Subscribe to receive latest Updates

Online :

You Are Here: Home - - this is total utapeli. No sio utapeli ni unyang'anyi. No sio unyang'anyi ni ufisadi? watoroka na computer kadhaa na fedha zisizopungua milioni moja.

IDADI YA WATU WALIOSOMA HABARI HII: counter tuma maoni yako kutokana na unyang'anyi huu katika hali isiyokuwa ya kawaida, baada ya bodi ya mikopo kudokeza bila kutaja majina kuwa kuna baadhi ya wanafunzi vyuo vikuu mbalimbali ndani na nje ya nchi ama wamegushi vyeti au wamepata mkopo au kujiunga na vyuo vikuu kwa njia zisizo za halali ikiwa ni pamoja na kukwepa adhabu zilizowekwa baada ya mwanafunzi ama kurudia mwaka wa masomo (ku-discore) au kufukuzwa vyuo vikuu,mambo yamekuwa sio mambo katika CHUO KIKUU CHA URAFIKI LUMUMBA baada ya wanafunzi mbalimbali kudaiwa kutoroka na mali za wanafunzi wengine ikiwa ni pamoja na fedha taslim (yaani dola). taarifa zilizoifikia The THOMCOM zinasema kuwa baadhi ya wanafunzi walifikia hatua hata ya kujaribu kuwazuia aeroport watekaji nyara hao wa mali za watu bila mafanikio. Baadhi ya mali ambazo zilithobitishwa na The THOMCOM kuchukuliwa ni pamoja na COMPUTER NYEPESI (laptop) na fedha taslim zenye dhamani ya zaidi ya milioni moja. Tabia ya kuazimana computer nyepesi yaani laptop imekuwa ni ya kawaida kwa wanafunzi vyuoni, kitu ambacho wanafunzi hao FEKI walitumia mwanya huo kuazima computer hizo kwa matumizi ya kawaida na kuangalia movie siku moja kabla ya kuondoka kwao. haikufaamika mara moja kama watuhumiwa hao waliondoka kwa pamoja au kila mmoja kwa nafasi yake. Wanafunzi wanashauriwa kuepuka kukopesha au kuazima mali nyepesi na za dhamani hasa kwa muda huu ili kuepuka adha ya kuchukuliwa mali au kutokomea na deni.....
Tags:

0 comments

Post a Comment