayo kikatiba, ikiachwa kama ilivyo inamfanya apoteze ubunge.
"Ninachoweza kusema ni kwamba watu wajue, mimi bado ni mbunge wa Kigoma Kusini na mwishoni mwa wiki hii, naenda huko kwa ziara ya kikazi," alisema Kafulila jana alipokuwa akizungumza na gazeti hili.
Kafulila alisema licha ya uamuzi wa Halmashauri Kuu (NEC) ya NCCR-Mageuzi kumfukuza uanachama, kuna michakato mingi inayoendelea ndani ya chama hicho kuhusu suala hilo.
"Nisingependa kueleza ni michakato gani, lakini ieleweke tu kwamba utekelezaji wa hatua ya kunifukuza ni mchakato usioweza kunifanya nikome sasa kuwatumikia wananchi wake," alisema.
Aliendelea, “bado naendelea na kazi kama Mbunge wa Kigoma Kusini, naomba wananchi watambue hilo.”
Ruhuza amjibu Tendwa
Hata hivyo, Ruhuza akizungumzia ushauri wa Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini kutaka suluhu ya jambo hilo, alisema "Tendwa, ni mtu wa kupenda kukurupuka katika kauli zake."
“Kwanza, siamini iwapo haya maneno yametoka kwenye mdomo wa Tendwa, ila kama ni kweli inatoka mdomoni mwake, basi yeye amekurupuka na mtu anayependa kutoa matamko sawa na mtu aliyetoka usingizini,” alisema Ruhuza.
Alisema ikiwa Tendwa anadai kwamba ofisi yake haikupata mwaliko wa kuhudhuria kikao cha kumng’oa Kafulila, wakati akielewa kilichofanya hivyo ni kikao cha NEC ya chama ambacho yeye, (Tendwa) siyo mjumbe basi matamshi yake yana kasoro.
“Anazungumza kuhusu wajumbe batili, yeye amewajuaje na amewaona wapi? Orodha ya wajumbe wa NEC ipo ofisini kwake, anaelewa kabisa idadi yao na kila kitu, sasa sijui haya maneno anayapata wapi?,” alihoji Ruhuza.
Ruhuza alienda mbali zaidi na kumuita Tendwa kuwa ni mchochezi wa migogoro ndani ya vyama vya siasa akidai kuwa, licha ya kusikia viongozi wa chama hicho wakitukanwa kwa muda mrefu, hakuwahi kuchukua hatua yoyote.
“Halafu leo anasema tutumie busara, kuna wakati alisema tulipata usajili bila kukaguliwa ikabidi tumpeleke mahakamani, akatuomba msamaha. Huyu anakurupuka usingizini anatoa matamko,” alisema Ruhuza.
Ruhuza alimshauri Tendwa kabla ya kuzungumzia suala hilo, asome Katiba ya NCCR – Mageuzi ili kubaini hatua zinazopaswa kuchukuliwa dhidi ya makosa yaliyofanywa na Kafulila.
Mbunge CCM
Mbunge wa Viti Maalum CCM, Sara Msafiri, alisema suala la Kafulila linapaswa kupewa uzito na si kwa mtizamo wa kisiasa pekee.“Utaratibu wa watu 30 kutofautiana na wananchi wa jimbo zima siyo jambo la kufurahia, hili jambo linahitaji busara zaidi,” alisema Msafiri.
Msafiri alisema kitendo cha NCCR-Mageuzi kumteua Hashim Rungwe agombee urais halafu baada ya muda mfupi kumwona hafai hata kuwa mwanachama, kinaonyesha udhaifu mkubwa kwa chama hicho.
“Mtu mliyemsimamisha kugombea urais hata mwaka haujaisha, mnamwona hafai tena hata kuwa mwanachama. Hii ni aibu na wananchi wanatakiwa kuwa macho na vyama kama hivi,” alisema Msafiri.
Hata hivyo, Ruhuza alijibu hoja hiyo akisema, “Leo unaweza kuwa na mtoto mzuri sana ,lakini kesho akawa mbaya mno. Kwa hiyo hata sisi mtu akibadilika kinachotakiwa ni kumchukulia hatua.”
Mwishoni mwa wiki iliyopita, wajumbe 38 wa NEC ya NCCR-Mageuzi waliamua kumvua uanachama Kafulila kwa tuhuma za kuongea mambo ya chama nje ya utaratibu wa vikao vya chama.Kafulila mbali ya tuhuma hizo pia alituhumiwa kutaka kufanya mapinduzi ya kumg’oa madarakani mwenyekiti wa chama hicho, James Mbatia.
Hata hivyo, uamuzi huo wa kumvua uanachama umepata upinzani mkali kutoka kwa wasomi na wanasiasa mbalimbali ambao wamenukuliwa wakisema kuwa NCCR- Mageuzi walikurupuka na inafifisha demokrasia ndani ya chama.
Kwa upande wake, Kafulila amesisitiza kuwa yeye bado ni mbunge, licha ya chama chake kutangaza kumvua uanachama, mwishoni mwa wiki iliyopita na kwamba anakamilisha taratibu za kwenda jimboni kwake kwa ajili ya ziara ya kikazi.Kauli hizo ni mwendelezo wa mjadala kuhusu hatma ya mbunge huyo, baada ya chama chake cha NCCR - Mageuzi, kumvua uanachama hatua ambayo kikatiba, ikiachwa kama ilivyo inamfanya apoteze ubunge.
"Ninachoweza kusema ni kwamba watu wajue, mimi bado ni mbunge wa Kigoma Kusini na mwishoni mwa wiki hii, naenda huko kwa ziara ya kikazi," alisema Kafulila jana alipokuwa akizungumza na gazeti hili.
Kafulila alisema licha ya uamuzi wa Halmashauri Kuu (NEC) ya NCCR-Mageuzi kumfukuza uanachama, kuna michakato mingi inayoendelea ndani ya chama hicho kuhusu suala hilo.
"Nisingependa kueleza ni michakato gani, lakini ieleweke tu kwamba utekelezaji wa hatua ya kunifukuza ni mchakato usioweza kunifanya nikome sasa kuwatumikia wananchi wake," alisema.
Aliendelea, “bado naendelea na kazi kama Mbunge wa Kigoma Kusini, naomba wananchi watambue hilo.”
Ruhuza amjibu Tendwa
Hata hivyo, Ruhuza akizungumzia ushauri wa Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini kutaka suluhu ya jambo hilo, alisema "Tendwa, ni mtu wa kupenda kukurupuka katika kauli zake."
“Kwanza, siamini iwapo haya maneno yametoka kwenye mdomo wa Tendwa, ila kama ni kweli inatoka mdomoni mwake, basi yeye amekurupuka na mtu anayependa kutoa matamko sawa na mtu aliyetoka usingizini,” alisema Ruhuza.
Alisema ikiwa Tendwa anadai kwamba ofisi yake haikupata mwaliko wa kuhudhuria kikao cha kumng’oa Kafulila, wakati akielewa kilichofanya hivyo ni kikao cha NEC ya chama ambacho yeye, (Tendwa) siyo mjumbe basi matamshi yake yana kasoro.
“Anazungumza kuhusu wajumbe batili, yeye amewajuaje na amewaona wapi? Orodha ya wajumbe wa NEC ipo ofisini kwake, anaelewa kabisa idadi yao na kila kitu, sasa sijui haya maneno anayapata wapi?,” alihoji Ruhuza.
Ruhuza alienda mbali zaidi na kumuita Tendwa kuwa ni mchochezi wa migogoro ndani ya vyama vya siasa akidai kuwa, licha ya kusikia viongozi wa chama hicho wakitukanwa kwa muda mrefu, hakuwahi kuchukua hatua yoyote.
“Halafu leo anasema tutumie busara, kuna wakati alisema tulipata usajili bila kukaguliwa ikabidi tumpeleke mahakamani, akatuomba msamaha. Huyu anakurupuka usingizini anatoa matamko,” alisema Ruhuza.
Ruhuza alimshauri Tendwa kabla ya kuzungumzia suala hilo, asome Katiba ya NCCR – Mageuzi ili kubaini hatua zinazopaswa kuchukuliwa dhidi ya makosa yaliyofanywa na Kafulila.
Mbunge CCM
Mbunge wa Viti Maalum CCM, Sara Msafiri, alisema suala la Kafulila linapaswa kupewa uzito na si kwa mtizamo wa kisiasa pekee.“Utaratibu wa watu 30 kutofautiana na wananchi wa jimbo zima siyo jambo la kufurahia, hili jambo linahitaji busara zaidi,” alisema Msafiri.
Msafiri alisema kitendo cha NCCR-Mageuzi kumteua Hashim Rungwe agombee urais halafu baada ya muda mfupi kumwona hafai hata kuwa mwanachama, kinaonyesha udhaifu mkubwa kwa chama hicho.
“Mtu mliyemsimamisha kugombea urais hata mwaka haujaisha, mnamwona hafai tena hata kuwa mwanachama. Hii ni aibu na wananchi wanatakiwa kuwa macho na vyama kama hivi,” alisema Msafiri.
Hata hivyo, Ruhuza alijibu hoja hiyo akisema, “Leo unaweza kuwa na mtoto mzuri sana ,lakini kesho akawa mbaya mno. Kwa hiyo hata sisi mtu akibadilika kinachotakiwa ni kumchukulia hatua.”
