Subscribe to receive latest Updates

Online :

You Are Here: Home - - Lebanon na Israel zafarakana, afisa wa juu wa Israel auawa katika mapambano

IDADI YA WATU WALIOSOMA HABARI HII: counter


Askari watatu wa Lebanon, afisa wa ngazi ya juu wa Israel na mwandishi wa habari wa Lebanon wameuawa katika majibizano ya risasi karibu na mpaka baina ya nchi hizo mbili.
Lebanon
Bendera ikipepea nchini Lebanon karibu na mpaka na Israel
Lebanon imedai kuwa walifyatua risasi baada ya kuona vikosi vya Israel vimeingia kwenye ardhi yao. Lakini Waisrael wamekanusha kuvuka mpaka.
Hii ni mara ya kwanza kwa mapambano makali kutokea tangu mwaka 2006 wakati wa mapambano baina ya Israel na wapiganaji wa kundi la Lebanon la Hizbullah.
Waziri mkuu wa Lebanon ameshutumu kitendo hicho cha uvamizi lakini Israel imejibu kwa kuionya kuwa itakiona cha moto ikiendelea kuleta fujo.
Lebanon
Askari wa Lebanon
Katika taarifa, Waziri Mkuu wa Lebanon Saad Hariri amesema kuwa hadhi ya taifa lake imekiukwa. Jeshi la Lebanon linasema kuwa askari wa jeshi la Israel walivuka mpaka na kuun'goa mti uliokuwa ukiwazuia kuona kijiji cha Adaysseh huko Lebanon.
Msemaji wa vikosi vya Lebanon amesema kuwa walifyatua risasi za kuwaonya askari hao na Israel ikajibu kwa kulipua makombora na kutuma helikopta.
Jeshi hilo limethibitishia BBC kuwa askari wake watatu waliuawa na wanne kujeruhiwa. Gazeti la Al Akhbar limethibitisha kifo cha mwandishi wao mmoja, Assaf Abu Rahhal.
Tags:

0 comments

Post a Comment