Wapinzani wa muswada huo wanasema sheria hiyo mpya inayopendekezwa inatishia usalama wa kujieleza na inakiuka katiba.
Askofu Mkuu Desmond Tutu ameielezea sheria hiyo kuwa haifai na ni matusi kwa wananchi wa Afrika Kusini.
Hata hivyo chama tawala cha African National Congress, ANC, kimesisitiza kuwa sheria hiyo inahitajika kulinda usalama wa taifa.
Muswada huo bado unahitaji kupitishwa na baraza la juu la bunge na Rais Jacob Zuma ili kuwa sheria.

0 comments