Mwishoni mwa wiki iliyopita, wajumbe 38 wa NEC ya NCCR-Mageuzi waliamua kumvua uanachama Kafulila kwa tuhuma za kuongea mambo ya chama nje ya utaratibu wa vikao vya chama.Kafulila mbali ya tuhuma hizo pia alituhumiwa kutaka kufanya mapinduzi ya kumg’oa madarakani mwenyekiti wa chama hicho, James Mbatia.
Hata hivyo, uamuzi huo wa kumvua uanachama umepata upinzani mkali kutoka kwa wasomi na wanasiasa mbalimbali ambao wamenukuliwa wakisema kuwa NCCR- Mageuzi walikurupuka na inafifisha demokrasia ndani ya chama.
![]() |
| Wafanyakazi wa Wizara ya Nishati na madini wakilisukuma gari la Katibu Mkuu wa wizara hiyo David Jairo wakati alipotakiwa kurudi kaziri na Katibu mkuu kiongozi Philemon Luhanjo. |
*Wanasheria: Wabunge walikosea njia kuandaa taarifa ya kamati
SIKU 15 baada ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuazimia serikali kuwachukulia hatua za kinidhamu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Bw. David Jairo,
Katibu Mkuu Kiongozi Bw. Philemon Luhanjo huku Mkaguzi na Mdhibiti na Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Bw. Ludovick Utoh, pia akituhumiwa kwa kushindwa kufanya kazi yake, hatma ya viongozi hao sasa ipo mkononi mwa Waziri Mkuu Mizengo pinda.
Bw. Jairo anadaiwa kuchangisha fedha kinyume cha sheria kwa ajili ya kuwezesha kupitishwa kwa bajeti ya wizara hiyo kinyume cha taratibu huku Bw. Luhanjo akidaiwa kumkingia kifua kiongozi huyo kwa kutoa hukumu bila kuhusisha Bunge lililoibua suala hilo.
Bw. Utoh anadaiwa na bunge kushindwa kazi yake kwa kutoa taarifa inayodaiwa kumsafisha Bw. Jairo kinyume na hali halisi.
Vyanzo vya habari ndani ya serikali vilieleza Majira kuwa tayari Ofisi ya Bunge imewasilisha taarifa za azimio la Bunge serikalini kwa Waziri Mkuu kama msimamizi wa shughuli za serikali ndani ya bunge na mtekelezaji wa shughuli za kila siku za serikali.
"Hivi sasa hatma ya akina Jairo na Luhanjo pamoja na Ngelenja zipo mkononi mwa Pinda, tayari amepewa taarifa ya azimio la Bunge tangu wiki iliyopita, "kilisema chanzo chetu ndani ya serikali.
Akizungumza na Majira Katibu wa Bunge Dkt. Thomas Kashililla, alikiri Ofisi ya Bunge kuwasilisha taarifa hiyo serikalini na kuongeza kuwa kwa kawaida huchukua muda wa saa 72 tu kuwasilisha Azimio la Bunge serikalini kama hakuna tatizo lolote.
"Ni kweli ofisi ya bunge imewasilisha taarifa ya azimio la bunge serikalini, kwa kawaida sisi tunawasilisha taarifa kama hiyo ofisi ya Mheshimiwa Waziri Mkuu ambaye ndiye Mkuu wa shughuli za serikali ndani ya Bunge," alisema Dkt. Kashililla na kuongeza.
Kwa kawaida tunachukua saa 72 tu kuwalisilisha azimio la bunge serikalini baada ya bunge kuahirishwa, sisi kama bunge tumemaliza kazi yetu labda tusubiri tu maamuzi ya serikali," alisema.
Majira lilipofika ofisi ya Waziri Mkuu kuomba ufafanuzi wa suala hilo lilijibiwa kuwa Bw. Pinda yupo katika ziara za kikazi nje ya Mkoa.
Majira ilipofika ofisi ya Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge Bw. William Lukuvi, ambaye kwa kawaida hupokea ripoti hizo kabla ya kumfikia Waziri Mkuu naye hakuwepo ofisini.
"Mheshimiwa Waziri hayupo tangu wiki iliyopita, alikuwa kwenye maadhimisho ya siku ya UKIMWI, hajafika ofisini bado, huenda atafika kesho (leo), yeye ndiye anaweza kusema lolote juu ya suala hilo, vuta subira," alisema mmoja wa wasaidizi wa waziri huyo.
Hata hivyo baadhi ya wanasheria waliozungumza na Majira kuhusu suala hilo walidai kuwa baada ya kupitia taarifa ya Bunge walibaini kuwa chombo hicho kilikosea baadhi ya vipengele vya taarifa ya Kamati Teule iliyochunguza suala hilo hivyo kuonesha wasiwasi iwapo serikali itachukulia hatua stahili kama ilivyoshauriwa dhidi ya wahusika.
Awali akiwasilisha taarifa ya uchunguzi juu ya sakata hilo la kuchangisha fedha kinyume na taratibu, aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati Teule ya Bunge Mbunge wa Tunduru Kaskazini, Bw. Ramo Makani (CCM) alisema kutokana na utaratibu huo ni vyema Bunge likaendelea kukemea kwa nguvu zote utaratibu wa uchangishaji wa fedha uliofanywa na wizara hiyo.
"Kamati teule inapendekeza kwamba serikali ichukue hatua za kinidhamu kwa ndugu David Kitundu Jairo, kwa matumizi mabaya ya madaraka, kukusanya na kutumia fedha za serikali kinyume cha sheria, kanuni na taratibu za umma na kuruhusu matumizi mabaya ya fedha za umma," alisema.
Mbali na hatua hizo kwa Bw. Jairo pia kamati hiyo imependekeza watumishi wote wa wizara hiyo ambao waliainishwa katika taarifa yao wachukuliwe hatua za kisheria.
"Aidha, kwa kuwa waziri kwa mujibu wa mwongozo wa Baraza la Mawaziri ndiye msimamizi mkuu wa wizara, hivyo suala la uchangishaji halikupaswa kufanyika bila yeye kufahamu, kamati Teule inapendekeza serikali ichukue hatua zinazofaa kwa Waziri wa Nishati na Madini, mheshimiwa William Ngeleja ambaye ni mbunge," alisema Bw. Makani.
Alisema kamati yake ilisitisha na jinsi Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG),Bw. Ludovick Utoh kwa kushindwa kutekeleza wajibu wake kikamilifu.
"Hususan katika kulisaidia Bunge na umma kwa ujumla, Kamati teule inapendekeza serikali ichukue hatua zinazofaa kwa CAG kwa upotoshaji huo," alisema Bw. Makani.
Katika hatua nyingine kamati hiyo ilipendekeza Katibu Mkuu Kiongozi, Bw. Phileom Luhanjo achukuliwe hatua zinazofaa na serikali.
"Katibu Mkuu kiongozi kwa makusudi aliamua kumsafisha ndugu David Kitundu Jairo kwa kufisha ukweli wa taarifa ya ukaguzi maalumu uliofanywa na mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali na kuamua kwamba ndugu Kitundu Jairo hakuwa na kosa la kinidhamu,kitendo ambacho kimeupotosha umma na Bunge," alisema Bw. Makani.
YASUSIA MCHAKATO WA KATIBA ALIOSAINI JK, CUF NAO WAALIKWA IKULU
CHAMA Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema kuwa kitendo cha Rais Jakaya Kikwete kusaini Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Katiba ya mwaka 2011, kimekiuka makubaliano yao, hivyo kimeamua kususia mchakato mzima wa kuratibu maoni kwa ajili ya kupata Katiba Mpya kwa kutumia sheria hiyo.Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa hatua hiyo imefikiwa ili kuonyesha kutoridhishwa na namna kiongozi huyo wa nchi, alivyowachezea akili.
"Kitendo cha Rais Kikwete kuusaini muswada huo bila ya kuupitia ni kinyume na makubaliano, jambo ambalo linatufanya tususie mchakato mzima wa kuuratibu maoni ya kwa ajili ya Katiba Mpya kupitia sheria ailiyoisaini,"alisema Mnyika na kuendelea:
“Tumeamua kujitoa kwenye mchakato mzima wa kuratibu Marekebisho ya Muswada wa Sheria ya Katiba kutokana na Rais kukiuka makubaliano yetu Ikulu yaliyomtaka aupitie kwanza kabla ya kuusaini.” Mnyika aliendelea kueleza kuwa Chadema iliwasilisha waraka wa mapendekezo sita kwa Rais ikiwa ni pamoja na kumtaka asiusaini muswada huo kutokana na wananchi kutoshirikishwa ipasavyo kwenye mchakato wa ukusanyaji wa maoni.
Alisema mapendekezo mengine ni uundaji wa tume huru, upatikanaji wa uwakilishi kutoka pande zote mbili za Muungano; Zanzibar na Bara ili kutoa fursa ya kupata maoni yao katika marekebisho hayo. "Suala la tatu ni uundaji wa Bunge la Katiba na kupunguza mamlaka ya Rais na jambo la nne ni nafasi ya Zanzibar katika Muungano pamoja na mfumo mzima wa uwakilishi wa pamoja katika muundo wa Bunge la Katiba."
Mnyika alisema kutokana na hali hiyo iliyojitokeza ya Rais kutowasikiliza, watawasilisha waraka huo waliompa, kwa wananchi ili nao wausome na kutoa maoni yao.
