Subscribe to receive latest Updates

Online :

You Are Here: Home - - Timu ya wauaji 11 wa Israel inasakwa kwa kutimiza mauaji ya Kiongozi wa Hamasi huko Emirates

IDADI YA WATU WALIOSOMA HABARI HII: counter

Wapalestina hao 2 waliohujiwa wote wakaazi wa Umoja wa Falme za Kiarabu (Emirates) "walikimbilia Jordan" mara tu baada ya Bw.Mahmud al-Mabhuh, kukutikana amefariki katika hoteli moja ya Dubai mwezi uliopita-hii ni kwa muujibu alivyoliambia shirika la habari la AFP , mkuu wa polisi Dahi Khalfan.Alisema kuwa, kuna shaka shaka nyingi kuwa mmoja kati ya wapalestina hao 2 alikutana na mmoja wa timu hiyo ya wauaji kabla ya kitendo chenyewe kufanyika.

Khalfan alitangaza juzi Jumatatu kuwa ,Polisi ya Dubai, inawasaka watu 6 walioingia Dubai na paspoti za Uingereza,watatu wengine wenye pasi za Ireland,miongoni mwao mwanamke mmoja na mmoja mwenye pasi ya kijerumani na mwengine mwenye pasi ya Ufaransa.Wote hao waliweza kuondoka Umoja wa Falme za Kiarabu baada ya mkasa huo.

Maafisa wa Uingereza,Ireland na Ufaransa, waliarifu hapo jana kuwa pasi hizo ni feki au za udanganyifu.Vyombo vya habari vya Israel, vimetangaza kwamba kiasi ya waisraeli 6 wenye uraia wa nchi 2-Uingereza na Israel wamo katika orodha ya kundi hilo la watu 11.

Mjini Dublin,msemaji wa wizara ya nje amesema pasi hizo zinazosemekana kuwa za Ireland si za kweli. Akaongeza kusema kwamba, wamechunguza nambari za pasi na majina na kugundua hakuna pasi za majina hayo wala nambari hizo.

Msemaji wa wizara ya nje ya Ufaransa, Bernard Valero, ameliambia shirika la habari la AFP baada ya uchunguzi kufanywa kuwa wamegundua hata pasi ya kifaransa iliotumika si ya kweli.

Nchini Israel, kituo cha TV cha Channel 10 kimearifu kwamba ,waisraeli 6 na muisraeli mwenye uraia wa kijerumani wamekuwa wahanga wa njama hiyo.Kituo cha TV cha channel 2, kimetaja waisraeli 4 tu wenye uraia wa nchi 2 na kwamba picha zao tu zimebadilishwa.

Chama cha wapalestina cha HAMAS kinachotawala mwambao wa Gaza ,kimeituhumu Israel ndio iliomuua bw.Mahmud Mabhuh,aliekuwa na umri wa miaka 50 na kikaahidi kulipiza kisasi.

Wanachama wa HAMAS wamearifu kwamba, Mabhuh aliepiga maskani yake mjini Damascus,Syria, alikuwa ziarani huko Dubai kwa madhumuni ya kununua silaha kwa ajili ya tawi la kijeshi la chama cha HAMAS ambalo yeye ndie aliolianzisha.

Juzi Jumatatu, msemaji wa kikosi cha polisi cha Mamlaka ya ndani ya Palestina,jamadari Adnan al-Dameeri, aliliambia shirika la habari la AFP huko Ramallah kuwa, wakuu wa usalama wa kipalestina wamethibitisha taarifa kuwa maafisa 2 wa Hamas, walihusika na mauaji ya Mahmud Mabhuh.

Wauaji wa Mabhuh, waliondoka Dubai masaa tu baada ya mauaji baada ya kupitisha masaa 24 tu huko Dubai na hawakutumia silaha yoyote,wala (credit cards ) au simu za Dubai wakati walipokuwa huko.Picha za timu hiyo ya wauaji 11 zilioneshwa baada ya kuchukuliwa na kamera za upelelzi.

Israel yakanusha kuhusika na mauaji ya kiongozi wa Hamas

Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Israel, Avigdor Lieberman amekanusha taarifa kuwa shirika la upelelezi la Israel la Mossad lilihusika katika mauaji ya kiongozi wa ngazi ya juu wa kundi la Hamas, Mahmoud al-Mahbouh. Avigdor amesema kuhusishwa kwa Waisraeli waliozaliwa nje ya nchi yao katika mauaji hayo haidhihirishi kwamba Mossad ndiyo ilitekeleza mauaji hayo.

Akizungumza leo kwa mara ya kwanza kujibu tuhuma hizo, Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Israel, Avigdor Lieberman, alisema siyo jambo sahihi kuhisi kuwa Israel inahusika na mauaji ya Mahmoud al-Mahbouh yaliyofanyika mwezi uliopita katika hoteli moja huko Dubai. Amesema hakuna haja ya kudhania kwamba Mossad ndiyo ilihusika na mauaji hayo na sio shirika lingine la kijasusi au nchi nyingine. Akizungumza katika Radio ya Jeshi la Israel, waziri Lieberman amesema hajui ni kwa nini Israel inahusishwa na mauaji hayo, ilhali pasi za kusafiria zilizotumiwa na wahalifu hao zilikuwa ni bandia.

Polisi katika Umoja wa Falme za Kiarabu imewataja watu 11 walioingia Dubai wakiwa na uraia wa nchi za Ulaya kama watuhumiwa wa mauaji hayo. Miongoni mwao wakiwemo raia watatau wa Ireland na sita wakiwa ni raia wa Uingereza waliohamia Israel. Pia yumo mwanamke mmoja na mwingine alikuwa na pasi ya kusafiria ya Ujerumani na mwingine ya Ufaransa. Lakini serikali za mataifa hayo zimesema hazikutoa pasi za kusafiria zenye udanganyifu. Wanaume wawili raia wa Uingereza ambao wamekuwa wakiishi Israel kwa miaka kadhaa wameripotiwa kushtushwa na utumiwaji wa majina yao.

Wasemavyo wachambuzi

Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya upelelezi nchini Israel wamesema kuwa shirika la Mossad litakuwa limevurunda kama kweli linahusika na mauaji hayo na kufanya ushiriki wake kuwa wa siri kwa kuwatumia watu ambao wanaweza wakatafutwa na kupatikana nchini Israel. Kundi la Hamas la Palestina limeishutumu Israel kwa kuhusika na mauaji hayo na polisi wa Dubai wamesema hawawezi kuthibitisha ushiriki wa Israel katika mauaji hayo. Mkuu wa polisi wa Dubai, Luteni Kanali Dhafi Khalfani Tamim amesema majina ya watuhumiwa hao yamepelekwa kwa polisi wa kimataifa-Interpol, ili hati ya kimataifa ya kukamatwa kwao iweze kutolewa. Chanzo cha habari cha serikali kimeeleza kuwa watu wengine sita ambao bado hawajatambuliwa wanadaiwa kuhusika katika mauaji hayo.

Al-Mahbouh, mwenye umri wa miaka 50 ambaye pia ni mmoja wa waanzilishi wa tawi la kijeshi la Hamas la al-Qassam Brigades, alikutwa amekufa katika chumba chake hotelini Januari 20, mwaka huu siku moja baada ya kuwasili Dubai. Chanzo cha habari cha usalama nchini Israel kimeeleza kuwa Al-Mahbouh alikuwa akishutumiwa kuhusika na uuzaji kimagendo silaha zilizofadhiliwa na Iran kwenda kwenye eneo la wanamgambo wa Kiislamu katika Ukanda wa Gaza.

Tags:

0 comments

Post a Comment