Subscribe to receive latest Updates

Online :

You Are Here: Home - - Wanafunzi 10 wafukuzwa shule. wanafunzi wengine 76 kufukuzwa chuo kwa kula ada ya mwaka 2008/2009. notisi ya siku 15 yatolewa.

IDADI YA WATU WALIOSOMA HABARI HII: counter Wnafunzi 10 wa chuo kikuu cha urafiki Lumumba wamekumbana na panga la mwaka huu kwa kufukuzwa chuo kutokana na sababu tofautitofauti. wanafunzi hao (majina tunayo) watano wa mwaka wa kwanza, wanne wa mwaka wa pili na mmoja wa mwaka wa nne wanasona vitivo vya Utalii, injinia, computer sayansi, medisini, uchumi na linguistic.
Habari nyingine iliyoifikia THE THOMCOM Inc. inasema kwamba chuo kikuu cha urafiki Lumumba (Moscow Russia) kimeapa kuwatimua chuo wanafunzi 76 watanzania watfukuzwa shule ifikapo tarehe 15/12/2009 kama wanafunzi hao watakuwa hawajalipa ada ya mwaka uliopita. Uongozi wa chuo umesema enzi za kuwadekeza watanzia zimekwisha na sasa wanafunzi wote wataadhibiwa kwa usawa. Akiongea na THE THOMCOM Inc. Mkuu wa kitengo cha ushirikiano wa kimataifa amesema chuo kinawadai watanzania hao dola za kimarekani 120 387.69 Notisi ya kuwafukuza chuo wanafunzi hao kwa kula ada imetolewa na Denisenko V.N. ambaye ni msaidizi wa mkuu wa chuo kwa maswala ya ushiriano wa kimataifa na kusainiwa na mkuu wa chuo Akademiki Filippov V.M.
Imeandaliwa na kutolewa na mwandishi wetu
Tags:

0 comments

Post a Comment