Alisema katika kutekeleza mkakati huo, hawatafanya maandamano yeyote, isipokuwa watatoa elimu sahihi kwa wananchi juu ya Katiba wanayopaswa kuwa nayo.
“Nia yetu ni mzuri, lengo ni kuboresha upatikanaji wa Katiba iwe bora na itakayoweza kutoa nafasi ya ushiriki wa pande zote. Lakini kinachofanyika sasa ni kinyume. Tumeamua kuwarudishia wananchi wenyewe ili waweze kuamua kama tumekosea au la,”alieleza. Tamko hilo la Chadema limekuja siku moja baada ya Rais Kikwete kutia saini muswada huo hivyo kuufanya kuwa sheria.
Rais Kikwete alitia saini muswada huo ikiwa ni siku moja baada ya yeye na viongozi wa Chadema wakiongozwa na mwenyekiti wao, Freeman Mbowe kukubaliana kwamba ipo haja ya kuendelea kuuboresha muswada ili ukidhi mahitaji ya kuaminiana na muafaka wa kitaifa. Pia, walikubaliana yawepo mawasiliano na mashauriano ya mara kwa mara kati ya Serikali na wadau mbalimbali juu ya kuboresha sheria hiyo kwa lengo la kudumisha muafaka wa kitaifa kwenye mchakato wa Katiba Mpya.
CUF nao wakubaliwa kukutana JK
Katika hatua nyingine, Chama Cha Wananchi (CUF) kimeomba kukutana na Rais Jakaya Kikwete ili kujadili Sheria ya Marekebisho ya Katiba ya Mwaka 2011, iliyotiwa saini juzi na mkuu huyo wa nchi. Taarifa ya Ikulu iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari ilieleza kuwa baada ya kupata ombi hilo, Rais Kikwete alikubali kukutana nao.
"Ofisi ya Rais, Ikulu, imepokea barua kutoka CUF kikiomba kukutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete," ilisema sehemu ya taarifa hiyo na kuongeza: " Rais amekubali ombi hilo la CUF na ameelekeza maandalizi ya mkutano huo yafanyike mara moja."
Wasomi, wanaharakati wapinga
Wakati huo huo, wasomi, wanaharakati na wanasiasa wametoa maoni tofauti kuhusu hatua ya Rais Kikwete kusaini sheria hiyo, huku Jukwaa la Katiba likieleza kuwa litafanya maandamano nchi nzima, kupinga hatua hiyo.
Mwenyekiti wa Jukwaa hilo, Deus Kibamba aliliambia Mwananchi jana kuwa hatua hiyo ya Rais, ni sawa na ‘maombolezo kwa taifa’.“Wananchi hawana uwezo wa kwenda Ikulu kuzungumza na Rais, uwezo wao ni kufanya maandamano ya amani yasiyo na ukomo nchi nzima,”alisema Kibamba anayeongoza Jukwaa hilo lenye Asasi za Kiraia zaidi ya 180.
“Serikali hii siyo sikivu, inaandaa Katiba kwa maslahi yake. Sisi tunatoa juma moja kwa polisi kukubali madai yetu ya kufanya maandamano vinginevyo uvumilivu basi,”alisema Kibamba.
Alisema kitendo cha Rais Kikwete kusaini muswada huo muda mfupi baada ya kufanya mazungumzo na Chadema ni dharau kwa chama hicho na wananchi.
Bana asema Rais ametimiza wajibu
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Dk Benson Bana alisema Rais ametimiza wajibu wake katika kusaini muswada huo kuwa sheria. Alisema kabla ya wananchi kuanza kulaumu, wanatakiwa kusubiri kwanza Rais aunde tume hiyo ndipo watoe maoni yao.
“ Duniani kote Katiba haiwezi kutosheleza mahitaji ya kila mtu, ni lazima pande fulani zitailalamikia hata kama itakuwa inafaa kwa asilimia kubwa,”alisema Dk Bana.
Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Julius Mtatiro alisema chama hicho kinasubiri kuiona Tume ya Katiba itakayoundwa na Rais. “Tunaunga mkono Rais kusaini muswada huo, tunachosubiri ni kuiona tume hiyo ikikusanya maoni ya wananchi, wakichakachua maoni ndipo tutakapoingilia kati,”alisema Mtatiro.
CHAMA Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema kuwa kitendo cha Rais Jakaya Kikwete kusaini Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Katiba ya mwaka 2011, kimekiuka makubaliano yao, hivyo kimeamua kususia mchakato mzima wa kuratibu maoni kwa ajili ya kupata Katiba Mpya kwa kutumia sheria hiyo.Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa hatua hiyo imefikiwa ili kuonyesha kutoridhishwa na namna kiongozi huyo wa nchi, alivyowachezea akili.
"Kitendo cha Rais Kikwete kuusaini muswada huo bila ya kuupitia ni kinyume na makubaliano, jambo ambalo linatufanya tususie mchakato mzima wa kuuratibu maoni ya kwa ajili ya Katiba Mpya kupitia sheria ailiyoisaini,"alisema Mnyika na kuendelea:
“Tumeamua kujitoa kwenye mchakato mzima wa kuratibu Marekebisho ya Muswada wa Sheria ya Katiba kutokana na Rais kukiuka makubaliano yetu Ikulu yaliyomtaka aupitie kwanza kabla ya kuusaini.” Mnyika aliendelea kueleza kuwa Chadema iliwasilisha waraka wa mapendekezo sita kwa Rais ikiwa ni pamoja na kumtaka asiusaini muswada huo kutokana na wananchi kutoshirikishwa ipasavyo kwenye mchakato wa ukusanyaji wa maoni.
Alisema mapendekezo mengine ni uundaji wa tume huru, upatikanaji wa uwakilishi kutoka pande zote mbili za Muungano; Zanzibar na Bara ili kutoa fursa ya kupata maoni yao katika marekebisho hayo. "Suala la tatu ni uundaji wa Bunge la Katiba na kupunguza mamlaka ya Rais na jambo la nne ni nafasi ya Zanzibar katika Muungano pamoja na mfumo mzima wa uwakilishi wa pamoja katika muundo wa Bunge la Katiba."
Mnyika alisema kutokana na hali hiyo iliyojitokeza ya Rais kutowasikiliza, watawasilisha waraka huo waliompa, kwa wananchi ili nao wausome na kutoa maoni yao.
Alisema katika kutekeleza mkakati huo, hawatafanya maandamano yeyote, isipokuwa watatoa elimu sahihi kwa wananchi juu ya Katiba wanayopaswa kuwa nayo.
“Nia yetu ni mzuri, lengo ni kuboresha upatikanaji wa Katiba iwe bora na itakayoweza kutoa nafasi ya ushiriki wa pande zote. Lakini kinachofanyika sasa ni kinyume. Tumeamua kuwarudishia wananchi wenyewe ili waweze kuamua kama tumekosea au la,”alieleza. Tamko hilo la Chadema limekuja siku moja baada ya Rais Kikwete kutia saini muswada huo hivyo kuufanya kuwa sheria.
Rais Kikwete alitia saini muswada huo ikiwa ni siku moja baada ya yeye na viongozi wa Chadema wakiongozwa na mwenyekiti wao, Freeman Mbowe kukubaliana kwamba ipo haja ya kuendelea kuuboresha muswada ili ukidhi mahitaji ya kuaminiana na muafaka wa kitaifa. Pia, walikubaliana yawepo mawasiliano na mashauriano ya mara kwa mara kati ya Serikali na wadau mbalimbali juu ya kuboresha sheria hiyo kwa lengo la kudumisha muafaka wa kitaifa kwenye mchakato wa Katiba Mpya.
CUF nao wakubaliwa kukutana JK
Katika hatua nyingine, Chama Cha Wananchi (CUF) kimeomba kukutana na Rais Jakaya Kikwete ili kujadili Sheria ya Marekebisho ya Katiba ya Mwaka 2011, iliyotiwa saini juzi na mkuu huyo wa nchi. Taarifa ya Ikulu iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari ilieleza kuwa baada ya kupata ombi hilo, Rais Kikwete alikubali kukutana nao.
"Ofisi ya Rais, Ikulu, imepokea barua kutoka CUF kikiomba kukutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete," ilisema sehemu ya taarifa hiyo na kuongeza: " Rais amekubali ombi hilo la CUF na ameelekeza maandalizi ya mkutano huo yafanyike mara moja."
Wasomi, wanaharakati wapinga
Wakati huo huo, wasomi, wanaharakati na wanasiasa wametoa maoni tofauti kuhusu hatua ya Rais Kikwete kusaini sheria hiyo, huku Jukwaa la Katiba likieleza kuwa litafanya maandamano nchi nzima, kupinga hatua hiyo.
Mwenyekiti wa Jukwaa hilo, Deus Kibamba aliliambia Mwananchi jana kuwa hatua hiyo ya Rais, ni sawa na ‘maombolezo kwa taifa’.“Wananchi hawana uwezo wa kwenda Ikulu kuzungumza na Rais, uwezo wao ni kufanya maandamano ya amani yasiyo na ukomo nchi nzima,”alisema Kibamba anayeongoza Jukwaa hilo lenye Asasi za Kiraia zaidi ya 180.
