Subscribe to receive latest Updates

Online :

You Are Here: Home - HABARI ZA KIMATAIFA - Muswada wa ndoa za jinsia moja warejeshwa bungeni Uganda

IDADI YA WATU WALIOSOMA HABARI HII: counter
Mbunge mmoja wa Uganda ameurejesha muswada wenye utata wa wapenzi wa jinsia moja, lakini kipengele cha hukumu ya kifo kimeondolewa, kwa kosa la vitendo kadhaa.
Mwandishi wa BBC amesema wabunge walicheka, kupiga makofi na kushangilia wakisema "Muswada wetu, muswada wetu," wakati mbunge huyo David Bahati alipourudisha tena bungeni siku ya Jumanne.
Muswada wa wapenzi wa jinsia moja uliwekwa kando mwaka 2011 kufuatia malalamiko kutoka jumuiya ya kimataifa.
Bado muswada huo unabeba adhabu ya kifungo cha maisha jela kwa kukutwa na hatia ya kufanya mapenzi ya jinsia moja.
Kufanya mapenzi ya jinsia moja ni kosa la kisheria nchini Uganda - katika jamii ambayo ina msimamo mkali - ambapo wengi hulaani mapenzi ya jinsia moja.
Yeyote anayemfahamu mtu anayefanya mapenzi ya jinsia moja na kukaa kimya bila kusema kwa mamlaka, pia huenda akashtakiwa.

0 comments

Post a Comment