“Serikali hii siyo sikivu, inaandaa Katiba kwa maslahi yake. Sisi tunatoa juma moja kwa polisi kukubali madai yetu ya kufanya maandamano vinginevyo uvumilivu basi,”alisema Kibamba.
Alisema kitendo cha Rais Kikwete kusaini muswada huo muda mfupi baada ya kufanya mazungumzo na Chadema ni dharau kwa chama hicho na wananchi.
Bana asema Rais ametimiza wajibu
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Dk Benson Bana alisema Rais ametimiza wajibu wake katika kusaini muswada huo kuwa sheria. Alisema kabla ya wananchi kuanza kulaumu, wanatakiwa kusubiri kwanza Rais aunde tume hiyo ndipo watoe maoni yao.
“ Duniani kote Katiba haiwezi kutosheleza mahitaji ya kila mtu, ni lazima pande fulani zitailalamikia hata kama itakuwa inafaa kwa asilimia kubwa,”alisema Dk Bana.
Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Julius Mtatiro alisema chama hicho kinasubiri kuiona Tume ya Katiba itakayoundwa na Rais. “Tunaunga mkono Rais kusaini muswada huo, tunachosubiri ni kuiona tume hiyo ikikusanya maoni ya wananchi, wakichakachua maoni ndipo tutakapoingilia kati,”alisema Mtatiro.

Rais Kikwete akijadiliana na Profesa Mwesiga Baregu (kulia), Freeman Mbowe na Mh Bernard Membe wakati wa mapumziko mafupi.

Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe akijadiliana na Jambo na Rais Jakaya Kikwete(katikati)Waziri wa Mambo ya Nje Na ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe akisikiliza.

Mkutano ambao leo umedumu kwa takriban masaa matano ukiendelea.

Wajumbe upande wa Serikali.

Ujumbe wa Uongozi wa CHADEMA ukipitia kwa makini taarifa ya pamoja kati ya serikali na chama hicho kabla ya kukisambaza kwenye vyombo vya habari ikiwa ni hitimisho la mkutano wao baada ya mazungumzo ya siku mbili Ikulu jijini Dar es salaam.
Prof. Baregu akiagana na Rais Kikwete.
Gari la Mwenyekiti wa CHADEMA Mh Freeman Mbowe na lingine lililobeba wajumbe wa uongozi wa CHADEMA yakiondoka IKULU baada ya mkutano na Rais Jakaya Kikwete leo.

PICHA ZOTE NA IKULU
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimekiri kuwa mwito wa ‘kujivua gamba’ kwa viongozi wake wanaotuhumiwa kwa ufisadi haujaitikiwa kiasi cha kuridhisha na walengwa.
Kutokana na hali hiyo kimeagiza kamati za maadili na usalama katika ngazi zote nchi nzima kuwachukulia hatua haraka watuhumiwa wote.
Aidha, watuhumiwa wa ngazi ya kitafa nao mbali na kutakiwa kushughulikiwa na Kamati ya Maadili na Usalama ya Taifa inayoundwa na viongozi wakuu wa Chama na baadhi ya wajumbe wa Kamati Kuu, pia tuhuma zao zitachunguzwa.
Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama, alisema hayo jana wakati akisoma maazimio ya kikao cha siku mbili cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM kilichomalizika juzi na kuongeza kuwa watuhumiwa hao watachunguzwa na Kamati Ndogo ya Uchunguzi itakayosimamiwa na Makamu Mweyekiti wa CCM Bara, Pius Msekwa.
Mbali na Msekwa, wajumbe wengine wa Kamati hiyo itakayofanya kazi hiyo na kuwapa nafasi ya kujitetea kabla ya kuwachukulia hatua watuhumiwa hao, ni Mukama mwenyewe na wajumbe wengine wanne; wawili kutoka Zanzibar na wawili Tanzania Bara.
Mukama pia alikiri kuwapo harakati za urais wa mwaka 2015 huku akilaani viongozi wanaoacha majukumu yao ya kiserikali na kujikita katika harakati hizo.
Pia alikiri uwepo wa alichokiita saratani ya kupanga safu za viongozi katika uchaguzi na kuelezea hatua zitakazochukuliwa kukabiliana na hali hiyo.
Mukama alirejea moja ya maazimio ya NEC Aprili mwaka huu; "Kwa kutambua kuwa suala la ufisadi limekuwa mzigo mkubwa sana kwa chama licha ya juhudi kubwa ambazo Serikali imezifanya kupambana nalo, Nec ilielekeza kuwa CCM lazima ipige vita ufisadi kwa nguvu kubwa zaidi na ionekane inafanya hivyo ndani yake
yenyewe.
"Nec iliamua kuwa viongozi wa CCM wanaotuhumiwa kwa ufisadi watafakari, wajipime na kuchukua hatua wenyewe kwa maslahi ya chama. Wasipofanya hivyo, chama kiwawajibishe bila kuchelewa," alimaliza kunukuu azimio hilo la Nec.
Alisema azimio hilo lilikuwa sehemu ya mageuzi ya kukipa chama sura mpya maarufu ‘kujivua gamba’, lakini akafafanua kuwa utekelezaji wake baada ya miezi saba tangu litolewe, haujaridhisha.
"Hali ilivyo sasa, takribani miezi saba baada ya azimio hilo kupitishwa, bado hatujapata mwitikio wa kuridhisha kutoka kwa viongozi wa ngazi zote za chama chetu, ambao ni walengwa wa azimio hilo.
"Bila shaka wakati umefika kwa chama kutekeleza ile sehemu ya pili ya azimio husika kwa kuwawajibisha wahusika ... kwa kufuata utaratibu uliowekwa na kanuni za CCM za uongozi na maadili," alisema Mukama.
Alisema, mbali na Kamati Ndogo ya Uchunguzi ambayo iko chini ya Kamati Kuu ya CCM, pia Nec iliagiza kamati za maadili na usalama nchi nzima, kuwachukulia hatua viongozi wanaotuhumiwa kwa haki na kuwapa fursa ya kujitetea na kupeleka taarifa kwa mamlaka za uteuzi za viongozi hao.
Mukama alifafanua, kuwa wako watakaochukuliwa hatua na mamlaka za wilaya, za mkoa na Taifa na hilo litatekelezwa wa kuzingatia Mamlaka iliyomteua au kumwidhinisha kiongozi husika.
Katibu Mkuu aliyefuatana na Msekwa na Katibu wa Nec, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, alifafanua kuwa hali ya siasa ndani ya chama hicho ni shwari, lakini si shwari sana.
Alisema chama kinakiri kuwapo harakati za viongozi wake kugombea urais mwaka 2015 na kuongeza kuwa hazina madhara kwa chama huku akinukuu kauli za kiongozi wa China, Mao Dze Dung kuwa waache mawazo na fikra 100 zishindane na fikra pevu
zitajidhihirisha, jambo lililoonesha kuwa harakati hizo zimeruhusiwa.
Hata hivyo, alionya kuwa harakati hizo zinatakiwa kufuata utaratibu, kuepuka kugawa wanachama katika makundi na kuepuka kuchafuana, kama njia ya kujitangaza, huku akilaani viongozi walioweka pembeni majukumu ya kiserikali na kujikita katika harakati za kutafuta urais.
Pia alikiri kuwapo alichokiita saratani ya kupanga safu ya viongozi huku akionesha kuwa inaweza kutokea katika uchaguzi wa ndani ya chama mwakani.
Alisema ili kuepuka harakati za urais zisilete madhara na kumaliza saratani ya kupanga safu, CCM inajipanga kuwa wazi katika uchaguzi wa ndani wa mwakani ili kipate viongozi watakaohaghaika na wavuja jasho.
Mbali na uongozi katika chama, Mukama alisema pia CCM inatafuta utaratibu mzuri wa kumpata mgombea urais usiotegemea makundi na fedha na kuongeza kuwa mgombea atapimwa kwa msimamo wake katika itikadi ya chama hicho na hoja zake za kupambana na umasikini wa Watanzania.
Kwa mujibu wa Mukama, ajenda ya mageuzi imepokewa vyema hasa na viongozi kwa kuwa kabla ya kuanzisha kwa ajenda hiyo, viongozi wa CCM walifikia mahali wakawa kama kuku kwenye tenga ambao wakifunguliwa watoke, hubakia wamezubaa.
Hata hivyo, alisisitiza umuhimu wa mageuzi hayo kufanyika kwa utaratibu, ili kuzuia mpasuko huku akionekana kutofautiana na falsafa ya Nape ya kuoga kwa kuanzia kichwani kwenda mwili mzima, kwa kusema kuwa watu wanaoishi kando ya ziwa, huanza kujaribu maji kwa mguu na kuingia kuanzia chini kwenda juu.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Martine Shigella, amekana taarifa za kuwapo mkakati wa kuasi ndani ya chama hicho, huku akikiri kuwa taarifa hizo za uasi 'zimechangia' wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya chama hicho kuzingatia maslahi ya chama.
Akizungumza jana muda mfupi baada ya Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama kutoa taarifa ya maazimio ya kikao cha Nec kilichomalizika juzi, Shigella alisema hata taarifa za uasi hazikutolewa na kiongozi wa umoja huo na kwamba kwa kuwa jumuiya hiyo ni ya CCM haiwezi kuasi chama.
Alipotakiwa kueleza sababu za wenyeviti wa umoja huo kutoka mikoa 17 nchini na makatibu wao kupiga kambi Dodoma wakati wa kikao cha Nec, alisema hana taarifa ya ujio wa viongozi hao, wala sehemu waliyosaini ingawa gazeti hili lilishuhudia wakiletwa na mabasi yenye bendera za chama hicho.
Hata hivyo, pamoja na kukana kuwapo kwa viongozi hao, Shigella pia alikiri kuwaona baadhi na kuongeza kwamba walikuja kusikiliza yanayoendelea katika vikao hivyo kwa karibu.
Shigella pia alimpongeza Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, kwa kuongoza vema vikao vya Kamati Kuu na Nec, kwa maelezo kuwa watu walichotarajia hakikutokea, lakini bila kufafanua.
Kutokana na hali hiyo kimeagiza kamati za maadili na usalama katika ngazi zote nchi nzima kuwachukulia hatua haraka watuhumiwa wote.
Aidha, watuhumiwa wa ngazi ya kitafa nao mbali na kutakiwa kushughulikiwa na Kamati ya Maadili na Usalama ya Taifa inayoundwa na viongozi wakuu wa Chama na baadhi ya wajumbe wa Kamati Kuu, pia tuhuma zao zitachunguzwa.
Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama, alisema hayo jana wakati akisoma maazimio ya kikao cha siku mbili cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM kilichomalizika juzi na kuongeza kuwa watuhumiwa hao watachunguzwa na Kamati Ndogo ya Uchunguzi itakayosimamiwa na Makamu Mweyekiti wa CCM Bara, Pius Msekwa.
Mbali na Msekwa, wajumbe wengine wa Kamati hiyo itakayofanya kazi hiyo na kuwapa nafasi ya kujitetea kabla ya kuwachukulia hatua watuhumiwa hao, ni Mukama mwenyewe na wajumbe wengine wanne; wawili kutoka Zanzibar na wawili Tanzania Bara.
Mukama pia alikiri kuwapo harakati za urais wa mwaka 2015 huku akilaani viongozi wanaoacha majukumu yao ya kiserikali na kujikita katika harakati hizo.
Pia alikiri uwepo wa alichokiita saratani ya kupanga safu za viongozi katika uchaguzi na kuelezea hatua zitakazochukuliwa kukabiliana na hali hiyo.
Mukama alirejea moja ya maazimio ya NEC Aprili mwaka huu; "Kwa kutambua kuwa suala la ufisadi limekuwa mzigo mkubwa sana kwa chama licha ya juhudi kubwa ambazo Serikali imezifanya kupambana nalo, Nec ilielekeza kuwa CCM lazima ipige vita ufisadi kwa nguvu kubwa zaidi na ionekane inafanya hivyo ndani yake
yenyewe.
"Nec iliamua kuwa viongozi wa CCM wanaotuhumiwa kwa ufisadi watafakari, wajipime na kuchukua hatua wenyewe kwa maslahi ya chama. Wasipofanya hivyo, chama kiwawajibishe bila kuchelewa," alimaliza kunukuu azimio hilo la Nec.
Alisema azimio hilo lilikuwa sehemu ya mageuzi ya kukipa chama sura mpya maarufu ‘kujivua gamba’, lakini akafafanua kuwa utekelezaji wake baada ya miezi saba tangu litolewe, haujaridhisha.
"Hali ilivyo sasa, takribani miezi saba baada ya azimio hilo kupitishwa, bado hatujapata mwitikio wa kuridhisha kutoka kwa viongozi wa ngazi zote za chama chetu, ambao ni walengwa wa azimio hilo.
"Bila shaka wakati umefika kwa chama kutekeleza ile sehemu ya pili ya azimio husika kwa kuwawajibisha wahusika ... kwa kufuata utaratibu uliowekwa na kanuni za CCM za uongozi na maadili," alisema Mukama.
Alisema, mbali na Kamati Ndogo ya Uchunguzi ambayo iko chini ya Kamati Kuu ya CCM, pia Nec iliagiza kamati za maadili na usalama nchi nzima, kuwachukulia hatua viongozi wanaotuhumiwa kwa haki na kuwapa fursa ya kujitetea na kupeleka taarifa kwa mamlaka za uteuzi za viongozi hao.
Mukama alifafanua, kuwa wako watakaochukuliwa hatua na mamlaka za wilaya, za mkoa na Taifa na hilo litatekelezwa wa kuzingatia Mamlaka iliyomteua au kumwidhinisha kiongozi husika.
Katibu Mkuu aliyefuatana na Msekwa na Katibu wa Nec, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, alifafanua kuwa hali ya siasa ndani ya chama hicho ni shwari, lakini si shwari sana.
Alisema chama kinakiri kuwapo harakati za viongozi wake kugombea urais mwaka 2015 na kuongeza kuwa hazina madhara kwa chama huku akinukuu kauli za kiongozi wa China, Mao Dze Dung kuwa waache mawazo na fikra 100 zishindane na fikra pevu
zitajidhihirisha, jambo lililoonesha kuwa harakati hizo zimeruhusiwa.
Hata hivyo, alionya kuwa harakati hizo zinatakiwa kufuata utaratibu, kuepuka kugawa wanachama katika makundi na kuepuka kuchafuana, kama njia ya kujitangaza, huku akilaani viongozi walioweka pembeni majukumu ya kiserikali na kujikita katika harakati za kutafuta urais.
Pia alikiri kuwapo alichokiita saratani ya kupanga safu ya viongozi huku akionesha kuwa inaweza kutokea katika uchaguzi wa ndani ya chama mwakani.
Alisema ili kuepuka harakati za urais zisilete madhara na kumaliza saratani ya kupanga safu, CCM inajipanga kuwa wazi katika uchaguzi wa ndani wa mwakani ili kipate viongozi watakaohaghaika na wavuja jasho.
Mbali na uongozi katika chama, Mukama alisema pia CCM inatafuta utaratibu mzuri wa kumpata mgombea urais usiotegemea makundi na fedha na kuongeza kuwa mgombea atapimwa kwa msimamo wake katika itikadi ya chama hicho na hoja zake za kupambana na umasikini wa Watanzania.
Kwa mujibu wa Mukama, ajenda ya mageuzi imepokewa vyema hasa na viongozi kwa kuwa kabla ya kuanzisha kwa ajenda hiyo, viongozi wa CCM walifikia mahali wakawa kama kuku kwenye tenga ambao wakifunguliwa watoke, hubakia wamezubaa.
Hata hivyo, alisisitiza umuhimu wa mageuzi hayo kufanyika kwa utaratibu, ili kuzuia mpasuko huku akionekana kutofautiana na falsafa ya Nape ya kuoga kwa kuanzia kichwani kwenda mwili mzima, kwa kusema kuwa watu wanaoishi kando ya ziwa, huanza kujaribu maji kwa mguu na kuingia kuanzia chini kwenda juu.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Martine Shigella, amekana taarifa za kuwapo mkakati wa kuasi ndani ya chama hicho, huku akikiri kuwa taarifa hizo za uasi 'zimechangia' wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya chama hicho kuzingatia maslahi ya chama.
Akizungumza jana muda mfupi baada ya Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama kutoa taarifa ya maazimio ya kikao cha Nec kilichomalizika juzi, Shigella alisema hata taarifa za uasi hazikutolewa na kiongozi wa umoja huo na kwamba kwa kuwa jumuiya hiyo ni ya CCM haiwezi kuasi chama.
Alipotakiwa kueleza sababu za wenyeviti wa umoja huo kutoka mikoa 17 nchini na makatibu wao kupiga kambi Dodoma wakati wa kikao cha Nec, alisema hana taarifa ya ujio wa viongozi hao, wala sehemu waliyosaini ingawa gazeti hili lilishuhudia wakiletwa na mabasi yenye bendera za chama hicho.
Hata hivyo, pamoja na kukana kuwapo kwa viongozi hao, Shigella pia alikiri kuwaona baadhi na kuongeza kwamba walikuja kusikiliza yanayoendelea katika vikao hivyo kwa karibu.
Shigella pia alimpongeza Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, kwa kuongoza vema vikao vya Kamati Kuu na Nec, kwa maelezo kuwa watu walichotarajia hakikutokea, lakini bila kufafanua.
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimemvua uongozi Katibu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Kilumbe
Ng'enda kwa kosa la kwenda kinyume na uamuzi halali wa vikao vya Chama wakati wa uchaguzi
wa madiwani wa viti maalumu wa mkoa huo.
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Nape Nnauye alisema jana kuwa kikao cha NEC kilichokuwa kikifanyika kwa siku ya pili jana, ndicho kilichotoa uamuzi huo na Ng'enda atapangiwa kazi nyingine.
Mbali na kuvuliwa uongozi kwa Ng'enda, Nape alisema pia NEC imepanga ratiba ya ndani ya kumpata mgombea wa CCM ya Mwakilishi wa Uzini baada ya Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) kutangaza ratiba ya uchaguzi mdogo wa jimbo hilo.
Kwa mujibu wa ratiba hiyo inayohusisha pia vikao vya chama hicho, wanachama wa CCM wataanza kuchukua na kurejesha fomu kuanzia Novemba 28 mpaka Desemba 2.
Kuanzia Desemba 3 mpaka 10, kutafanyika kampeni za wagombea wa chama hicho katika ngazi ya matawi.
Ratiba hiyo imeonesha kuwa siku ya kupiga kura kumchagua mgombea wa CCM ni Desemba 11 na baada ya hapo Kamati ya Usalama na Maadili itakaa Desemba 13.
Baada ya Kamati hiyo, itafuatiwa na kikao cha Kamati ya Siasa ya Wilaya Desemba 14, Kamati ya Siasa ya Mkoa Desemba 17, Sekretarieti ya Kamati Maalumu ya NEC Desemba 20 mwaka huu na kufuatiwa na Kamati Maalumu ya NEC, Desemba 24.
Sekretarieti ya NEC itakutana Januari 4 na 5 na Kamati Kuu ya CCM kumthibitisha mgombea huyo itakaa Januari 7 na 8.
Wachunguzi wa masuala ya siasa ndani ya CCM wanabaini kuwa uamuzi huo umejikita zaidi katika sintofahamu iliyotokea Dar es Salaam kuhusiana na uchaguzi wa wabunge wa madiwani wa viti maalumu na kuzusha lawama kutoka kwa Mbunge wa Kinondoni, Iddi Azzan dhidi ya
Ng’enda.
Mgogoro huo ulifikia Azzan kupewa adhabu ya kufungiwa kugombea nafasi yoyote katika chama hicho na kujihusisha kwa namna moja ama nyingine katika masuala ya uongozi.
Hata hivyo baadhi ya wanachama wa CCM wa wilaya za Mkoa wa Dar es Salaam walijitosa katika sakata hilo wakiitaka Kamati Kuu ya CCM Taifa (CC), kuingilia kati na kutengua adhabu dhidi ya Azzan.
Wanachama hao pia walimtaka Ng’enda na sekretarieti ya siasa ya mkoa huo kuwajibika kutokana na matokeo mabaya ya uchaguzi mkuu wa mwaka jana.
Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Ilala, Jumanne Kolekole, alikaririwa wakati mmoja akisema mazingira ya uendeshaji wa shughuli za CCM Dar es Salaam, yanawafanya baadhi ya wana-CCM kujiona kama wanatengwa kutokana na kushindwa kwa viongozi wa mkoa na hasa Katibu wake, kuwashirikisha katika uamuzi wenye maslahi.
“Viongozi wa Mkoa wa Dar es Salaam, wamekuwa wabinafsi na wenye kuona nafasi zao ni kama mamlaka isiyohitaji kuhojiwa na mtu au mwanachama mwingine yeyote na ndiyo maana hata wakishauriwa jambo wanakuwa wakali na kuchukua hatua zikionesha chuki,” alipata kusema
Kolekole.
“Mimi nadhani CCM Mkoa wa Dar es Salaam hauna viongozi wazuri, hawa akina Kilumbe na John Guninita (Mwenyekiti wa Mkoa) ni aina ya watu walioshindwa kazi na ambao kinachowafanya kuendelea na uongozi ni siasa za mazoea, na huyu ni mwenzetu na wala hawana sifa za uongozi,” alisema mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Mangundala.
Alisema wanaCCM Wilaya ya Ilala wanaunga mkono kauli ya Mbunge Azzan ya kutaka viongozi wa mkoa na kwa kuanzia katika sekretarieti ya mkoa kuwajibika na kujivua gamba.
Wilayani Temeke, wana-CCM wa kata za Yombo Makangarawe, Keko, Temeke, Kurasini alisema kilichofanywa na Kamati ya Kilumbe kilitokana na hasira ya kuelezwa ukweli ambao viongozi wengi hawataki kuusikia.
Hata hivyo, Kilumbe na Guninita walikaririwa wakijibu kwa kusema wanakiachia chama kuchukua uamuzi na ikiwa itabainika wamekosea kuchukua hatua watalazimika kuwajibika.
Wakati huo huo, Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete leo atafungua semina ya watendaji wa chama hicho wa ngazi ya Taifa hadi wilaya yenye lengo la kufanikisha utendaji wa ndani ya chama.
Nape alisema semina hiyo itafanyika kwa siku tatu mpaka keshokutwa na itashirikisha wajumbe wa Sekretarieti ya NEC na Sekretarieti ya jumuiya za CCM na makatibu wa CCM wa mikoa na wilaya zote nchini.
Wakati huo huo, Nape amesema taarifa rasmi kuhusiana na maamuzi mengine ya kikao hicho ambayo yanasubiriwa kwa hamu na Watanzania yatatolewa leo.
Ng'enda kwa kosa la kwenda kinyume na uamuzi halali wa vikao vya Chama wakati wa uchaguzi
wa madiwani wa viti maalumu wa mkoa huo.
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Nape Nnauye alisema jana kuwa kikao cha NEC kilichokuwa kikifanyika kwa siku ya pili jana, ndicho kilichotoa uamuzi huo na Ng'enda atapangiwa kazi nyingine.
Mbali na kuvuliwa uongozi kwa Ng'enda, Nape alisema pia NEC imepanga ratiba ya ndani ya kumpata mgombea wa CCM ya Mwakilishi wa Uzini baada ya Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) kutangaza ratiba ya uchaguzi mdogo wa jimbo hilo.
Kwa mujibu wa ratiba hiyo inayohusisha pia vikao vya chama hicho, wanachama wa CCM wataanza kuchukua na kurejesha fomu kuanzia Novemba 28 mpaka Desemba 2.
Kuanzia Desemba 3 mpaka 10, kutafanyika kampeni za wagombea wa chama hicho katika ngazi ya matawi.
Ratiba hiyo imeonesha kuwa siku ya kupiga kura kumchagua mgombea wa CCM ni Desemba 11 na baada ya hapo Kamati ya Usalama na Maadili itakaa Desemba 13.
Baada ya Kamati hiyo, itafuatiwa na kikao cha Kamati ya Siasa ya Wilaya Desemba 14, Kamati ya Siasa ya Mkoa Desemba 17, Sekretarieti ya Kamati Maalumu ya NEC Desemba 20 mwaka huu na kufuatiwa na Kamati Maalumu ya NEC, Desemba 24.
Sekretarieti ya NEC itakutana Januari 4 na 5 na Kamati Kuu ya CCM kumthibitisha mgombea huyo itakaa Januari 7 na 8.
Wachunguzi wa masuala ya siasa ndani ya CCM wanabaini kuwa uamuzi huo umejikita zaidi katika sintofahamu iliyotokea Dar es Salaam kuhusiana na uchaguzi wa wabunge wa madiwani wa viti maalumu na kuzusha lawama kutoka kwa Mbunge wa Kinondoni, Iddi Azzan dhidi ya
Ng’enda.
Mgogoro huo ulifikia Azzan kupewa adhabu ya kufungiwa kugombea nafasi yoyote katika chama hicho na kujihusisha kwa namna moja ama nyingine katika masuala ya uongozi.
Hata hivyo baadhi ya wanachama wa CCM wa wilaya za Mkoa wa Dar es Salaam walijitosa katika sakata hilo wakiitaka Kamati Kuu ya CCM Taifa (CC), kuingilia kati na kutengua adhabu dhidi ya Azzan.
Wanachama hao pia walimtaka Ng’enda na sekretarieti ya siasa ya mkoa huo kuwajibika kutokana na matokeo mabaya ya uchaguzi mkuu wa mwaka jana.
Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Ilala, Jumanne Kolekole, alikaririwa wakati mmoja akisema mazingira ya uendeshaji wa shughuli za CCM Dar es Salaam, yanawafanya baadhi ya wana-CCM kujiona kama wanatengwa kutokana na kushindwa kwa viongozi wa mkoa na hasa Katibu wake, kuwashirikisha katika uamuzi wenye maslahi.
“Viongozi wa Mkoa wa Dar es Salaam, wamekuwa wabinafsi na wenye kuona nafasi zao ni kama mamlaka isiyohitaji kuhojiwa na mtu au mwanachama mwingine yeyote na ndiyo maana hata wakishauriwa jambo wanakuwa wakali na kuchukua hatua zikionesha chuki,” alipata kusema
Kolekole.
“Mimi nadhani CCM Mkoa wa Dar es Salaam hauna viongozi wazuri, hawa akina Kilumbe na John Guninita (Mwenyekiti wa Mkoa) ni aina ya watu walioshindwa kazi na ambao kinachowafanya kuendelea na uongozi ni siasa za mazoea, na huyu ni mwenzetu na wala hawana sifa za uongozi,” alisema mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Mangundala.
Alisema wanaCCM Wilaya ya Ilala wanaunga mkono kauli ya Mbunge Azzan ya kutaka viongozi wa mkoa na kwa kuanzia katika sekretarieti ya mkoa kuwajibika na kujivua gamba.
Wilayani Temeke, wana-CCM wa kata za Yombo Makangarawe, Keko, Temeke, Kurasini alisema kilichofanywa na Kamati ya Kilumbe kilitokana na hasira ya kuelezwa ukweli ambao viongozi wengi hawataki kuusikia.
Hata hivyo, Kilumbe na Guninita walikaririwa wakijibu kwa kusema wanakiachia chama kuchukua uamuzi na ikiwa itabainika wamekosea kuchukua hatua watalazimika kuwajibika.
Wakati huo huo, Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete leo atafungua semina ya watendaji wa chama hicho wa ngazi ya Taifa hadi wilaya yenye lengo la kufanikisha utendaji wa ndani ya chama.
Nape alisema semina hiyo itafanyika kwa siku tatu mpaka keshokutwa na itashirikisha wajumbe wa Sekretarieti ya NEC na Sekretarieti ya jumuiya za CCM na makatibu wa CCM wa mikoa na wilaya zote nchini.
Wakati huo huo, Nape amesema taarifa rasmi kuhusiana na maamuzi mengine ya kikao hicho ambayo yanasubiriwa kwa hamu na Watanzania yatatolewa leo.
WALIA KUCHAFULIWA NA MAKADA WENZAO,NEC YARIDHIA GAMBA KUREJESHWA CC
MAWAZIRI Wakuu wa zamani, Edward Lowassa na Frederick Sumaye, jana walishambulia kwa maneno makali wajumbe wawili wa Sekretarieti ya CCM kwamba wamekuwa wakikivuruga chama na kusababisha mgawanyiko uliopo.Lowassa aliyejiuzulu Uwaziri Mkuu, kutokana na kashfa ya Richmond ndiye aliyekuwa wa kwanza kuzungumzia suala hilo wakati wa mjadala wa hali ya siasa, katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) kilichomazika jana mjini Dodoma.
Habari za uhakika kutoka ndani ya kikao hicho zinasema Lowassa alianza kubwaga moyo wake baada ya NEC kuridhia ombi la Kamati Kuu ya chama hicho (CC) kwamba suala la mageuzi ndani ya CCM maarufu kama kujivua gamba lirejeshwe katika kamati hiyo ili lifanyiwe kazi kwa taratibu za kawaida za kinidhamu baada ya wahusika kukataa kuachia nafasi zao.
“Mwenyekiti kwanza napongeza uamuzi huu wa kurejesha jambo hili katika taratibu za kawaida, lakini napenda kufahamu kwa miezi saba nimetukanwa nikiitwa fisadi, watu wamezunguka nchi nzima kwa fedha za chama wakinitukana, hivi hatukujua kwamba kuna kamati hizo za maadili,”Lowassa alinukuliwa akihoji.
Lowassa alinukuliwa akiwataja Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Tanzania Bara, John Chiligati kwamba wamekuwa wakitukana watu ovyo kwa fedha wanazopewa na CCM.
Kwa mujibu wa taarifa hizo, Lowassa alitumia dakika saba kumshambulia Nape kwamba amekuwa akifanya mambo nje ya utaratibu na kwamba mwenendo huo umekuwa ukikibomoa chama badala ya kukijenga.
Baada ya maneno ya Lowassa, Waziri Mkuu mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Tatu, Sumaye alisimama na kuhoji sababu za chama hicho kunyamazia ukiukwaji wa taratibu ambao umekuwa ukifanywa na watendaji hao.
“Mwenyekiti huyu bwana (Lowassa) amesema kwamba amechafuliwa kwa miezi saba, sasa kama leo tunasema kwamba tunarudi kwenye utaratibu wa kamati za maadili, hao waliomchafua watafanywaje?”Sumaye alinukuliwa akihoji.
Hata hivyo, taarifa za ndani ya kikao hicho zilimnukuu Kikwete akisema kwamba viongozi hao watakuchukuliwa hatua za kinidhamu kama watakuwa wamefanya hivyo.
Kutokana na hali hiyo, Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete aliwasihi wajumbe kuachana na suala hilo na badala yake kuchangia maeneo mengine ya taarifa hiyo ya hali ya siasa iliyowasilishwa na Katibu wa Siasa na Mambo ya Nje ya CCM, January Makamba.
Kikwete alinukuliwa akihitimisha hoja hiyo kwa kusema kwamba: “Jamani hapa tunajenga chama, watu wanasubiri kusikia tukimaliza kikao chetu kwa ugomvi, naomba tumalize kwa amani na twendeni tukajenge chama chetu”.
Richmond yatajwa
Vyanzo vyetu vilimnukuu Lowassa akizungumzia suala la Kampuni tata ya kufua umeme ya Richmond kwamba yeye aliamua kuvunja mkataba baina ya kampuni hiyo, lakini Rais KIkwete alimwambia subiri baada ya kuwa amepata ushauri wa Makatibu Wakuu.
Lowassa ambaye ni Mbunge wa Monduli (CCM), alinukuliwa akisema: “Mwenyekiti utakumbuka kwamba mimi nilishaamua kuvunja mkataba wa Richmond mapema, lakini baada ya kukupigia simu ukiwa katika safari nje ya nchi ulisema tusubiri kwani ulikuwa umepata ushauri wa makatibu wakuu wa wizara, sasa leo hii ninahukumiwa nakuitwa fisadi kwanini?”.
“Nilijiuzulu kuwajibika kwa ajili ya kuilinda Serikali yangu na kwa heshima ya chama changu, sasa kwanini leo nahukumiwa kwa jambo hili, tena natukanwa na wana CCM wenzangu na siyo wapinzani nchi nzima kwamba mimi eti fisadi?,”alinukuliwa akihoji Lowassa.
Kadhalika kada huyo wa CCM alinukuliwa akimkumbusha Rais Kikwete kwamba: “Mwenyekiti nikukumbushe mwaka 1997 kule Zanzibar, kina Mzee Daudi Mwakawago walikuja na mafaili yakiwa na tuhuma dhidi ya mtizamo hasi wa jamii dhidi yako, kwa hiyo wakati ule kama si busara za kina Mzee Mkapa (Benjamin) leo usingekuwa hapo ulipo”.
Lowassa alisema kama alivyozungumza na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa walipokutana jijini Dar es Salaam, tatizo kubwa analolifahamu la vita ya sasa ni urais wa 2015.
“Mwenyekiti nikukumbushe jambo jingine, kule Zanzibar mwaka 1997 walipoleta tuhuma za mtizamo wa umma dhidi yako, ulisema kwamba kuwa Rais ni mipango ya Mungu,”alinukuliwa Lowassa katika maelezo yake ndani ya NEC
Alisema kwa kuzingatia mazingira hayo, hii leo si sahihi hata yeye (Lowassa) kuhukumiwa kwa kuzingatia kile kinachodaiwa kuwa ni mtizamo wa umma dhidi yake unaompa sura ya ufisadi, jambo ambalo alidai kwamba siyo la kweli.
Baada ya Lowassa na Sumaye kuongoa, kada maarufu wa chama hicho, Kingunge Ngombale Mwiru alisimama akitaka kuongelea dhana ya gamba ndipo Mkapa alipomshtua Kikwete kwamba hoja hiyo ifikie mwisho.
Baadhi ya wajumbe waliiambia Mwananchi kwamba wakati Lowassa akiongea Mkapa alionekana kufurahi.
Kujivua gamba
Kufuatia uamuzi huo wa NEC hivi sasa mpango wa kujivua gamba ulioasisiwa na chama hicho, Aprili mwaka huu unarejeshwa CC ambapo watuhumiwa wote wa makosa mbalimbali watafikishwa mbele ya Kamati za maadili na kuchukuliwa hatua kwa taratibu za chama hicho.
Mpango wa kujivua gamba ulilenga kuwashinikiza watuhumiwa wa ufisadi kuachia nafasi zao za uongozi ndani ya chama hicho na sasa unarejeshwa Kamati Kuu (CC) ili ichukue hatua zaidi kwa wale waliogoma kujiuzulu.
Hatua hiyo inatokana na kuwapo ukimya ambao unaashiria kutokuwapo viongozi na makada ambao wako tayari kujiuzulu nyadhifa zao kwa hiari yao kama ilivyotarajiwa.
Tangu kupitishwa kwa mpango huo maarufu kwa jina la kujivua gamba katika kikao cha NEC kilichopita cha Aprili mwaka huu, ni kada mmoja tu, Rostam Aziz aliyechukua hatua za kujiuzulu ubunge wa Jimbo la Igunga na ujumbe wa NEC, lakini wengine wamekuwa kimya hadi sasa.
Katika kikao cha Aprili NEC hiyo ya CCM ilipitisha maazimio 26, lakini kubwa ni lile lililokuwa likihimiza vita dhidi ya ufisadi kuendelea na kutoa mwito kwa watu wanaotajwa na jamii kuhusika na ufisadi ambao wako ndani ya chama kujitathmini kisha kuchukua hatua za kuachia madaraka waliyonayo.
Sehemu ya mwisho ya azimio hilo inasomeka: “Wasipoachia madaraka chama kiwachukulie hatua mara moja”.
Mmoja wa wajumbe wa CC ambaye ameomba jina lake kuhifadhiwa alisema: “Tunawaomba NEC waturuhusu jambo hili tulifanyie kazi sisi (CC) na litafanyiwa kazi kupitia taratibu za kawaida za chama kwa kuzingatia kanuni na taratibu za maadili za chama hicho”.
Nec yawakaanga kina Jairo
Katika hatua nyingine, NEC imeunga mkono hatua zilizopendekezwa na Bunge dhidi ya watumishi wa umma waliotajwa katika ripoti ya Kamati Teule ya Bunge, iliyoanika uozo wa matumizi mabaya ya fedha za Umma ndani ya Wizara ya Nishati na Madini.
Kamati hiyo katika ripoti yake iliyowasilishwa mwishoni mwa Mkutano wa Tano wa Bunge uliomalizika wiki iliyopita mjini Dodoma, iliwataja Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati na Madini (aliyesimamishwa), David Jairo na Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo kwamba wanastahili kuchukuliwa hatua.
Wengine ni Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali, Ludovick Utouh, huku wabunge wakipendekeza pia kuondolewa madarakani kwa Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Adam Malima.
MAWAZIRI Wakuu wa zamani, Edward Lowassa na Frederick Sumaye, jana walishambulia kwa maneno makali wajumbe wawili wa Sekretarieti ya CCM kwamba wamekuwa wakikivuruga chama na kusababisha mgawanyiko uliopo.Lowassa aliyejiuzulu Uwaziri Mkuu, kutokana na kashfa ya Richmond ndiye aliyekuwa wa kwanza kuzungumzia suala hilo wakati wa mjadala wa hali ya siasa, katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) kilichomazika jana mjini Dodoma.
Habari za uhakika kutoka ndani ya kikao hicho zinasema Lowassa alianza kubwaga moyo wake baada ya NEC kuridhia ombi la Kamati Kuu ya chama hicho (CC) kwamba suala la mageuzi ndani ya CCM maarufu kama kujivua gamba lirejeshwe katika kamati hiyo ili lifanyiwe kazi kwa taratibu za kawaida za kinidhamu baada ya wahusika kukataa kuachia nafasi zao.
“Mwenyekiti kwanza napongeza uamuzi huu wa kurejesha jambo hili katika taratibu za kawaida, lakini napenda kufahamu kwa miezi saba nimetukanwa nikiitwa fisadi, watu wamezunguka nchi nzima kwa fedha za chama wakinitukana, hivi hatukujua kwamba kuna kamati hizo za maadili,”Lowassa alinukuliwa akihoji.
Lowassa alinukuliwa akiwataja Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Tanzania Bara, John Chiligati kwamba wamekuwa wakitukana watu ovyo kwa fedha wanazopewa na CCM.
Kwa mujibu wa taarifa hizo, Lowassa alitumia dakika saba kumshambulia Nape kwamba amekuwa akifanya mambo nje ya utaratibu na kwamba mwenendo huo umekuwa ukikibomoa chama badala ya kukijenga.
Baada ya maneno ya Lowassa, Waziri Mkuu mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Tatu, Sumaye alisimama na kuhoji sababu za chama hicho kunyamazia ukiukwaji wa taratibu ambao umekuwa ukifanywa na watendaji hao.
“Mwenyekiti huyu bwana (Lowassa) amesema kwamba amechafuliwa kwa miezi saba, sasa kama leo tunasema kwamba tunarudi kwenye utaratibu wa kamati za maadili, hao waliomchafua watafanywaje?”Sumaye alinukuliwa akihoji.
Hata hivyo, taarifa za ndani ya kikao hicho zilimnukuu Kikwete akisema kwamba viongozi hao watakuchukuliwa hatua za kinidhamu kama watakuwa wamefanya hivyo.
Kutokana na hali hiyo, Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete aliwasihi wajumbe kuachana na suala hilo na badala yake kuchangia maeneo mengine ya taarifa hiyo ya hali ya siasa iliyowasilishwa na Katibu wa Siasa na Mambo ya Nje ya CCM, January Makamba.
Kikwete alinukuliwa akihitimisha hoja hiyo kwa kusema kwamba: “Jamani hapa tunajenga chama, watu wanasubiri kusikia tukimaliza kikao chetu kwa ugomvi, naomba tumalize kwa amani na twendeni tukajenge chama chetu”.
Richmond yatajwa
Vyanzo vyetu vilimnukuu Lowassa akizungumzia suala la Kampuni tata ya kufua umeme ya Richmond kwamba yeye aliamua kuvunja mkataba baina ya kampuni hiyo, lakini Rais KIkwete alimwambia subiri baada ya kuwa amepata ushauri wa Makatibu Wakuu.
Lowassa ambaye ni Mbunge wa Monduli (CCM), alinukuliwa akisema: “Mwenyekiti utakumbuka kwamba mimi nilishaamua kuvunja mkataba wa Richmond mapema, lakini baada ya kukupigia simu ukiwa katika safari nje ya nchi ulisema tusubiri kwani ulikuwa umepata ushauri wa makatibu wakuu wa wizara, sasa leo hii ninahukumiwa nakuitwa fisadi kwanini?”.
“Nilijiuzulu kuwajibika kwa ajili ya kuilinda Serikali yangu na kwa heshima ya chama changu, sasa kwanini leo nahukumiwa kwa jambo hili, tena natukanwa na wana CCM wenzangu na siyo wapinzani nchi nzima kwamba mimi eti fisadi?,”alinukuliwa akihoji Lowassa.
Kadhalika kada huyo wa CCM alinukuliwa akimkumbusha Rais Kikwete kwamba: “Mwenyekiti nikukumbushe mwaka 1997 kule Zanzibar, kina Mzee Daudi Mwakawago walikuja na mafaili yakiwa na tuhuma dhidi ya mtizamo hasi wa jamii dhidi yako, kwa hiyo wakati ule kama si busara za kina Mzee Mkapa (Benjamin) leo usingekuwa hapo ulipo”.
Lowassa alisema kama alivyozungumza na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa walipokutana jijini Dar es Salaam, tatizo kubwa analolifahamu la vita ya sasa ni urais wa 2015.
“Mwenyekiti nikukumbushe jambo jingine, kule Zanzibar mwaka 1997 walipoleta tuhuma za mtizamo wa umma dhidi yako, ulisema kwamba kuwa Rais ni mipango ya Mungu,”alinukuliwa Lowassa katika maelezo yake ndani ya NEC
Alisema kwa kuzingatia mazingira hayo, hii leo si sahihi hata yeye (Lowassa) kuhukumiwa kwa kuzingatia kile kinachodaiwa kuwa ni mtizamo wa umma dhidi yake unaompa sura ya ufisadi, jambo ambalo alidai kwamba siyo la kweli.
Baada ya Lowassa na Sumaye kuongoa, kada maarufu wa chama hicho, Kingunge Ngombale Mwiru alisimama akitaka kuongelea dhana ya gamba ndipo Mkapa alipomshtua Kikwete kwamba hoja hiyo ifikie mwisho.
Baadhi ya wajumbe waliiambia Mwananchi kwamba wakati Lowassa akiongea Mkapa alionekana kufurahi.
Kujivua gamba
Kufuatia uamuzi huo wa NEC hivi sasa mpango wa kujivua gamba ulioasisiwa na chama hicho, Aprili mwaka huu unarejeshwa CC ambapo watuhumiwa wote wa makosa mbalimbali watafikishwa mbele ya Kamati za maadili na kuchukuliwa hatua kwa taratibu za chama hicho.
Mpango wa kujivua gamba ulilenga kuwashinikiza watuhumiwa wa ufisadi kuachia nafasi zao za uongozi ndani ya chama hicho na sasa unarejeshwa Kamati Kuu (CC) ili ichukue hatua zaidi kwa wale waliogoma kujiuzulu.
Hatua hiyo inatokana na kuwapo ukimya ambao unaashiria kutokuwapo viongozi na makada ambao wako tayari kujiuzulu nyadhifa zao kwa hiari yao kama ilivyotarajiwa.
Tangu kupitishwa kwa mpango huo maarufu kwa jina la kujivua gamba katika kikao cha NEC kilichopita cha Aprili mwaka huu, ni kada mmoja tu, Rostam Aziz aliyechukua hatua za kujiuzulu ubunge wa Jimbo la Igunga na ujumbe wa NEC, lakini wengine wamekuwa kimya hadi sasa.
Katika kikao cha Aprili NEC hiyo ya CCM ilipitisha maazimio 26, lakini kubwa ni lile lililokuwa likihimiza vita dhidi ya ufisadi kuendelea na kutoa mwito kwa watu wanaotajwa na jamii kuhusika na ufisadi ambao wako ndani ya chama kujitathmini kisha kuchukua hatua za kuachia madaraka waliyonayo.
Sehemu ya mwisho ya azimio hilo inasomeka: “Wasipoachia madaraka chama kiwachukulie hatua mara moja”.
Mmoja wa wajumbe wa CC ambaye ameomba jina lake kuhifadhiwa alisema: “Tunawaomba NEC waturuhusu jambo hili tulifanyie kazi sisi (CC) na litafanyiwa kazi kupitia taratibu za kawaida za chama kwa kuzingatia kanuni na taratibu za maadili za chama hicho”.
Nec yawakaanga kina Jairo
Katika hatua nyingine, NEC imeunga mkono hatua zilizopendekezwa na Bunge dhidi ya watumishi wa umma waliotajwa katika ripoti ya Kamati Teule ya Bunge, iliyoanika uozo wa matumizi mabaya ya fedha za Umma ndani ya Wizara ya Nishati na Madini.
Kamati hiyo katika ripoti yake iliyowasilishwa mwishoni mwa Mkutano wa Tano wa Bunge uliomalizika wiki iliyopita mjini Dodoma, iliwataja Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati na Madini (aliyesimamishwa), David Jairo na Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo kwamba wanastahili kuchukuliwa hatua.
Wengine ni Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali, Ludovick Utouh, huku wabunge wakipendekeza pia kuondolewa madarakani kwa Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Adam Malima.










